Ni neno la kiswahili <i>corrupt</i> lililotokana na kushangaa.....wanawake wenye maumbile yakuvutiavutia miaka ya 1988-1992 watu walikuwa wakiwashangaa sahangaa(<i>wakishangingi</i>) hivyo wakaitwa mashangingi(kabla walikuwa pashkuna,wowowoo etc)...wabunge wetu walipoanza utukufu mwaka 1990 Mzee Mwinyi aliwakopesha LandCruisers (TZC 90xx) na hivyo watu waliyaita MASHANGINGI sambamba na PAJERO kufananishwa na noti ya 500 ambayo ilitoka 1988 na ndiyo ilikuwa kubwa(hakukuwa na 1,000 2,000 5,000 wala 10,000 wakati huo) ilipokuja 1,000 ikaitwa BUKU kwa kuwa ilibidi ukusanye noti za 100 kumi kama kitabu upate hiyo alfu.