Jinsi siasa inavyoua soka la bongo na jinsi wanasiasa wanavyopandikiza uhasama ili wawatawale

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,868
FB_IMG_1526828367514.jpg
FB_IMG_1526828374916.jpg
MJADALA WA TIMU ZA TANZANIA KUTOENDELEA KWA SABABU ZA KISIASA UNAENDELEA...

Rafiki yangu hapa mtandaoni, #Fareed_S. Al - Abeid ameniandikia kisa kifuatacho;

Ndugu Mtatiro, soma kisa cha mechi ya Yanga na Simba 1975 Nyamagana, Mwanza. Msafara wa Yanga uliposhuka Dodoma ulikua Mkubwa wa Kihistoria. Inasemekana Mwalimu alikuwapo Dodoma ...ulimshtua.
Mzee Mangara aliekuwa Mwenyekiti alikua pia Rafiki wa Mwalimu. Yanga walipofika Dar Es Salaam mapokezi yalikua makubwa sana..zaidi ya Dodoma.

Haikuchukua mwezi, Yanga ikaingizwa katika mgogoro mkubwa ambao haujawahi kutokea. Ilikua vita, Tambwe Leya aliyekuwa kocha aliyeleta ubingwa akatimuliwa na Yanga ikakatika vipande viwili, kipande cha Yanga na cha Pan Africa. Juhudi za Mangara kumuona Mwalimu kuokoa jahazi ziligonga mwamba! Yanga ikashuka daraja!

Simba nao wakafika Nusu Fainali kombe la Afrika na kutolewa na Mehhala El Kubra kwa penalti kule Cairo. Baada ya mechi hiyo Simba ilikua jina kubwa Afrika nzima na Afrika Mashariki, Umaarufu wa Simba ukawa mkubwa ukishindana na TANU, hawakuchukua muda ukatokea mgogoro mkubwa, kukawa na Simba ya King Kibaden na Haidar Abeid na Maulid Dilunga ikakatika vipande na kuzaliwa Red Star au Nyota Nyekundu

Kuanzia wakati huo soka la Tanzania halijaimarika mpaka leo. Haya pia yaliwatokea Coastal Union na Africa Sports za Tanga, timu pinzani ambazo zilikua na ushindani mkubwa kwenye soka la Tanzania, timu hizi zilidhibitiwa na dola kwa kuhusishwa na Yanga na Simba.

Mikoa iliyokuwa ikitoa wachezaji wengi makinda waliokuwa wanachukuliwa au kukimbiliwa na Simba na Yanga - ambayo ni Morogoro, Mwanza na Tanga ikafa kisoka, haikuwa bahato mbaya. Ni mipango tu.

Haya hayapo Simba na Yanga tu, hata FAT na Sasa TFF, zote zimekuwa zikitumiwa kwa maslahi ya dola na CCM na siyo uhalisia wa kukuza soka.

Na mara nyingi ukiangalia chanzo cha migogoro hakionekani ila kuna nguvu ya nje inayotumia Vyombo vya Habari kukuza migogoro hiyo.

Ni kweli, mfano umati kama ule ulio tokea kuwapokea Simba baada ya Kuwatoa Al Ahly ya Misri huwa unawatisha sana wanasiasa, wanaanza kuhofia kwamba vyama vyao vitaporwa utii na mamlaka na njia ya pekee inakuwa kuzitumia timu hizi kwa mbinu za hali ya juu na wakishindwa kuzitumia huziingiza kwenye mgogoro au mpasuko mkubwa.

Mzee Masonga wa Morogoro na Fareed, wanazidi kunitafakarisha sana.

[HASHTAG]#Mtatiro[/HASHTAG] J
 
Mi naskiaga yanga ni ccm lakini kwa kauli ya mkulu jana, yeye ni simba, sasa sijui bado yanga wanapendwa na ccm tena au laa.!
 
Umeandika vzr lkn kuna makosa kidogo...Simba haikutoa al hilal ,Bali Alitoa Zamalek ,na Yanga haijawahi kushuka daraja ,ni hayo tu ,lkn Mada yako inajadilika
 
Kama ni kweli tutafika tu
Tatizo kubwa ni kuwa hapa TZ wapinzani walikosa siku nyingi credibility kwa ajili ya kuzusha hasa Tundu Lissu. Hivyo watu hawaamini tena. Katika nchi za wenzetu reliable source of information hutoka kwa wapinzani maana wao ni watchdog ya serikali iliyo madarakani.
 
Tatizo kubwa ni kuwa hapa TZ wapinzani walikosa siku nyingi credibility kwa ajili ya kuzusha hasa Tundu Lissu. Hivyo watu hawaamini tena. Katika nchi za wenzetu reliable source of information hutoka kwa wapinzani maana wao ni watchdog ya serikali iliyo madarakani.
Una akili timamu ?
 
Wasioaminika ni nani kati ya wapinzanina ccm?
Ni nani kamweka propesa CUF?
Ni nani kaiba kura Zanzibar?
Ni nani analaumiwa kwa kusema uwongo daima kuhusu uchumi?
 
conne
View attachment 782061 View attachment 782057 MJADALA WA TIMU ZA TANZANIA KUTOENDELEA KWA SABABU ZA KISIASA UNAENDELEA...

Rafiki yangu hapa mtandaoni, #Fareed_S. Al - Abeid ameniandikia kisa kifuatacho;

Ndugu Mtatiro, soma kisa cha mechi ya Yanga na Simba 1975 Nyamagana, Mwanza. Msafara wa Yanga uliposhuka Dodoma ulikua Mkubwa wa Kihistoria. Inasemekana Mwalimu alikuwapo Dodoma ...ulimshtua.
Mzee Mangara aliekuwa Mwenyekiti alikua pia Rafiki wa Mwalimu. Yanga walipofika Dar Es Salaam mapokezi yalikua makubwa sana..zaidi ya Dodoma.

Haikuchukua mwezi, Yanga ikaingizwa katika mgogoro mkubwa ambao haujawahi kutokea. Ilikua vita, Tambwe Leya aliyekuwa kocha aliyeleta ubingwa akatimuliwa na Yanga ikakatika vipande viwili, kipande cha Yanga na cha Pan Africa. Juhudi za Mangara kumuona Mwalimu kuokoa jahazi ziligonga mwamba! Yanga ikashuka daraja!

Simba nao wakafika Nusu Fainali kombe la Afrika na kutolewa na Mehhala El Kubra kwa penalti kule Cairo. Baada ya mechi hiyo Simba ilikua jina kubwa Afrika nzima na Afrika Mashariki, Umaarufu wa Simba ukawa mkubwa ukishindana na TANU, hawakuchukua muda ukatokea mgogoro mkubwa, kukawa na Simba ya King Kibaden na Haidar Abeid na Maulid Dilunga ikakatika vipande na kuzaliwa Red Star au Nyota Nyekundu

Kuanzia wakati huo soka la Tanzania halijaimarika mpaka leo. Haya pia yaliwatokea Coastal Union na Africa Sports za Tanga, timu pinzani ambazo zilikua na ushindani mkubwa kwenye soka la Tanzania, timu hizi zilidhibitiwa na dola kwa kuhusishwa na Yanga na Simba.

Mikoa iliyokuwa ikitoa wachezaji wengi makinda waliokuwa wanachukuliwa au kukimbiliwa na Simba na Yanga - ambayo ni Morogoro, Mwanza na Tanga ikafa kisoka, haikuwa bahato mbaya. Ni mipango tu.

Haya hayapo Simba na Yanga tu, hata FAT na Sasa TFF, zote zimekuwa zikitumiwa kwa maslahi ya dola na CCM na siyo uhalisia wa kukuza soka.

Na mara nyingi ukiangalia chanzo cha migogoro hakionekani ila kuna nguvu ya nje inayotumia Vyombo vya Habari kukuza migogoro hiyo.

Ni kweli, mfano umati kama ule ulio tokea kuwapokea Simba baada ya Kuwatoa Al Ahly ya Misri huwa unawatisha sana wanasiasa, wanaanza kuhofia kwamba vyama vyao vitaporwa utii na mamlaka na njia ya pekee inakuwa kuzitumia timu hizi kwa mbinu za hali ya juu na wakishindwa kuzitumia huziingiza kwenye mgogoro au mpasuko mkubwa.

Mzee Masonga wa Morogoro na Fareed, wanazidi kunitafakarisha sana.

[HASHTAG]#Mtatiro[/HASHTAG] J
reading between the lines ni kwamba ... dola inahofu kwamba kama yanga wakienda kwenye uchaguzi pamoja wanaweza kuungana na wale waliomtia matatizoni mwenyekiti wao bwana manji ? wakaamua kutompigia kura. kwakuwa uchaguzi upo karibu tuwavuruge yanga ili wasiwe wamoja. ukifuatilia sana kwa undani utaona yanga wanashiriki mashindano makubwa ya cuf lakini wanaoandikwa sana ni simba? kwann? nimekuelewa bwana mtatiro
 
Back
Top Bottom