Manyanza
JF-Expert Member
- Nov 4, 2010
- 9,485
- 14,353
Mbunge wa Kigoma Kusini kwa tiketi ya NCCR- Mageuzi, David Kafulila, alimshangaa Rais Kikwete kusema hawajui wamiliki wa Dowans wakati waziri wake Ngeleja alikwishawataja.
Ngeleja alikwishawataja wamiliki wa Dowans, inakuwaje Rais anasema hawafahamu..., suala hili linazidi kuwachanganya wananchi, inabidi likajadiliwe bungeni,alirejea msimamo wa hoja yake anayotarajia kuiwasilisha bungeni kama ikikubaliwa.
Kafulila alifafanua kwamba, suala hilo likijadiliwa bungeni ndipo linaweza kutoa majibu sahihi kwa wananchi.
Kwa ujumla Rais Kikwete kusema hawajui wamiliki wa Dowans ni kielelezo kuwa wale tuliotangaziwa na Waziri Ngeleja sio wenyewe kwani wangekuwa wamiliki Rais angewajua, alisema Kafulila na kuongeza:
Je waziri wake na Mwanasheria Mkuu wa Serikali waliposema lazima tulipe Dowans hawakumwambia wanamlipa nani?
Alisema katika sakata hili ataendelea kupigana hadi ijulikane nani amefikisha taifa katika hali hii. Serikali ilipe isilipe ni lazima iwajibike maana hoja ya msingi hapa tumefikishwaje hapa hadi kushindwa kesi, alihoji Kafulila
Ngeleja alikwishawataja wamiliki wa Dowans, inakuwaje Rais anasema hawafahamu..., suala hili linazidi kuwachanganya wananchi, inabidi likajadiliwe bungeni,alirejea msimamo wa hoja yake anayotarajia kuiwasilisha bungeni kama ikikubaliwa.
Kafulila alifafanua kwamba, suala hilo likijadiliwa bungeni ndipo linaweza kutoa majibu sahihi kwa wananchi.
Kwa ujumla Rais Kikwete kusema hawajui wamiliki wa Dowans ni kielelezo kuwa wale tuliotangaziwa na Waziri Ngeleja sio wenyewe kwani wangekuwa wamiliki Rais angewajua, alisema Kafulila na kuongeza:
Je waziri wake na Mwanasheria Mkuu wa Serikali waliposema lazima tulipe Dowans hawakumwambia wanamlipa nani?
Alisema katika sakata hili ataendelea kupigana hadi ijulikane nani amefikisha taifa katika hali hii. Serikali ilipe isilipe ni lazima iwajibike maana hoja ya msingi hapa tumefikishwaje hapa hadi kushindwa kesi, alihoji Kafulila