AX!! JIRANI TAM TAMUU
24
Endeleaa...
Nilikaa ndani kumsubili Nasra sema ukweli nilikuwa na hamu ya kumuona Nasra kwani moyo wangu ulikuwa umemchagua kuwa naye,
Nilika kama dk16 nikasikia nje jina la Nasra likitajwa,
"Nasra una mgeni wako yuko ndani ana kusubili,,
"Mgeni wangu mimi?
"Ndio, "ni nani?.
"Yumo ndani si ukamuangalie..
Mahojiano hayo yalinidhihilishia kuwa Nasra wa kipindi hicho zanzibar ndio yule yule hajabadilika maana hakuamini kama anaweza kuwa na mgeni,
Nasra aliingia ndani akanisogelea bila kuniangalia usoni akaniuliza,
"Unasemaje maana huu ni mda wa kazi na istoshe huwa sipendelei maongezi na watu napenda kufanya kazi zangu nikimaliza nipumzike nifikilie maisha ya kesho,,
"Nasra Nasra...
Aliposikia sauti yangu alikuwa kama amepigwa shoti ya umeme akanigeukia na kuniangalia,,
Hakuamini kuniona pale aliniangalia kwa tahamaki kisha akasimama akaniangalia usoni akasimama na kutaka kuondoka,,
"Nasra namba unisamehe naomba kuongea na wewe..
"Seif ulinitia aibu ya mwaka,,
"Naomba unisikilize nasra,,
"Seif kwa sasa niko kazini niko nasambaza chakula kwa wateja,,
"Kwani mko wangapi hapa kwa kuhudumia?.
"Tuko wawili..
"Twende nikuombee kwa bos,
"Seif utanihalibia kazi yangu,,
Nilitoka naye nje nikmuomuaga yule mama mwenye hotel,,
"Mama namchukua huyu ndungu yangu hatarudi tena hapa,,
"Eeeh!! Kwanini?
Nasra alishangaa ile kauri ila akanyamanza,
"Sasa mbona sina hapa pesa yakumlipa kwa sasa?
"Hiyo usijari mama,,
"Sawa safari njema,,
"Haya kwaheli,,
Nilimuingiza kwenye gari nasma tukaianza safari mda wote Nasra alikuwa kimya,
"Nasra wewe ndie ulikiwa chaguo langu niliyekuchagua ila hila za pale kwenu wakanibadilishia mke wakanipa yule ndugu yako,
"Niliyajuwa hayo ndugu yangu alinisimulia,,
"Pole kwa matatizo nasra,
Niliisha poa,
Nilimpeleka mpaka maeneo ya sinza nikamchukulia chumba hotel nzuri ya garama,
"Ingia ukaoge uje,,
Baada ya kuoga tulishuka sehem ya kula tukala chakula huku tunapiga story mbali mbali baada ya kula nikampeleka duka la nguo za kisasa nikamnunulia nguo za bei kali baada ya hapo nikampeleka saloon kubwa yenye hadhi kubwa wakamlemba nikamnunulia mahitaji yote ya kujipodoa siyo siri Nasma alingaa alipendeza na uzuri wake ukaonekana kumbe Nasra alikuwa mzuri kuliko hata zahara,,
Mida ya saa kumi na moja nilirudi nyumbani nikakuta Zahara hayupo nikamuuliza shomy,
"Vp zahara katoka saa ngapi?
"Mida hii,
"Alikwambia ameenda wapi?.
"Amesema ana shift ya usiku kazini,
"Ok, vp mme wako yupo?.
"Hayupo nae kaingia kazini shift ya usiku,
"Sawa,
Nilitika nikaingia chumbani nikajua hakuna cha shift ya usiku atakuwa na juma,,
Itaendelea....