Ningekuwa mimi dawa yao ni kuwa na mziki mkubwa zaidi yao,natafuta siku akiwa anaumwa nami nafungulia muziki kwa sauti ya juu,atajirekebisha tu.
Enzi zangu nilikuwa nawakomesha wenye tabia hizo, baada yakuona nanyanyasika, niliamua kumfuata mshikaji wangu aliyekuwa na vyombo vya mziki vya kukodisha,
Nikamuomba viwe vinakaa kwangu,
Sasa limbukeni yule tuliyepanga nyumba moja akiwasha tu kiredio chake, mie namuwashia vyombo vyangu kwa mziki wa Bob Marley mpaka nyumba inatikisika!
Mbona aliamua yeye kwenda kwa mjumbe, mjumbe mwenyewe tayari nilishampa taarifa, hivyo akampuuza!
Mwisho aliama kuhama yeye!
Hilo tatizo hata mimi linanisibu, nasubiria ushauri pia, manake mtu mzima kumfundisha kazi kweli kweli
Kitewo nkiki noseka monoama!??
Hahah kumbe ni Mdengereko....!!!
Baada ya ulimwengu kuhamia dijitali basi hata wao wamehama kutoka ngoma za "Mdundiko, Segere" nk na kuja kwenye ulimwengu wa kubofya...
Ila hao dawa yao ni moja tu, ongea na vishoka wa mtaani wapige shoti nyumbani kwake, hizo tabu hutazipata tena
Hahaha ote awae...lekana naso. nivea, nyi kui ohenda?
Aaaaagh........na nyie bana!
Awuaraa!Nkiki mbe??!
Tabia zingine bwana sijui ni za asili? Tuna jirani yetu anatusumbua sana, yaani anasikiliza muziki kwa sauti kubwa sana na hana usiku wala mchana! Anaanza saa 11 asubuhi na anaweka sauti kubwa muda wote mpaka saa 5 au 6 usiku, yaani kelele tu. Yeye na mke wake wote wako hivyo na wana watoto wadogo sana, inanishangaza kwa kweli.
Mkewe huweka taarabu, mipasho kwa sauti kubwa sana, jamaa mwenyewe mfano asubuhi hii kaweka cd ya Remi Ongala (nafikiri kainunua jana) basi kaweka sauti kubwa sana wakati yeye mwenyewe kakaa nje ya nyumba yake akisikilizia. Jamaa ni Mndengereko, sasa sijui ni asili ya uswahili? Siku nyingi tu nilitaka nimfuate kumjulisha tatizo hili, lakini wife anasema huyu kuna analotafuta kwa majirani kwa hiyo tumuache tu na ulimbukeni wake.
Naomba ushauri wenu wadau, tutaishi hivi mpaka lini?
Mimi nilikomesha tabia ya hivyo kwenye nyumba ninayoishi
watu walikua wanafungulia ufa mshenzi mm nikawa nakodi ufa
kubwa kwa jamaa yangu mmoja mwenye duka la electronics
nikawakomesha wenyewe wakaja kunifuata jamani sauti nikawaambia
waanze wao kwanza kuwa wastaarabu mpaka
leo heshima.
Tabia zingine bwana sijui ni za asili? Tuna jirani yetu anatusumbua sana, yaani anasikiliza muziki kwa sauti kubwa sana na hana usiku wala mchana! Anaanza saa 11 asubuhi na anaweka sauti kubwa muda wote mpaka saa 5 au 6 usiku, yaani kelele tu. Yeye na mke wake wote wako hivyo na wana watoto wadogo sana, inanishangaza kwa kweli.
Mkewe huweka taarabu, mipasho kwa sauti kubwa sana, jamaa mwenyewe mfano asubuhi hii kaweka cd ya Remi Ongala (nafikiri kainunua jana) basi kaweka sauti kubwa sana wakati yeye mwenyewe kakaa nje ya nyumba yake akisikilizia. Jamaa ni Mndengereko, sasa sijui ni asili ya uswahili? Siku nyingi tu nilitaka nimfuate kumjulisha tatizo hili, lakini wife anasema huyu kuna analotafuta kwa majirani kwa hiyo tumuache tu na ulimbukeni wake.
Naomba ushauri wenu wadau, tutaishi hivi mpaka lini?
Amanakoy orospo cucuk. Susar misin bee?Awuaraa!