MAGEUZI KWELI
JF-Expert Member
- Jul 16, 2011
- 1,947
- 253
Jamani nimejiuliza kidogo, Rais wetu mpendwa sana Mtukufu JK amezindua kampeni za kupanda mlima kilimanjaro kuhimiza utokomezaji wa adhabu za watoto na wamama,
Nimekubaliana na kampeni za kupambana na tohara za watoto na wakinana kupata mikong'oto.Swali ambali sijapata jibu,
Swali, Hivi umati huu wooote ulioenda kupanda mlima kilimanjaro, ujumbe wake unamfikia je ngariba aliyepo kijijini ambaye hata kiswahili hakijui?Au je mmng'ati wa Balangda atajua je kampeni zilizozinduliwa na JK huko marangu wakati Radio haijui na tv haijui?
Hivi kama serikali ingekuwa imeazimia kupambana na janga hili, hao waliokuja woooote si wangeenda kwenye vijiji ambavyo majanga haya hutokea ili kuongea na wananchi??
Sasa mimi sijaelewa jamii inayolengwa itapata je ujumbe kwa kadamnasi iliyokuja toka nchi 35 na sijui kama si wamekuja kutalii kusingizia mapambano ya tohara na ubakaji na mengine kama hayo.
Ni upeo wangu jamani ila kama kuna anayeweza nieleza kwa undani nikaelewa vema, basi na iwe hivyo.
Sintashangaa siku moja wakaja wengine kupanda mlima kupambana na ngono zembe na kuhimiza ngono salama na Condom. it can be possible
Nimekubaliana na kampeni za kupambana na tohara za watoto na wakinana kupata mikong'oto.Swali ambali sijapata jibu,
Swali, Hivi umati huu wooote ulioenda kupanda mlima kilimanjaro, ujumbe wake unamfikia je ngariba aliyepo kijijini ambaye hata kiswahili hakijui?Au je mmng'ati wa Balangda atajua je kampeni zilizozinduliwa na JK huko marangu wakati Radio haijui na tv haijui?
Hivi kama serikali ingekuwa imeazimia kupambana na janga hili, hao waliokuja woooote si wangeenda kwenye vijiji ambavyo majanga haya hutokea ili kuongea na wananchi??
Sasa mimi sijaelewa jamii inayolengwa itapata je ujumbe kwa kadamnasi iliyokuja toka nchi 35 na sijui kama si wamekuja kutalii kusingizia mapambano ya tohara na ubakaji na mengine kama hayo.
Ni upeo wangu jamani ila kama kuna anayeweza nieleza kwa undani nikaelewa vema, basi na iwe hivyo.
Sintashangaa siku moja wakaja wengine kupanda mlima kupambana na ngono zembe na kuhimiza ngono salama na Condom. it can be possible