Jinsi Ya Kuweka Ukomo wa matumizi ya data ktk internet

mludego

JF-Expert Member
Mar 16, 2013
2,395
3,197
Msaada wana jukwaa, nimekua na tatizo la matumizi makubwa ya bando mpaka imekua kero kwangu kujiunga unga mara kwa mara na vifurushi vya internet.

Hata zile apps zinazo tumia data huwa nazi shutdown lkn tatizo lipo pale pale , pia sio mtu wa kuangalia videos mtandaoni kiviile lkn kifurushi kinaisha before the date na mara nyingi huwa nanunua kifurushi cha week Chenye GB 1 kwa mtandao wa Halotel na tigo.

Tafadhali naomba mwenye kufahamu ni kwa namna gani naweza kuweka data limitation ktk simu mfano nataka nitumie MB 400 pekee kwa wakati huo na hizo MB 600 zibaki hivyo hivyo ata kama Niko online nitumiwe alert ya taarifa kuwa nimefikia matumizi ya mb fulani

NB natumia samsung j6+ asante karibuni


cc CHIEF MKWAWA
 
Acha kuwasha data kipindi huna cha kufanya kwenye internet
Hata usipowasha data.muda wao ukifika wanachukua tu.
Juzi niliwapigia halotel.
Wakaniambia muda wa kifurushi umeisha.
Nikawauliza ikiwa nimemaliza kifurushi kabla ya muda wangu kuisha je mtaniongezea kifurushi ili nifidie muda wangu?uliobaki?
Yaani wao muda ukifika wanakomba vyote.
Ila ukimaliza kifurushi kabla ya muda hawafidii ule muda.
TUNATAPELIWA SANA
 
Ingia tu settings kwenye simu yako huwa kuna namna ya kuzuia matumiz makubwa ya data
Settings>network & internet>data usage>data warning and limit alaf utamalizia
 
Kama unaona vifurushi havikusaiidii ACHA kujiunga na uanze Kutumia Salio la kawaida kuongea, kutuma sms na kuperuzi mtandaoni.

Nakuhakikishia utapiga magoti kuishukuru mitandao ya simu kwa kutuletea vifurushi.
Hata usipowasha data.muda wao ukifika wanachukua tu.
Juzi niliwapigia halotel.
Wakaniambia muda wa kifurushi umeisha.
Nikawauliza ikiwa nimemaliza kifurushi kabla ya muda wangu kuisha je mtaniongezea kifurushi ili nifidie muda wangu?uliobaki?
Yaani wao muda ukifika wanakomba vyote.
Ila ukimaliza kifurushi kabla ya muda hawafidii ule muda.
TUNATAPELIWA SANA
 
Kama unaona vifurushi havikusaiidii ACHA kujiunga na uanze Kutumia Salio la kawaida kuongea, kutuma sms na kuperuzi mtandaoni.

Nakuhakikishia utapiga magoti kuishukuru mitandao ya simu kwa kutuletea vifurushi.
Unaelewa nilichozungumzia?
 
Nawasha data pale ninapohitaji kutumia tuu,pia na shutdown all apps zinazotumia data na zisizo

Nachohitaji nimekieleza Aya ya mwisho soma vizuri
Ili kujua tatizo Nenda settings angalia matumizi ya data Kwa kila app
Utakuta app zimejipanga kuanzia inayo consume data nyingi Hadi ya mwisho chini inayoconsume data kidogo

Hapa utagundua kuna apps zinakula data hata km huzitumii zi disable hizo apps

Sent from my CPH1923 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu mludego hii ishu rahisi sana. Nenda setting> network> internet> data usage> data warning hapo unalimit kiasi cha MB's unazotaka zitumike na ikifikia hizo ulizozilimit simu inakunotify then utaamua mwenyewe uendelee au uongeze MB's.
 
Back
Top Bottom