Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,505
- 9,286
Kabla hujaanza kujihusisha na mambo ya makeup ni vitu vingi sana unakuwa hujui na nadhani kuwa bado wapo wale wasiojua utaratibu wa makeup vizuri, kama vile makeup products au makeup tools..na hivyo kuna wengine bado wanatumia wanja wa kawaida kujazia/kuchorea nyusi zao, hiyo pia ni sawa lakini brow powder ndio better zaidi.
Jinsi ya kujaziliza/kuchora nyusi zako.
Uwe na wanja wa powder au wa jel, eyebrow brush na concealer ( hii ya mwisho sio lazima maana mimi siitumii natumia foundation na wanja wangu unakaa vizuri tuu).
Anza kwa kuzichana nyusi zako kwa kutumia brush au kitana kidogo sana ili nyusi zikae kwenye mpangilio mzuri, then chukua brow brush yako na uchukulie wanja wako wa powder kisha uanze kupaka.
Kama haupo vizuri katika kupaka unaweza kutumia eyebrow shaper na uchore shape inayokufaa
Halafu chukua foundation yako ili usawazishe ile iliyotokeza/kunyoosha ule brow powder. Tumia concealer brush kupaka mstari mwembamba ulionyooka ukifuatisha uliyochora au kujaziliza nyusi zako. Fanya hivi kwa juu na chini kisha sawazisha vizuri.
Hapa chini ni njinsi ambavyo unaweza kuchora mistari ya namna unavyotaka wanja wako uwe. Mimi kwenye kuchora hiyo mistari huwa natumia wanja wa kawaida huu wa penseli halafu katikati humo ndo naweka wanja wangu wa poda au jel.
Hapa kuna wanja wa poda na wanja wa jel
Mimi natumia zote mbili kutegemea na sehemu ninayoenda na event husika. Wanja wa jel unakaa sana kuliko wa poda. Huo wa jel hata ukitokwa jasho wenyewe hautoki mpaka utakaponawa uso na sabuni
Hii ndio eyebrow shaper. zinakuwa 3 ndani ya pakti yake na zinakuwa za shape tofauti. Kwahiyo wewe mwenyewe utachagua shape unayoipenda kutumia.
Jinsi ya kujaziliza/kuchora nyusi zako.
Uwe na wanja wa powder au wa jel, eyebrow brush na concealer ( hii ya mwisho sio lazima maana mimi siitumii natumia foundation na wanja wangu unakaa vizuri tuu).
Anza kwa kuzichana nyusi zako kwa kutumia brush au kitana kidogo sana ili nyusi zikae kwenye mpangilio mzuri, then chukua brow brush yako na uchukulie wanja wako wa powder kisha uanze kupaka.
Kama haupo vizuri katika kupaka unaweza kutumia eyebrow shaper na uchore shape inayokufaa
Halafu chukua foundation yako ili usawazishe ile iliyotokeza/kunyoosha ule brow powder. Tumia concealer brush kupaka mstari mwembamba ulionyooka ukifuatisha uliyochora au kujaziliza nyusi zako. Fanya hivi kwa juu na chini kisha sawazisha vizuri.
Hapa chini ni njinsi ambavyo unaweza kuchora mistari ya namna unavyotaka wanja wako uwe. Mimi kwenye kuchora hiyo mistari huwa natumia wanja wa kawaida huu wa penseli halafu katikati humo ndo naweka wanja wangu wa poda au jel.
Hapa kuna wanja wa poda na wanja wa jel
Mimi natumia zote mbili kutegemea na sehemu ninayoenda na event husika. Wanja wa jel unakaa sana kuliko wa poda. Huo wa jel hata ukitokwa jasho wenyewe hautoki mpaka utakaponawa uso na sabuni
Hii ndio eyebrow shaper. zinakuwa 3 ndani ya pakti yake na zinakuwa za shape tofauti. Kwahiyo wewe mwenyewe utachagua shape unayoipenda kutumia.