JK: Kupanda mlima kilimanjaro ili utokomeze maonevu ya watoto na wanawake ipo sawa?

MAGEUZI KWELI

JF-Expert Member
Jul 16, 2011
1,947
253
Jamani nimejiuliza kidogo, Rais wetu mpendwa sana Mtukufu JK amezindua kampeni za kupanda mlima kilimanjaro kuhimiza utokomezaji wa adhabu za watoto na wamama,
Nimekubaliana na kampeni za kupambana na tohara za watoto na wakinana kupata mikong'oto.Swali ambali sijapata jibu,
Swali, Hivi umati huu wooote ulioenda kupanda mlima kilimanjaro, ujumbe wake unamfikia je ngariba aliyepo kijijini ambaye hata kiswahili hakijui?Au je mmng'ati wa Balangda atajua je kampeni zilizozinduliwa na JK huko marangu wakati Radio haijui na tv haijui?
Hivi kama serikali ingekuwa imeazimia kupambana na janga hili, hao waliokuja woooote si wangeenda kwenye vijiji ambavyo majanga haya hutokea ili kuongea na wananchi??
Sasa mimi sijaelewa jamii inayolengwa itapata je ujumbe kwa kadamnasi iliyokuja toka nchi 35 na sijui kama si wamekuja kutalii kusingizia mapambano ya tohara na ubakaji na mengine kama hayo.
Ni upeo wangu jamani ila kama kuna anayeweza nieleza kwa undani nikaelewa vema, basi na iwe hivyo.
Sintashangaa siku moja wakaja wengine kupanda mlima kupambana na ngono zembe na kuhimiza ngono salama na Condom. it can be possible
 
Ukitaka kutokomeza uonovu kwa watoto, wamama, wababa, vijana, paka, kuku, vikapu etc unatunga sheria na kuisamia hiyo sheria kwa nguvu zote. Kupanda mlima ni utalii. period. Wakati umefika kwa viongozi wetu including rais kuacha kutuchezea akili na hoja za kikoloni. Tumesumbuliwa sana na kelele na 'malaria no more' na sasa wanahamia kwenye kupanda mlima, what next? Kama mtu anataka kupanda mlima Kilimanjaro na afanye hivyo lakini kwa hakika hakuna litakalo badilika kuhusu uonovu/ukatili ndani ya jamii.
 
Wacha ujinga wewe mleta mada. Unawafanya Musoma hawajui Kiswahili. Nyerere alitokea maeneo hayo hayo na alipokuja Dar kaja kiswahili anakijuwa. Ni nani alimfundisha? Wewe? Wacha dharau. Na hao wamasai wacha radio, wana madishi ya satalaiti ambayo hata wewe huna. Wacha kutukana watu kirejareja.
 
Wacha ujinga wewe mleta mada. Unawafanya Musoma hawajui Kiswahili. Nyerere alitokea maeneo hayo hayo na alipokuja Dar kaja kiswahili anakijuwa. Ni nani alimfundisha? Wewe? Wacha dharau. Na hao wamasai wacha radio, wana madishi ya satalaiti ambayo hata wewe huna. Wacha kutukana watu kirejareja.
Kama vyote vingekuwa vimeenea kwa jamii hiyo unayoisemea, them Tanzania ni nchi imeendelea sana basi, Every where people they knows what is happening around,Punguza jazba, Mangariba Musoma huko wanafanya Sherehe na kila mtu anajua, Wamasai nalo usikatae wamama wanakatwa (Emouo)Kupunguza makali ya msisimko, Unadhani nimeandika kitu nisichikijua? By the way, nalo uliloandika ni comment pia na ni accepted.
 
Atakuwa ndiye Rais wa kwanza wa Tanzania akiwa madarakani kupanda mlima kilimanjaro inapendeza kama njia ya kukuza na kutangaza utalii wa mlima kilimanjaro. Picha za Rais zikitumika kama nembo ya kuutangaza mlima huo itakuwa mojawapo ya njia ya kuvuatia utalii
 
Nyerere alipopandisha koroboi juu ya mlima k'njaro limulike nchi nzima haikuwa na shida,kweli nimeamini kunya anye kuku akinya bata 'anendesha'.
 
Jamani nimejiuliza kidogo, Rais wetu mpendwa sana Mtukufu JK amezindua kampeni za kupanda mlima kilimanjaro kuhimiza utokomezaji wa adhabu za watoto na wamama,
Nimekubaliana na kampeni za kupambana na tohara za watoto na wakinana kupata mikong'oto.Swali ambali sijapata jibu,
Swali, Hivi umati huu wooote ulioenda kupanda mlima kilimanjaro, ujumbe wake unamfikia je ngariba aliyepo musoma ambaye hata kiswahili hakijui?Au je mmasai wa Oldonyo lengai atajua je kampeni zilizozinduliwa na JK huko marangu wakati Radio haijui na tv haijui?
Hivi kama serikali ingekuwa imeazimia kupambana na janga hili, hao waliokuja woooote si wangeenda kwenye vijiji ambavyo majanga haya hutokea ili kuongea na wananchi??
Sasa mimi sijaelewa jamii inayolengwa itapata je ujumbe kwa kadamnasi iliyokuja toka nchi 35 na sijui kama si wamekuja kutalii kusingizia mapambano ya tohara na ubakaji na mengine kama hayo.
Ni upeo wangu jamani ila kama kuna anayeweza nieleza kwa undani nikaelewa vema, basi na iwe hivyo.
Sintashangaa siku moja wakaja wengine kupanda mlima kupambana na ngono zembe na kuhimiza ngono salama na Condom. it can be possible
Sioni tatizo kutumia Mlima Kilimanjaro au popote kama ishara ya uzinduzi. Kwa upande mwengine wamechagua pahali muafaka kama palivyochaguliwa "kuangaza nuru ya uhuru na ukombozi wa Afrika nzima", pamoja na kutangaza utalii. Hilo halinipi wasiwasi, wasiwasi wangu ni uendelezaji wa hizo kampeni na harakati; wasiwasi wa kuwa zimeanza hapo na zitaishia hapo hapo, kama ambavyo tumezowea kufanya Tanzani. Unakumbuka "Fagio la Chuma" lililokuwa alama ya kupambana na rushwa? Rushwa imezidi na hakuna kinachoendelea.

Tunachotakiwa kufanya, pamoja na nia zuri ya uzinduzi huu, ni pamoja na uelimishaj jamii na ufuatiliaji wa dhamira yenyewe, pamoja na kutunga sheria na kuzisimamia.
 
Mkuu analysis kama hizi za kisomi uwa watawala wetu hawaelewi..waache wapande mlima na kushuka wakati haina madhara chanya ya moja kwa moja kwa wanaofanya hivi vitendo.
 
Jamani nimejiuliza kidogo, Rais wetu mpendwa sana Mtukufu JK amezindua kampeni za kupanda mlima kilimanjaro kuhimiza utokomezaji wa adhabu za watoto na wamama,
Nimekubaliana na kampeni za kupambana na tohara za watoto na wakinana kupata mikong'oto.Swali ambali sijapata jibu,
Swali, Hivi umati huu wooote ulioenda kupanda mlima kilimanjaro, ujumbe wake unamfikia je ngariba aliyepo musoma ambaye hata kiswahili hakijui?Au je mmasai wa Oldonyo lengai atajua je kampeni zilizozinduliwa na JK huko marangu wakati Radio haijui na tv haijui?
Hivi kama serikali ingekuwa imeazimia kupambana na janga hili, hao waliokuja woooote si wangeenda kwenye vijiji ambavyo majanga haya hutokea ili kuongea na wananchi??
Sasa mimi sijaelewa jamii inayolengwa itapata je ujumbe kwa kadamnasi iliyokuja toka nchi 35 na sijui kama si wamekuja kutalii kusingizia mapambano ya tohara na ubakaji na mengine kama hayo.
Ni upeo wangu jamani ila kama kuna anayeweza nieleza kwa undani nikaelewa vema, basi na iwe hivyo.
Sintashangaa siku moja wakaja wengine kupanda mlima kupambana na ngono zembe na kuhimiza ngono salama na Condom. it can be possible

We Kijana shika adabu zako, nani kakwambia Musoma hatujui kishwahili?? Wewe hujui huyo aliyekikuza na kukilea kiswahili hadi kikaongewa nchi nzima alikuwa mwana wa Musoma??!!! Anyway we don't take any pride with that language of ubwabwa
 
Back
Top Bottom