JK Alivyokosa Sifa za Kugombea!

Buchanan

JF-Expert Member
May 19, 2009
13,199
1,969
Tunakumbuka jinsi JK alivyodai kwamba hazitaki kura za wafanyakazi wa Tanzania na kwamba hata kama wakigoma MIAKA NANE (8) wasingeweza kuongezewa mishahara! Lakini muda si muda JK pamoja na wasemaji wake walitushangaza kwa kudai kwamba eti JK hakusema maneno hayo na kabla vumbi halijatua JK aliwaahidi wafanyakazi eti "atawaongezea mishahara" na kweli aliwaongezea! Mpaka sasa Dkt Slaa anakusudia kupeleka pingamizi kwa msajili wa vyama vya siasa dhidi ya JK kwa "kuwahonga" wafanyakazi ili apigiwe kura!

Ni vifungu gani basi vilivyovujwa?

Kifungu cha 21 (1) (a) cha Sheria ya Gharama za Uchaguzi, 2010 ambacho kinazungumzia "matendo yaliyokatazwa" kinasema kwamba:

"Kila mtu ambaye kabla au wakati wa kipindi cha kampeni, moja kwa moja au kwa namna nyingine yoyote, kupitia kwa mtu mwingine yeyote au kwa niaba yake, anatoa, anakopesha au anakubali kutoa au kukopesha, au anatoa, anaahidi au kumpatia au anajaribu kumpatia fedha yoyote au kitu chochote chenye thamani, mpiga kura au kwa ajili ya mtu yeyote kwa niaba ya mpiga kura yeyote au kwa ajili ya mtu mwingine yeyote kwa nia ya kumshawishi kupiga kura, au kuacha kupiga kura au kumrubuni mtu yeyote kutendo hicho kwa niaba ya mpiga kura huyo kupiga kura au kuacha kupiga kura katika kura za maoni au uchaguzi wowote."

Kifungu cha 24 (2), (7) kinasema:

"Mgombea yeyote ambaye, yeye mwenyewe, wakala wake au chama chake kitafanya kitendo ambacho kimekatazwa atakuwa au kitakuwa kimepoteza sifa za kushiriki katika kura za maoni na uchaguzi. Endapo mgombea au wakala wake au chama chake cha siasa atafanya kitendo ambacho kinapelekea kuwa ni kitendo kilichokatazwa na hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa, Mwanasheria Mkuu wa Serikali anaweza kufungua kesi ya jinai au kesi ya uchaguzi dhidi ya mgombea huyo."

ADHABU: Mgombea atatozwa faini isiyozidi milioni moja. (Kifungu cha 26 (b))

Kwa maoni yangu, JK anatakiwa akae pembeni ili watu wenye sifa za kugombea waendelee na mchakato wa uchaguzi! Msajili wa Vyama vya Siasa achukue hatua zinazostahili na kama hajachukua hatua hizo basi Mwanasheria Mkuu amfikishe mahakamani kama Sheria inavyosema!

Tujadili!
 
Section 21 subsection 1 naona iko straight JK na serikali yake kwa kumtumia yule katibu na Kapuya wamethibitisha kuwa wametoa rushwa ya wazi kwa wafanyakazi.
Msanii Tendwa na Lewis makame wasilete usanii wa aina yoyote ile icho kifungu kiko straight CCM wapumzishwe.
Tundu Lisu na Marando jumatatu iwakilisheni ilo pingamizi kama mlivoahidi please.
Mwaka huu mpaka kieleweke
 
Section 21 subsection 1 naona iko straight JK na serikali yake kwa kumtumia yule katibu na Kapuya wamethibitisha kuwa wametoa rushwa ya wazi kwa wafanyakazi.
Msanii Tendwa na Lewis makame wasilete usanii wa aina yoyote ile icho kifungu kiko straight CCM wapumzishwe.
Tundu Lisu na Marando jumatatu iwakilisheni ilo pingamizi kama mlivoahidi please.
Mwaka huu mpaka kieleweke

Yaani kama haki itatendeka, JK nje ya ulingo!
 
sheria inasema kabla au wakati wa kampeni, naomba nifahamu hii kabla inaanza lini? pili hivi JK alisema hawataongeza mishahara au hawatawapa 315,000/=?

kuweni makini msije mkaonekana ninyi ndio wajinga, maana kumbukumbu zangu zaonyesha jk alikataa kulipa 315,000/= kama kima cha chini ila alisema mishahara ya wafanyakazi itapanda,na serikali ilikataa kutangaza itapanda kwa kiasi gani, kama mnakumbuka wakati wa bunge la bajeti waziri wa fedha alisema mishahara ingepanda

ijapokuwa mimi si mwanasheria na ni maamuma wa sheria ila ningewashauri chadema waende mahakamani kwa hoja nyingine na wala sio hii, hii iko wazi na hawana hoja,

swali langu nalirudia tena kabla ya kampeni inaanza lini na inaisha lini?wajuzi nitanabahisheni
 
Ngoja nimtafute Dr Mwakyembe sijui kwa hili analizungumziaje

Sasa ndugu yangu mfianchi unategemea nini kesi ya nyani akipelekewa ngedere. Hata kama dr. Mwakyembe anajua ukweli kwa hili ni dhahiri atamtetea jk
 
Kila mtu ambaye kabla au wakati wa kipindi cha kampeni, moja kwa moja au kwa namna nyingine yoyote, kupitia kwa mtu mwingine yeyote au kwa niaba yake, anatoa, anakopesha au anakubali kutoa au kukopesha, au anatoa, anaahidi au kumpatia au anajaribu kumpatia fedha yoyote au kitu chochote chenye thamani, mpiga kura au kwa ajili ya mtu yeyote kwa niaba ya mpiga kura yeyote au kwa ajili ya mtu mwingine yeyote kwa nia ya kumshawishi kupiga kura, au kuacha kupiga kura au kumrubuni mtu yeyote kutendo hicho kwa niaba ya mpiga kura huyo kupiga kura au kuacha kupiga kura katika kura za maoni au uchaguzi wowote.[/COLOR]


Mkuu sidhani kama ndani ya chama chao au Makamba wanaweza kuielewa hii. Wanaweza kudai hawaielewi maana inaonekana kama is too redundant. tehe teheheheheh
 
Back
Top Bottom