Wazee wote wachangiaji,
(1). Mimi ninasema kuwa ni vigumu kuwa on top ya mikataba ambayo hata wewe kiongozi you have no idea faida na hasara zake, na that is the case na viongozi wetu ni lazima tukubali kuwa hawaelewi kinachoendelea, kuanzia kwenye uchumi, Afya, mikataba, wao wanachojua ni kampeni za siasa tu!
(2). Mabepari ni binadamu ambao wanajali masilahi yao na wala sio ya nchi zao, na serikali kama za West zina sheria kabisa katika vitabu zinazoisukuma serikali kuwa involved katikia kuyasaidia mashirika binafsi ya biashara, yanapokwama nje ya nchi kama zetu, lakini hawa wafanya biashara binafsi ni lazima tujiulize kinachowakimbizia kwetu ni nini? Ni kwa sababu kwetu huku hakuna sheria! Hivi majuzi kampuni moja ya US ilienda kuutupa uchafu wao wa mafuta huko Guinea kwa kuilipa seriakli dola 600,000 tu! Kule kwao kwa sheria za environment ingewacost kama millioni dola 3, waziri wa Guinea alipoulizwa alijibu kuwa we needed the money, alipoulizwa kuhusu madhara ya afya ya ule uchafu akasema tusipokufa kwa uchafu huu wa US, tutakufa kwa njaa ni afadhali tufe tukiwa tumeshiba! Unafikiri kuna tofauti ya hao wa Guinea na bongo? Mara ngapi unga na mchele mbovu unauzwa tu mitaani kwa kuruhusiwa na serikali? Viongozi wetu hawana idea na mambo mengi wanayoyapitisha kwa kushinikizwa na mashirika ya biashara!
(3). Sasa hivi mashirika ya nje ya biashara yamekuwa na ujanja sana, kwani yote yanapitia South Africa, kule yanapata mashirika mengine ya kuwa front na kuja bongo kwa niaba yao, haya ya south Africa yanatujua sisi waafrika nje ndani kwa yanapata deal kiurahisi, maana yanajua kuwa hatujui lolote na tuna njaaa, jamani niambieni ATC tumeshuhudia mara ngapi ikibadili mikataba na hakuna lolote? Sasa hivi Tanzania tuna viwanda viwili tu ambavyo angalau vinaendeshwa na mashirika ya nje lakini yanatuletea faida kidogo nayo ni Bia na Sigara, lakini hata hayo mawili utashangaa kusikia hayo mashirika yanavyotengeneza hela, na hakuna kitu chochote cha ajabu yanachofanya kuendesha hivi viwanda,
sisi tulishindwa, sasa kama Guntram Itatiro walikirun hichi kiwanda cha bia to the ground wakaenda mapak kuwa mawaziri ili wafanya nini tofauti? Mwapachu ATC ilimshinda kabisaa sio siri leo ni waziri, Mungai ATC neye imemshinda kabisaa leo ni waziri ili afanye nini tofauti, yaani mifano ya kwa nini tunamatatizo tunayo kibao ni kwamba viongozi wetu hawafai na hawaelewi hii mikataba faida na hasara zake, hata kuwashauri ni kazi ya bure je kuna wataalamu wangapi hapa bongo? Ukiwakuta hawa wataalamu bungeni utafikiri kuwa nikweli kumbe ni uozo tu!
Kiongozi safi ni watu kama Kaduma ambaye ninajua kuwa aliendesha NMB kwa kiutaalamu na ana uwezo, kina Sumaye Kigoda na wenziwe wezi na mashirika toka South Afria, wakamshabikia kwa Mkapa ili afukuzwe kazi na wauze NMB kwa makaburu, mpaka siku Kaduma alipoitwa pale bungeni kueleza ukweli ndio viongozi kushituka kuwa hawa kina Sumaye ni wahuni, sasa ulitegemea mtu kama Kaduma awe nafasi kubwa katika serikali yetu katika kuangalia hii mikataba, NO! hata hiyo NMB alifukuzwa na Mkapa,
Ubepari hauna tatizo lolote kwa sababu unajali faida tu, sasa na serikali ni lazima iipiganie nfasi yake katika ubepari nayo ni kukusanya kodi na ajira kwa wananchi, leo kule US majengo kama Rockfeller Center yanamilikiwa na shirika toka Japan, lakini seriakli ya US inahakikisha kuwa hakuna hata senti moja wanaikosa kuitoza kodi, na kuna sheria za nchi kuwa only CEO ndiye atatoka Japan otherwise wote watakuwa wananchi wa US, Tanzania ni lazima ufike mahali tuwaheshimu na kwainua wataalamu wetu wa kweli kwani wapo ila hawapewi nafasi kwa sababu political system yetu imejengwa kwa ajli ya mkao wa kula. Mzee JK kabla ya kuingia alikuwa na mipango mingi kabambe lakini na yeye ameshaingia kwenye ile ile system ya kukaa na kusubiri a miracle, baraza la mawaziri ni bovu mno ni afadhali makatibu wa wizara wangebadilishana na mawaziri, otherwise tunaelekea shimoni tu!