Jk azidi kuandika historia

du! watu wagumu humu,mi nasema mnyonge mnyongeni lkn haki yake mpeni
 

Usidanganye watu wenye akili. JK hakuwahi kuwa na nia ya kuwapeleka watuhumiwa wa EPA na wengineo mahakamani, alilazimishwa na wafadhili baada ya tuhuma nyingi kuwekwa wazi na Wapinzani, hasa Dr. Slaa. Kwa sababu ya kubanwa na wafadhili, na kuwepo hatari ya kunyimwa misaada ndipo alipotaka kuonesha kuwa amefanya kitu, lakini bado alifanya kwa uangalifu mkubwa kuhakikisha anaendelea kuwalinda mafisadi wakubwa kama KAGODA, DEEP GREEN, MEREMETA na TANGOLD.

Watu ambao wanastahili kusifiwa sana angalao kwa hukumu kama hizi ni Dr. Slaa na wanahabari (siyo wa mtanzania, uhuru, Habari Leo na Daily News) ambao pamoja na kupingwa sana na serikali na CCM walisimama imara kufichua kwa uwazi tuhuma hizi na nyingine ambao mpaka leo si JK wala CCM waliowahi kuchukua hatua.

KAGODA iliyochota 40 bilioni na DEEP GREEN haijaguswa kwa namna yeyote ile licha ya ukweli kuwa kila mmoja anajua wamiliki wake, na yeye JK akiwa mnufaika mkubwa wa fedha hiyo maana ndiyo iliyomweka madarakani.

Kwa mbinu hii hakuna wa kudanganyika. Kama ana dhamira ampeleke mahakamani rafiki yake wa KAGODA, na DEEP GREEN ya chama chake.
 



Kijana bado hujakua kisheria sio JK wala ofisi ya rais ni Mahakama ndio imetoa hiyo hukumu, kwanza tumpongeze Dr Slaaa kwa kuibua hizo tuhuma maana kama siyo yeye wala usingesikia hao watuhumiwa uliowataja na wala JK asingevunja baraza la mawaziri.
 

You are too blind to see!! I am afraid nothing can be done to assist you.
 
Sasa hapa rais apongezwe kwa lipi?
Waziri mkuu akijiuzulu unatarajia rais angefanya nini?
Kuandamana na uhuru wa habari sio HURUMA ya rais ni haki ya wananchi.
Yani we kila kitu unaona ni fadhila za rais.
AMKA tumeingia zama mpya.
 

Tumpongeze pia kwa kuwasamehe bila kuwafungulia mashitaka wale waliorudisha fedha za EPA. Hii inaonyesha ana huruma sana kwa watu wanaiba mabilioni ya wananchi. Pia wakati huu wananchi wasio na hatia wanapigwa risasi na kuuwawa na polisi halafu yeye amekaa kimya. Hii inaonyesha yeye ni mtu mpole sana.
 

Unataka kutuaminisha akina Maranda wamefungwa kwa shinikizo la JK?

Kwa maana hiyo JK anaingilia uhuru wa mahakama
 
Slaa atapongezwa kwa kuratibu maandamano yasiyo na kikomo HATAHIVYO inabidi ampongeze JK kwa kumpa uhuru wa kuandamana

JK siyo mgawa uhuru wa kuandamana, KUANDAMANA NI HAKI YA KILA MTU KIKATIBA, KAMA WEWE YAKO UMEMPA JK UTAJIBEBA maana atakuvua GAMBA.................... NA mta-DEAL sana na vidagaa huku mkiyaacha mapapa yakiendelea kutesa KIMAGAMBA..............

Haya ........... mmewafunga hao wawili ..na wale waliorudisha kimya kimya ....MTAWAFANYA NINI............??? AU MNAWASAMEHE MBUNGUNI NA DUNIANI................??? AU HAWA NDO WALIGOMA KURUDISHA...........???
 
Nikirejea Maelezo yako..............
1. Kuvunja Baraza la Mawaziri ikiwa ni kujiuzulu kwa Waziri Mkuu ................ Ilikuwa lazima avuje na wala haikuwa kwa mapenzi yake tena maana waliojiuzulu walikuwa wengi na wengine walikuwa hawana imani naye...........
2. Kuwafikisha mahakamani viongozi wandamizi wa serikali; Mramba, Yona na Mgonja .......... Baada ya kuwafikisha nini kimetokea....??? Ni kiini macho tu ambacho wewe na wenzio mtabaki kujisifia nacho...........
3. Kuwapeleka watuhumiwa wa EPA mahakamani ............ Si wote wengine wamebaki siri yake................ Wale waliorudisha kimya kimya hakuna kati yetu anayewajuwa............. inawezekana hata yeye alirudisha..........
4. Kuwa na moyo wa uvumilivu kwa vyombo vya habari ............. Hana moyo wa uvumilivu bali analazimika kufuata katiba inayotoa uhuru huo.............
5. Kutoa vibali vya maandamano kwa vyama vya siasa pasiipo mkomo .............. Maandamamno ni haki ya kikatiba

 
Jina linalo kufaa ni ' Bubu ataka kupigwa mhogo'
Mnazidi kuongezeka tu................... Maleria sugu aka GeniusBrain aka Lilombe............ Mkiishiwa POINT tunajuwa mnachokimbilia.............. maana akili zinawatuma hayooo......
 
Tumpe kura uone kama kina Mkulu na kampani yake hawajaenda kunyea debe
 
Namuuliza mtoa mada, Je anawajua mafisadi waliokula fedha za epa?????? Huwezi kumpongeza kwa kwaonea dagaa na kuwaacha mapapa.
 
Bange mbaya sana jamani

Hawa akina Miranda walikwapua bilin 1.8 tu kati ya zaidi ya bilion 133 zilizochotwa EPA;Waliofungwa jana ni vidagaa tu lkn wale manyangumi yaliyochota panono hata mahakamamani hawajafikishwa na wala hawapelekwi popote

Fedha za EPA zilitumika kwenye kampeni za CCM mwaka 2005 na Dr Slaa amekuwa kila siku anasema hivyo na HAYUPO MWENYE UTHUBUTU NDANI YA SERIKALI YA CCM WA KUKANUSHA NA KUMPELAKA MAHAKAMANI hadi sasa!
 
Hivi unataka kutuaminisha kwamba Mh. Rais ndiye polisi, mwendesha mashitaka, mahakama na magereza!! Kwa hiyo kwako huyu ni dikteta na unataka tumpongeze. Nadhani hujui usemalo.
 
Hivi watuhumiwa wa EPA ni wawili tu? Au hawa ni mbuzi wa kafara!? Wapi Jituu Patel, Ben, Zakia Megji, JK na wengine wengi?
 
Kama CDM wanavyojishughulisha na shughuli za mahakama kule NYAMONGO...USHABIKI usio na Maana. We si ulikuwa unapiga kelele kwamba hawashughulikii watuhumiwa wa EPA. Ulitaka yeye ndo awashughulikie au mahakama ndo iwashughulikie?? Usiwe mfinyu wa mawazo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…