Jinsi nilivyowahi kutapeliwa, Wewe je?

Jinsi nilivyowahi kutapeliwa, Wewe je?

tuanze na sabuni.
inakuwa hivi; sabuni zinakuwa vipande vitatu ambavyo kwa juu vinabandikiwa karatasi ya kufunika zinazo fanana mfano karata. sabuni mbili za kukosea zikishabandikwa zile karata basi zinawekwa pembeni kisha wanachukua kile kipande cha tatu ambacho ndio chakupatia kinachimbwa kwa ajiri ya kuweka alama ya kupatia mfano labda kisoda sasa basi hiki kipande kinawekewa zile karata juu na chini kwa hiyo ukifunua kwa juu utakiona kile kisoda ila ukiigeuza chini juu kwenye ile karata ya upande wa pili ukiifunua ile karata hutakiona kisoda kitakuwa tayari kwa chini.anavyofanya sasa tupu na tupu anakufunulia unaona kabisa hazina kitu hivyo unajipa moyo kuwa ulipo weka hela yako umepatia kisha anakuambia ongeza hela hii ni bahati yako ukiongeza poa usipoongeza poa sasa kabla hajaifunua atafanya kila awezalo kuhakikisha ile sabuni anakuwa ameigeuza chini juu.akiifunua karata utaona umekosea kumbe sabuni hiyohiyo ukiigeuza kwa upande wa pili utaikuta karata tena ambayo ukiifunua utakiona kile kisoda.done.(samahanini jamani kuna kitu hapa nakimalizia kwanza nitakuja kuendelea)
 
tuanze na sabuni.
inakuwa hivi; sabuni zinakuwa vipande vitatu ambavyo kwa juu vinabandikiwa karatasi ya kufunika zinazo fanana mfano karata. sabuni mbili za kukosea zikishabandikwa zile karata basi zinawekwa pembeni kisha wanachukua kile kipande cha tatu ambacho ndio chakupatia kinachimbwa kwa ajiri ya kuweka alama ya kupatia mfano labda kisoda sasa basi hiki kipande kinawekewa zile karata juu na chini kwa hiyo ukifunua kwa juu utakiona kile kisoda ila ukiigeuza chini juu kwenye ile karata ya upande wa pili ukiifunua ile karata hutakiona kisoda kitakuwa tayari kwa chini.anavyofanya sasa tupu na tupu anakufunulia unaona kabisa hazina kitu hivyo unajipa moyo kuwa ulipo weka hela yako umepatia kisha anakuambia ongeza hela hii ni bahati yako ukiongeza poa usipoongeza poa sasa kabla hajaifunua atafanya kila awezalo kuhakikisha ile sabuni anakuwa ameigeuza chini juu.akiifunua karata utaona umekosea kumbe sabuni hiyohiyo ukiigeuza kwa upande wa pili utaikuta karata tena ambayo ukiifunua utakiona kile kisoda.done.(samahanini jamani kuna kitu hapa nakimalizia kwanza nitakuja kuendelea)
Duuuu.
Tunakusubiri...
 
Nakumbuka ilikuwa miaka ya tisini mwanzoni,brother wangu alitapeliwa mnazi mmoja pale. Siku hiyo asubuhi aliaga anaenda shule boarding iringa,akaondoka na baraka zote za wazazi,ghafla saa nne asubuhi asharudi home anahema kichizi,wazee wakamuuliza kulikoni hujaenda shule?akawakusanya wazazi chumbani wakajifungia mi nikawa nachungulia ,bro akatoa kidude flan hivi nikamsikia anasema dhahabu,aisee wazee wakaenda funga mageti yote nje,bro akawaambia alikutana na msukuma stand eti aliokota hiko kidude ila yeye hakitaki kimeandikwa GOLD FIRST CLASS FROM ..nimesahau jina la mgodi akaamua mpa nauli ya ke ya bus to iringa na poketi money yote. Aisee ile ishu iliwachanganya wazee wakajua utajiri huu. Milango imefungwa home hamna wa kutoka mpaka mimi wanani ignore,ikafika usiku wa saa nne wakatoka kwenda kwa mzee jirani yeye mtaalam wa madini hahaha,yule mzee akawasha stovu akayaiunguza yale mawaya dooh yakawa meupe na biashara ikaishia hapo.
Nimeipenda hii. Hasa jinsi ulivyoisimlia, nimecheka sana.
 
Mie nliwahi kumpatia huyo tapeli mpk aliomba poo...
Ilikua naingia Ubungo kama saa 9 nielekee Morogoro kuna jamaa akaja na simu kanionyesha na kusema nimpe 10000 mie nlikua nishaskia habari zao basi ile kunionyesha tu nikaishika sijaiangalia sn nikaitia mfukoni naanza kumpa pesa akaanza ooh siuzi nimuongeze pesa laki 1 nikamwambia wee unauza 10000 kamata hii nenda na nlikua na jamaa pale Ubungo aliimba segere aisee...nakumbuka mpk leo!!!Kumbe ilikua ile botion kwanza unaiangalia ile ukimrudishia tuu akikupa tena mche umewekwa housing!!!
 
Namshukuru MUNGU sijawahi kutapeliwa hata siku moja Zaidi ya kuwaokoa watu wengine, nimeshaokoa watu Zaidi ya wane kwa utapeli wa Simu/dawa za kutunzia samaki/Matrekta n.k. Sijisifu ila namshukuru MUNGU tu huwa nachezwa na machale mwanzoni kabisa mwa gemu.... kiasi kwamba na mimi nimegeuka kuwa mtaalamu sasa hasa nikikutana na Traffic......

Sikiliza nilivyomtapeli Traffic, natoka Dar naenda Morogoro, mbele kidogo ya Chalinze kuna vibwana mdogo vinashinda pale na nguo zao nyeupe na Kitochi chao wanakua wamejificha infact wanakuvizia! Ghafla hawa hapa, nikasimama, wakanifuata wakaanza maelezo marefuuuuuu ila nikawasihi sana Sanaa kuwa kwa muda ule sikua na kitu na kwamba wanisamehe tu, wakakomaa kabisa, nikaona isiwe shida. Nikamwambia kuwa nauza simu kwahio kama atakubali nimapatie ile simu halafu yeye aniongeze pesa kidogo baada ya ku-deduct pesa yake ya Fine, Dogo akajaa, kuangalia kitu iTel kubwaaa, screen kubwa, hahahahahaaa. Akaitest inawaka safi kabisa nini, nikamwambia anipe mia themanini tu, akaanza kulialia paleee, tukashushana hadi hadi mia ishirini, ukikata fine yake 30 elfu inabaki 90 elfu, nikaona haina shida.

Akafungua Kofia yake (kumbe pesa wanafichia kwenye kofia) akanihesabia change, nikaweka mguu kati nikatimka! Hahahahaha nadhani mpaka kesho atakua ananisubiri wakati nilirudi Dar saa moja kasoro. The issue is, ile simu ukiweka chip haifanyi kazi, hai-detect simcard, nimepeleka kwa mafundi kibao imeshindikana. Ngoja nae apeleke kwa mafundi wake pia. akome kupenda vya dezo na rushwa

Hope na wewe hiyobsimu ulipigwa hapo mwanzo, so wewe na trafiki ni =
 
Umejuaje best!!! Alilamba kidole chake akasugua kwenye vumbi then akanisugua mkononi ukatoka moshi mwingiiiiiii huku anaongea makorokocho, hapo akili ikapaaa akanambia niende karibu na kanisa fulan eti nikifika niseme utukufu juu mbinguni na amani dunian ntaona Pete ya Bahati inashushwa! Daaah waliniweza wale jamaaa nikikumbuka nachekaa😀
Duuuh pole sana. Haya yakikukuta ndo unakuwa mjanja.
 
Pasaka hii hakuna alopigwa?
 
Nakumbuka ilikuwa miaka ya tisini mwanzoni,brother wangu alitapeliwa mnazi mmoja pale. Siku hiyo asubuhi aliaga anaenda shule boarding iringa,akaondoka na baraka zote za wazazi,ghafla saa nne asubuhi asharudi home anahema kichizi,wazee wakamuuliza kulikoni hujaenda shule?akawakusanya wazazi chumbani wakajifungia mi nikawa nachungulia ,bro akatoa kidude flan hivi nikamsikia anasema dhahabu,aisee wazee wakaenda funga mageti yote nje,bro akawaambia alikutana na msukuma stand eti aliokota hiko kidude ila yeye hakitaki kimeandikwa GOLD FIRST CLASS FROM ..nimesahau jina la mgodi akaamua mpa nauli ya ke ya bus to iringa na poketi money yote. Aisee ile ishu iliwachanganya wazee wakajua utajiri huu. Milango imefungwa home hamna wa kutoka mpaka mimi wanani ignore,ikafika usiku wa saa nne wakatoka kwenda kwa mzee jirani yeye mtaalam wa madini hahaha,yule mzee akawasha stovu akayaiunguza yale mawaya dooh yakawa meupe na biashara ikaishia hapo.
Hahahaaa kweli pesa haina ndugu mkapa wewe wakawa wanakupotezea
 
Jaman wa kwenye mpesa nao watupe uzoef...maana vilio ni vingi
 
Kuna jamaa walikuja na mfuko umetuna kweli kuashiria kuna kitu kizito wakaniambia braza tuna gearbox ya rav4 tunaipeleka gereji ilikuwa mida ya saa tatu usiku nikafungua buti la gari wakapakia tukaondoka kufika nyamongoro mmoja akasema niazime 30000/= tukifika huko nitakupa zote na hii ya tripu nami kiroho safi nikampa kufika kisesa wakashuka wakasema wanachukua tairi kwa jamaa yao nilikaa kusubiri mpaka saa sita hawajafika nikaamua kuondoka nafika kijiwani kufungua niangalie hiyo gearbox aisee nilichoka kulikuwa na mawe kwenye mfuko nikawa nimeingizwa mjini ndani ya jiji stasahau
 
Back
Top Bottom