Jitahidi mwanao asisome masomo ya Sanaa

Jitahidi mwanao asisome masomo ya Sanaa

Red Giant

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2012
Posts
15,650
Reaction score
20,994
Mi nimesoma PCB, katika A-level niliyosoma kulikuwa na PCB na CBG. Katika tuliomaliza form six wengi wamefika vyuo vikuu hata wale waliopata div 3 na 4. Kuna walioenda computer science, food science, veterinary medicine, udaktari, uclinical officer, uafisa kilimo, uafisa wanyama, unesi, maabara, ualimu, uinjinia, uhasibu, clearing and forwading nk.


Wale waliopata ziro walienda vyuo ka matokeo yao ya form 4 nawengine walipata tempo za kufundisha. Hawakuwepo waliokaa kihasarahasara. Ninachotaka kusema ni kuwa sayansi ina uwanja mpana wa mambo ya kusomea. Pia sayansi inakupa nafasi ya kusomea kozi zenye soko tofauti na arts.


Nyakati za kusomesha watoto ilimradi umesomesha zimepitwa na wakati. Inatakiwa kusomesha kwakuangalia future yake. Ukisikia graduate hawana ajira utashangaa 90% ni waliosoma arts. Watoto wanatabia ya kufuata vitu vinavyoonekana ni rahisi. Ni jukumu lako mzazi kumuonyesha njia sahihi na kumtia moyo. Sayansi haina ugumu kwamba mtu mwenye bidii imshinde
 
Daaa aisee kuna ka ukweli hapa,kuna challenge hapa Pia

,coz za science ni uhakika wa Maisha yaani ajira, ila kupato chake ni kidogo au cha kusotea,kozi za biashara ikikupata kwenye anga zako duuu unatoka na mshahara unaoeleweka,

Pia hizi kozi ni za Msimu,sasa hivi Science pay Much,ila baada ya Miaka 5 Mbele duu,Kozi za biashara wanaweza nao kutoka tena sana tuu,miaka ya 2000-2010 kozi za biashara na Arts zilifana sana Kama Hr,Uhasibu,ugavi,usafirishaji,nk 2010-2015 duu hoi,science ndo zinafana,nime predict 5 ijayo kwa sababu ya miradi ambayo itakuwa imekamilika Kama Reli ya Kati to Rwanda,Reli ya tanga mpaka bahari ya Atlantic,bandari ya bagamoyo,na miradi mingine ambayo italeta Multiplier effect ktk uchumi!unaweza kuangalia Miradi mikubwa Tanzania utapata data!

So finally kozi za science muda wote ajira zipo regardless ya kipato chake na nafasi zake!
 
Nakubaliana na wewe kabisa.

Hata mimi watoto wangu wote lazima wasome masomo ya sayansi tena nataka wawe madaktari. Mungu atawasaidia. however, ukiangalia mabilionea wote tz hakuna aliyesoma masomo ya sayansi.

pia ugonjwa mkubwa wa watz ni rushwa, kati ya wale waliokula ESCROW ukianza na mzee wa tumbili hadi woote, hakuna aliyesoma sayansi hata mmoja.

hivyo hata arts ina mazuri yake pamoja na kwamba sayansi ni bora zaidi kwa kupata hela ya halali, art ni kupata hela ya wizi. mimi ni lawyer najua ninachoongea.
 
Kama mwanao ana kichwa kidogo haviwezi kuhimili hayo mambo ya science kwanini umtengenezee zero katika maisha yake the world is charging and what the child wants to accomplish in his future is his/her decision usitake apate zero kisa atapata tempo akafundishe au akaanze certificate huoni kama utakuwa umemrudisha nyuma na miaka inaenda plus pesa imekuwa ngumu
 
marijuana;

mkuu mimi ni advocate mkubwa wa kujiajiri na nimeshatake serious initiatives. hivi huoni kuna faida kusoma kozi ambazo unaweza kuchagua kujiajiri au kuajiriwa kuliko inayokulazimisha kujiajiri kwasababu kuajiriwa ni kugumu!.

madaktari kushindwa kudiagnose kuna mambo mengi. maabara mbovu na wagonjwa wengi navyo huchangia.
 
Last edited by a moderator:
Basi sawa, ila nahisi mtoa mada katuwekea mabano ila kama nimekuelewa vibaya nisamehe
 
Tupo tofauti sana, wakati wengine tunafikiria wanetu wasome ili waweze kujiajiri wengine wanafikiria watoto wao wasome ili waajiriwe.. Wakati mimi niliyesoma arts nimeajiri watu kadhaa japo wachache including waliosoma science wewe unaendelea kufikiria mimi nikutengenezee ajira wewe na watoto wako!!

Ok its its all good though..
 
Kwanza siyo kila mtu ataweza kusoma science,kila mtu ana uwezo katika kitu fulani,ebu fikiria kila mtu asome science subjects nani atafanya kazi ya kuwa lawyer, accountant,mwandishi wa habari n.k

Pili, siyo kila mtu anasoma ili aajiriwe, na ndiomana tatizo la ajira ni kubwa kwasababu hatufundishwi kutengeneza ajira kwa wengine
 
Still bado uko na LIMITED MIND kusoma sio kupata ajira TU bali kupata maarifa ambayo yanaweza kusaidia katika maisha yako na hayo maarifa hayapatikan tu kwa kusoma PCB ama CBG.
Unaweza soma hyo PCB yako na ukaajiriwa ila mimi niliesoma arts na kukosa ajira na nikawa na maisha MAZURI kuzid wewe
 
Mtoa mada inaonekana CAREER GUIDANCE AND COUNSELING hujataka kuitilia maanani kabisaaaa. Mtoto haambiwi asome nini bali uwezo wake ndio utakaoamua asome nini kwa kupata muongozo ulio sahihi toka kwa wazazi, walezi na hata walimu.

Msituandalie madaktari wa kutudunga sindano za Quinine wakati tuna kiharusi wala walimu wa masomo ya sayansi watakao tuandalia mifano ya waliosoma sayansi na wataalamu wengine wa aina hiyo kwa mtazamo wa KUSOMA MASOMO YA SAYANSI.

Mtoto aende shule kwa ajili ya kupata mwanga wa maisha na si ajira pekee kwani hayo si malengo ya elimu!
 
Back
Top Bottom