Jiwe Lililoko Kamanga Fery Jijini Mwanza Libadilishwe jina Kutoka Bismack Rock na kuwa Muujiza wa Mwanamalundi

Intelligence Justice

JF-Expert Member
Oct 23, 2020
3,039
3,486
Wakuu,

Hili ni bandiko la ushauri kwa mam;laka husika lakini kuwekwa kwenye mjadala kuhusu jiwe kubwa la aina yake ambalo linatumika kama utambulisho wa jiji la Mwanza.

Jiwe hili liko pembezoni mwa mwa ufukwe wa ziwa Viktoria karibu na feri ya Kamanga na sambamba na barabara ya Nasser inayoelekea Ikulu ndogo huko Capri-Point.

Jiwe hili alilitumia mchezaji wa ngoma za kienyeji za kisukuma aitwaye Igulu Bugomola (Ng'wanamalundi/Mwanamalundi-thin legs and tall) ambapo alipanda juu yake baada ya kusimika vijiti vya miti kwenye mwamba na kukwea hadi juu kisha akaa na kucheza. Mpaka leo kuna masalia ya matundu ya yaliyotumika kusimika vijiti hivyo na sehemu alipokaa aliacha alama ya upande mmoja wa kalio. Igulu Bugomola alias Mwanamalundi alizaliwa huko Mwakabunga Nera wilaya ya Kwimba mkoa wa Mwanza mwaka 1846. Huyu Mwanamalundi alitokea kuwa na uwezo wa kucheza vizuri ngoma za kisukuma kwa ufasaha mkubwa akiambatana na miujiza ya kimazingara. (Soma kitabu kilichoandikwa na Boniphas Z. Boaz kwa undani zaidi).

Wakati wakoloni walipoingia nchini Tanganyika, moja ya maeneo ambayo Mjerumani aliyatamani sana ni jiji la Mwanza ambapo mtawala aitwaye Otto Von Bismarck sanamu lake liliwekwa juu ya jiwe hilo lililoko karibu na Kamanga feri. Baada ya sanamu kuwekwa juu ya jiwe na jina likaitwa 'BISMARCK'.

Ilipotokea vita kuu ya pili ya dunia kati ya Mjerumani na Mwingereza (WWII) 1939-1945 ambapo Mjerumani alishindwa vita na Mwingereza na kwa kuwa Mwingereza alimchukia Mjerumani waliamuru sanamau la mtawala wa Kijerumani kuvunjwa na kutupwa majini kitendo ambacho kilitekelezwa haraka sana.Masalia ya sanamu hilo yapo mpaka leo hapo majini.


Napendekeza ili kulinda urithi wa kihistoria wa wenyeji jiwe hilo libadilishwe na kuitwa jina la 'Miujiza ya Mwanamalundi-The miracles of Mwanamalundi' kama utambulisha wa jiji hilo la miamba ya mawe.

1607603548412.png
1607603575855.png

Pamoja na jiwe hilo lipo jingine lenye maajabu maeneo ya Bugarika linaitwa majimoto ambalo linaukumbi wa wazi chini yake linafaa kwa utalii wa ndani na nje
1607603834627.png


Nawasilisha
 
Mkuu kabla hawajabadilisha jina pale wajaribu kupaboresha maan now maji yamejaa balaa hapavutii tena...
Mkuu,

Nakubaliana na wewe ndio maana serikali inahangaika kutafuta vyanzo vya mapato lakini wanashindwa kubaini na kuthamini vilivyo bayana na kuboresha maana ili mtu avutike kwenda kushangaa lazima juhudi zenye gharama zifanyike. Hata pale kwenye mti wa mkuyu ambapo wajerumani walikuwa wakinyongea wale waliowaita wahalifu kwenye mzunguko mbele ya ofisi ya CCM, paboreshwe na barabara itafutiwe mtambuka wa kuhamishwa hapo. Sanamu ya Indira Ghandi (maarufu Ghandi hall) pahifadhiwe kwa ajili ya utalii. Utaratibu wa ndani unausumbufu mkubwa sana kwa sasaq ndio maana huwezi kuona lia mwisho wa wiki watu wengi wa kawaida wakitembelea kisiwa cha saanane kutokana na mlolongo mrefu wa kupata tiketi.
 
Mkuu,

Nakubaliana na wewe ndio maana serikali inahangaika kutafuta vyanzo vya mapato lakini wanashindwa kubaini na kuthamini vilivyo bayana na kuboresha maana ili mtu avutike kwenda kushangaa lazima juhudi zenye gharama zifanyike. Hata pale kwenye mti wa mkuyu ambapo wajerumani walikuwa wakinyongea wale waliowaita wahalifu kwenye mzunguko mbele ya ofisi ya CCM, paboreshwe na barabara itafutiwe mtambuka wa kuhamishwa hapo. Sanamu ya Indira Ghandi (maarufu Ghandi hall) pahifadhiwe kwa ajili ya utalii. Utaratibu wa ndani unausumbufu mkubwa sana kwa sasaq ndio maana huwezi kuona lia mwisho wa wiki watu wengi wa kawaida wakitembelea kisiwa cha saanane kutokana na mlolongo mrefu wa kupata tiketi.
Watakumbuka shuka kumekucha
 
Mkuu kabla hawajabadilisha jina pale wajaribu kupaboresha maan now maji yamejaa balaa hapavutii tena...
Yamejaa tena..?..!!maana mwaka jana palifurika hapo,ila baadae pakakauka,kama yamejaa tena,basi hiyo ni nature,hakuna namna venye itafanyika...
 
Umenikumbusha nyumbani kiongozi, nimepapeza sana nyumbani Mwanza


Historia ya mwamba , Mwanamalundi ina mengi sana ya kutufundisha, nilisoma maandiko mengi kuhusu maajabu aliyoyafanya pamoja na masimulizi ya IBAMBA NGULU hakika endapo historia ya nchi yetu na ma kabila zingekuwa documented tungekuwa mbali sana, cha kushangaza wazungu walipokuja wakaanza kubadili majina hata Ziwa Victoria liliitwa hivyo kama.heshima kwa malkia wa Uingereza aliyekuwa akiitwa Quuen Victoria Alexandria kama sikosei, nilisoma pia historia ya Ziwa Tanganyika ambapo ndo chanzo cha jina Tanzania / ilikuwa miongoni mwa majina yaliyopendekezwa nchi hii kuitwa,,, kuna uzi humu nilisoma!

In short kuna mengi ya kuvutia nchini kwetu, na Africa kwa ujumla, Wazungu wametumia ukosefu wa documentation KU ignore na kupoteza historia yetu! Nampongeza Rais Magufuli kwa kuonyesha nia yake ya dhati kuhamasisha na kuishauri wizara ya elimu umuhimu wa somo la historia mashuleni! I Unfeigned congratulate HE JPM!

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Yamejaa tena..?..!!maana mwaka jana palifurika hapo,ila baadae pakakauka,kama yamejaa tena,basi hiyo ni nature,hakuna namna venye itafanyika...
Hakuna namna venye itafanyika???

Hapa ndipo fikra zako zilipoishia?? Watu wanahamisha bahari na kuifanya ardhi, ardhi na kuifanya ziwa (man made lake).
Ama kweli tembea uone
 
Mkuu,

Nakubaliana na wewe ndio maana serikali inahangaika kutafuta vyanzo vya mapato lakini wanashindwa kubaini na kuthamini vilivyo bayana na kuboresha maana ili mtu avutike kwenda kushangaa lazima juhudi zenye gharama zifanyike. Hata pale kwenye mti wa mkuyu ambapo wajerumani walikuwa wakinyongea wale waliowaita wahalifu kwenye mzunguko mbele ya ofisi ya CCM, paboreshwe na barabara itafutiwe mtambuka wa kuhamishwa hapo. Sanamu ya Indira Ghandi (maarufu Ghandi hall) pahifadhiwe kwa ajili ya utalii. Utaratibu wa ndani unausumbufu mkubwa sana kwa sasaq ndio maana huwezi kuona lia mwisho wa wiki watu wengi wa kawaida wakitembelea kisiwa cha saanane kutokana na mlolongo mrefu wa kupata tiketi.
You're touching me so much , unaonekana unaifahamu vyema Mwanza, ubarikiwe Sana!

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Wasukuma wapo hapa kujadili utamaduni wao.

Kisha wanatumia lugha ya kigeni kujadili utamaduni wao.

Na hilo ni tatizo letu wengi. Hakuna nchi itaendelea huku inapiga teke utamaduni wake.

Utamaduni unatia ndani lugha.

Leo hii mambuzi mengine yanachanganya 'L' na 'R' mengine hayaweki 'H' inapotakiwa na kuiweka isipotakiwa. Mengine yapo bize kuandika 'Bhana' mengine yanachanganya 'dh' na 'th' mengine yanachanganya kwa kujiamini kabisa 'nadra' na 'aghalabu'

Yapo mengi. Huu uzi unamaanisha cha kuhifadhiwa siyo hilo jiwe tu.
 
Wakuu,

Hili ni bandiko la ushauri kwa mam;laka husika lakini kuwekwa kwenye mjadala kuhusu jiwe kubwa la aina yake ambalo linatumika kama utambulisho wa jiji la Mwanza.

Jiwe hili liko pembezoni mwa mwa ufukwe wa ziwa Viktoria karibu na feri ya Kamanga na sambamba na barabara ya Nasser inayoelekea Ikulu ndogo huko Capri-Point.

Jiwe hili alilitumia mchezaji wa ngoma za kienyeji za kisukuma aitwaye Igulu Bugomola (Ng'wanamalundi/Mwanamalundi-thin legs and tall) ambapo alipanda juu yake baada ya kusimika vijiti vya miti kwenye mwamba na kukwea hadi juu kisha akaa na kucheza. Mpaka leo kuna masalia ya matundu ya yaliyotumika kusimika vijiti hivyo na sehemu alipokaa aliacha alama ya upande mmoja wa kalio. Igulu Bugomola alias Mwanamalundi alizaliwa huko Mwakabunga Nera wilaya ya Kwimba mkoa wa Mwanza mwaka 1846. Huyu Mwanamalundi alitokea kuwa na uwezo wa kucheza vizuri ngoma za kisukuma kwa ufasaha mkubwa akiambatana na miujiza ya kimazingara. (Soma kitabu kilichoandikwa na Boniphas Z. Boaz kwa undani zaidi).

Wakati wakoloni walipoingia nchini Tanganyika, moja ya maeneo ambayo Mjerumani aliyatamani sana ni jiji la Mwanza ambapo mtawala aitwaye Otto Von Bismarck sanamu lake liliwekwa juu ya jiwe hilo lililoko karibu na Kamanga feri. Baada ya sanamu kuwekwa juu ya jiwe na jina likaitwa 'BISMARCK'.

Ilipotokea vita kuu ya pili ya dunia kati ya Mjerumani na Mwingereza (WWII) 1939-1945 ambapo Mjerumani alishindwa vita na Mwingereza na kwa kuwa Mwingereza alimchukia Mjerumani waliamuru sanamau la mtawala wa Kijerumani kuvunjwa na kutupwa majini kitendo ambacho kilitekelezwa haraka sana.Masalia ya sanamu hilo yapo mpaka leo hapo majini.


Napendekeza ili kulinda urithi wa kihistoria wa wenyeji jiwe hilo libadilishwe na kuitwa jina la 'Miujiza ya Mwanamalundi-The miracles of Mwanamalundi' kama utambulisha wa jiji hilo la miamba ya mawe.

View attachment 1646192View attachment 1646194
Pamoja na jiwe hilo lipo jingine lenye maajabu maeneo ya Bugarika linaitwa majimoto ambalo linaukumbi wa wazi chini yake linafaa kwa utalii wa ndani na nje
View attachment 1646199

Nawasilisha
Hicho kitabu kilichoandikwa na Boniphas Z. Boaz kinaitwaje na kinapatikana wapi
 
Hicho kitabu kilichoandikwa na Boniphas Z. Boaz kinaitwaje na kinapatikana wapi
Mkuu,
Kitabu kinaitwa hivi na kilitolewa kwa idhini ya wizara ya elimu ya Taifa mwaka 1974, kinapatikana kwenye maduka yenye kuthamini vitabu vya kiTanzania

Mwanamalundi: Mtu maarufu katika historia ya Usukuma​

Bonephas Z. Boaz
Wizara ya Elimu ya Taifa, 1974
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom