JK hawajui wamiliki wa Dowans, Ngeleja anawajua

Manyanza

JF-Expert Member
Nov 4, 2010
9,485
14,353
Mbunge wa Kigoma Kusini kwa tiketi ya NCCR- Mageuzi, David Kafulila, alimshangaa Rais Kikwete kusema hawajui wamiliki wa Dowans wakati waziri wake Ngeleja alikwishawataja.

“Ngeleja alikwishawataja wamiliki wa Dowans, inakuwaje Rais anasema hawafahamu..., suala hili linazidi kuwachanganya wananchi, inabidi likajadiliwe bungeni,”alirejea msimamo wa hoja yake anayotarajia kuiwasilisha bungeni kama ikikubaliwa.

Kafulila alifafanua kwamba, suala hilo likijadiliwa bungeni ndipo linaweza kutoa majibu sahihi kwa wananchi.

“Kwa ujumla Rais Kikwete kusema hawajui wamiliki wa Dowans ni kielelezo kuwa wale tuliotangaziwa na Waziri Ngeleja sio wenyewe kwani wangekuwa wamiliki Rais angewajua,” alisema Kafulila na kuongeza:

Je waziri wake na Mwanasheria Mkuu wa Serikali waliposema lazima tulipe Dowans hawakumwambia wanamlipa nani?

Alisema katika sakata hili ataendelea kupigana hadi ijulikane nani amefikisha taifa katika hali hii. “Serikali ilipe isilipe ni lazima iwajibike maana hoja ya msingi hapa tumefikishwaje hapa hadi kushindwa kesi,” alihoji Kafulila
 
Mbunge wa Kigoma Kusini kwa tiketi ya NCCR- Mageuzi, David Kafulila, alimshangaa Rais Kikwete kusema hawajui wamiliki wa Dowans wakati waziri wake Ngeleja alikwishawataja.

"Ngeleja alikwishawataja wamiliki wa Dowans, inakuwaje Rais anasema hawafahamu..., suala hili linazidi kuwachanganya wananchi, inabidi likajadiliwe bungeni,"alirejea msimamo wa hoja yake anayotarajia kuiwasilisha bungeni kama ikikubaliwa.

Kafulila alifafanua kwamba, suala hilo likijadiliwa bungeni ndipo linaweza kutoa majibu sahihi kwa wananchi.

"Kwa ujumla Rais Kikwete kusema hawajui wamiliki wa Dowans ni kielelezo kuwa wale tuliotangaziwa na Waziri Ngeleja sio wenyewe kwani wangekuwa wamiliki Rais angewajua," alisema Kafulila na kuongeza:

Je waziri wake na Mwanasheria Mkuu wa Serikali waliposema lazima tulipe Dowans hawakumwambia wanamlipa nani?

Alisema katika sakata hili ataendelea kupigana hadi ijulikane nani amefikisha taifa katika hali hii. "Serikali ilipe isilipe ni lazima iwajibike maana hoja ya msingi hapa tumefikishwaje hapa hadi kushindwa kesi," alihoji Kafulila

Hapo kwenye red, ina maana Ngereja alikuwa anaropoka tu? au yalikuwa mawazo yake binafsi? na mwanasheria mkuu wa serikali aliposema kuwa suala la kuilipa Dowans haliepukiki alikuwa inamaanisha kua wamiliki wa Dowans anawafahamu.... inakuwaje bosi wao ambaye amewaajiri anasema hawatambui wamiliki wa Dowans??
 
JK anathubutu leo hii kutundanganya ilihali yeye na lowasa na msabaha/karamangi walifanikisha richmond kupewa zabuni.je wa RIChMOND anawajua?????????????????????????? Haya yote yana mwisho...............wataficha weeeeeeeeeeee mwishowe watatajana tu.
 
Ngoma karibia inapasuka.......Unajua Ngoma ikianza hulia kidogo kidogo kwa sauti nene kisha sauti hupaa sana lakini ikikaribia kuisha au kuzima ladha yake hupotea....'' LAZA YA VIONGOZI WETU HAWA WA CHAMA CHA KUPINDUA IMEPOTEA '' Sasa hivi ni unafiki tu ndio unaendelea....JK kasoma ramani akagundua ya Tunisia na Misri yanawza kumtokea sasa anaona azuge!!!!!!!!!!!!!!! Kweli ameshikwa pabaya safari hii
 
Hiki ni kichekesho cha mwaka. Nashindwa kuelewa hii ni dharau au ninini!

Haiingii hakilini hatakidogo, huyu jamaa kutowajua wamiliki wa DOWANS ni

kichekesho tena Dharau kubwa sana kwa watanzania.

Ikiwa mtu kama yeye mwenye mamlaka juu ya vyombo vya ulinzi na

usalama anashindwa kutambua watu wanaoitia hasara nchi na kuhujumu

uchumi, itakuwaje kwa watendaji wa chini yake au mwananchi wa

kawaida?

Kama hawajui wenye kampuni hiyo, je,hiyo mikataba ilisainiwa online?

Kama hawajulikani, hiyo kesi ilifunguliwa na akina nani kama sio watu?

Je, hayo malipo wanayotaka kufanya nani analipwa? je hizo hundi hazi sainiwi?na kama zinasainiwa ninani wanaosaini?


OK, mzee yawezekana huwajui hao wenye kampuni, pengine hutaki! Je,

wabongo wenzio waliosaini hiyo mikataba feki nao huwajui? Pengine wewe

ulikuwa umelala wakati huo, sasa umeamshwa, je, umefanya bidii yoyote

kuwatafuta na kuwachukulia hatua?


Hii ni daliii iliyo wazi kabisa Viongozi wetu hawakio serious na mambo ya nchi wako serious zaidi na matumbo yao!


Majibu ya Muheshimiwa kutowafahamum wamiliki wa DOWANS ni dharau kwa Watanzania.

Kwa kauli hii sinashaka kuwa yeye pia anahusika na umiliki wa DOWANS
 
Hapo ndio mjue mnaongozwa na Raisi ambaye akili yake inawaza kwenda kukaa Bilila Serengeti au kwenda kula kuku majuu
 
Mbunge wa Kigoma Kusini kwa tiketi ya NCCR- Mageuzi, David Kafulila, alimshangaa Rais Kikwete kusema hawajui wamiliki wa Dowans wakati waziri wake Ngeleja alikwishawataja.

"Ngeleja alikwishawataja wamiliki wa Dowans, inakuwaje Rais anasema hawafahamu..., ..........

Jamani jamani TZ, hivi JK ana wasaidizi kweli? Aidha Ni wazi kuwa maelezo ya JKaliyotoa kule DOM wakati wa maadhimisho ya miaka 34 ya CCM kama sijakosea yanatokana na utashi wake na si swala ambalo amekaa na wenzake na kulijadili. Inanipelekea kuamini kuwa raisi hana wasaidizi wazuri au ashauriki, napenda kuamini la kwanza kuwa hana wasaidizi wazuri au tuseme wasaizidi wake ni wanafiki wakubwa.

Kwanini nasema haya moja kama wasaidizi wangekuwa makini wangeshamshauri raisi kutoa kauli muda mrefu sana juu ya sakata ya DOWANS. Kuchelewa huko kunanifanya niamini kuwa si watu makini hata kidogo. Naamini kutokana na hilo JK imebidi ajitose na kuliongelea swala hilo mwenyewe bila kushauriwa vizuri na wenzake. Kitendo cha JK kuongelea swala hilo kwangu limezua mengi kuliko ilivyokuwa kabla ya kauli yake ambayo kimsingi haikuwa na nguvu sana.

Yanayonipa shida ni haya; Hivi raisi alitoa maelezo yale kama raisi wa nchi, M/Kiti wa CCM au JK mtu binafsi? Kwamba hawajui DOWANAS na hakuna wanachohitaji toka kwake! Hivi DOWANS ilipoingia hiyo mikataba ya Ki-Karl Peters wizara ya Nishati na Madini ilihusika au la? Kama ilihusika, wizara hiyo si iko kwa mamlaka ya raisi? Je kuna possibility kwamba hiyo mikataba ilifika ktka baraza la mawaziri? Hivi riasi si ndiye mwenyekiti wa baraza hilo? (I stand to be corrected). Kwa hiyo kama mikataba hiyo ilifika wizarani basi technically JK anawafahamu DOWANS kwa maana ya kitaasisi ya uraisi!! Kwa hiyo akikataa kuwa hawafahamu basi kuna udhaifu mkubwa sana hapo wa kiuongozi

What if JK alitoa maelezo yale kama mtu binafsi ya kwamba hanawafahamu DOWANS? Hapo patakuwa na upungufu mkubwa sana ki-uongozi because JK kama president ni kiongozi wa serikali/nchi he is expected to be on-top. Nasema ni upungufu wa kiuongozi kwani alipashwa kujua kutoka kwa wenzake.Kwa kutokana na kutofanya hivyo amejikuta (sijui kama analifahamu hili) akijitoa kama kiongozi wa nchi kwa kusema hawajui DOWANS. Kama kauli ya JK ni ya kweli toka moyoni kwake basi hii ina maana moja tu kuwa si yeye anayeongoza (technically) hii nchi ya TZ na kwamba yuko tu as a symbol of presidency.
 
Naungana na Dr. Slaa kupinga kauli ya rais wetu kuwa hamjui nani mmiliki wa Dowans. Wakati anapitisha azimio na baraza lake la mawaziri kuipa Dowans mkataba wa Richmond, hakujua alikuwa anampa nani?

Ni Kikwete huyu aliyetumia pesa nyingi tu kumfuatilia mmiliki wa ze utamu, anashindwa nini kumfuatilia mmiliki wa Dowans?
 
Tena huwa wanakuwa naye lkulu mara nyingi tu, ni mtu wake wa karibu aliyemsaidia sana kugharamia kampeni zake.
 
Tena huwa wanakuwa naye lkulu mara nyingi tu, ni mtu wake wa karibu aliyemsaidia sana kugharamia kampeni zake.

Asimjue vipi rafiki yake kipenzi,wanaswali wote msikiti mmoja,siku nguvu ya umma itakapo mtoa ikulu atakwenda kuishi kwa ndugu wa rafiki yake huyo huko iran,ili aende hija kiurahisi pale makka.....anyway nimenuna kwa kauli hizi za kipuuzi ndio maana hata mm nimeamua kumpa kavu.
 
Tena huwa wanakuwa naye lkulu mara nyingi tu, ni mtu wake wa karibu aliyemsaidia sana kugharamia kampeni zake.

guud point dada! Ni mwendawazimu pekee ndiye anayeweza kusema JK hamjui mmiliki wa DOWANS, kwanza katika hotuba yake alikuwa na tones za hofu hofu hivi kutamka maneno hayo, kigugumizi kama wakati Mtume Petro alipomkana Yesu na kusema yeye si Mgalilaya na hamjui Yesu.

tieni akili kichwani. JK is only buying, playing and passing time!
 
hilo linajulikana hawa ni mafisadi kuanzia magogoni hadi china na kila mtu ana njia zaake za kuiba.
mf kikwete yeye ni mwizi wa kutupwa ila yeye anamtumia rz1 na wanakwapua kweeeeeeeeeeeli
mjomba ben aliiba kivyake.na mwinyi alimtumia mke mdogo kuiba mali za umma ila na yeye pia
aliibiwa na huyo mke wa kiarabu.jomba ben walikutana majizi yote yeye anakwiba na mke kivyake
hii nchi inaliwa na wajanja bana.ukiwa kule halali chukua chako mapema na ukaishi upendavyo.
na ni maisha bora kwa kila fisadi.je watanzania tutaibiwa mpaka lini?

duuuuuuuuuuuuh INAUMA!
 
Anafahamu sana sema anaogopa kuropoka mana watamtaja na yeye akiropoka tu.
 
Mbona sikuelewi nini chazo chako cha habari hizo si vizuri kuja hapa na kulipuka tu kikwete mwizi kaiba nini.
 
Nyie hamkumuona mwenye dowans? Au mnataka rais aseme nn basi dowans ni yangu msinilipe.
 
Back
Top Bottom