hahahahahaJK ana magonjwa mengi. Pamoja na hayo yanayomfanya azimike, kuna ugonjwa huu wa "AHADIsm". Ndani ya wiki moja ya Kampeini ametoa ahadi mpya zisizokuwa katika Ilani ya CCM kama ifuatavyo:
-Kununua boti za kisasa Ziwa Victoria kupambana na majangiri ziwani
-Kununua Meli mpya ya kufidia MV Bukoba
-Kujenga Uwanja mpya wa ndege wa Kimataifa Kajunguti-Kyaka (Wa
Mbeya haujaisha!)
-Kuleta umeme mwingine wa Uganda kwa dola bilioni 1.6 kwa ajili ya
wilaya ya Misenyi
-Kupanua Uwanja wa ndege wa Bukoba ili upokee ndege kubwa
-Kuwaruhusu wananchi wa Misenyi waendelee kukaa katika Ranchi
aliyoiuza yeye mwenyewe kwa wawekezaji!
Huu ni mkoa mmoja. Mpaka tumalize mikoa 5, tutakuwa na kitabu cha ahadi. Zile zilizomo ndani ya Ilani hajazigusa. Ofisa mmoja aliye na JK kwenye msafara amenidokeza kuwa akianza kuhutubia wanashika mapu... kwa hofu ya kusikia ahadi mpya ambazo hazijazungumziwa popote.
Kumnyima JK ni uzalendo.
MNYIME KURA JK ULIOKOE TAIFA NA UGONJWA WA AHADIsm.
Inabidi hizi ahadi zote ziandikwe somewhere halafu kuelekea mwisho mwisho wa kampeni aulizwe vitu alivyoahidi na jinsi atakavyotekeleza hizo ahadi
JK aahidi vyandarua viwili kwa kila nyumba,hahahahaha
hahahahaha
nimecheka sana hapo kwenye bold