n00b
JF-Expert Member
- Apr 10, 2008
- 1,006
- 2,667
Japo nimeiweka kama tetesi lakini muda wowote atakuwa kaingia Dodoma na tutarajie lolote. Safari hii hakuna cha "Wazee wa Dar".
Nitakuja na updates baadae kidogo
Updates:
Nitakuja na updates baadae kidogo
Updates:
More updates baadae.JK amewasili Dodoma lakini ngoma bado nzito. Katibu wa CCM, Wilson Mukama naye amefika Dodoma. Hakuna kujiuzulu, ngoma bila bila. Taratibu za CCM, hakuna atakeyejiuzulu, Kamati ya wabunge CCM ilichemka kuwalazimisha mawaziri wanane kujiuzulu, wamekuza sana na kupoteza seriousnes, ikaonekana kila mtu aliamua kutumia nafasi hiyo kwa maslahi ya kisiasa na baadhi wanaonekana kama wanatafuta nafasi za uwaziri.
Kwa ufupi JK ameona pia kwamba huo ni mtego kwake na kwamba wanakoelekea wanataka 'kichwa' chake na si Pinda wala mawaziri, huo ni mwanzo tu. Kwa sasa mawaziri wachache sana kati ya wanane waliandika barua za kujiuzulu, wengi waliandika maelezo ya kujitetea na kutaka Rais awaondoe ikiwa atabaini walikosea katika uwajibikaji wao. Wametoa nafasi ya kuchunguzwa.
JK anaondoka kesho kueelekea Dar na baadae Malawi kwenye mazishi.