Namshukuru MUNGU sijawahi kutapeliwa hata siku moja Zaidi ya kuwaokoa watu wengine, nimeshaokoa watu Zaidi ya wane kwa utapeli wa Simu/dawa za kutunzia samaki/Matrekta n.k. Sijisifu ila namshukuru MUNGU tu huwa nachezwa na machale mwanzoni kabisa mwa gemu.... kiasi kwamba na mimi nimegeuka kuwa mtaalamu sasa hasa nikikutana na Traffic......
Sikiliza nilivyomtapeli Traffic, natoka Dar naenda Morogoro, mbele kidogo ya Chalinze kuna vibwana mdogo vinashinda pale na nguo zao nyeupe na Kitochi chao wanakua wamejificha infact wanakuvizia! Ghafla hawa hapa, nikasimama, wakanifuata wakaanza maelezo marefuuuuuu ila nikawasihi sana Sanaa kuwa kwa muda ule sikua na kitu na kwamba wanisamehe tu, wakakomaa kabisa, nikaona isiwe shida. Nikamwambia kuwa nauza simu kwahio kama atakubali nimapatie ile simu halafu yeye aniongeze pesa kidogo baada ya ku-deduct pesa yake ya Fine, Dogo akajaa, kuangalia kitu iTel kubwaaa, screen kubwa, hahahahahaaa. Akaitest inawaka safi kabisa nini, nikamwambia anipe mia themanini tu, akaanza kulialia paleee, tukashushana hadi hadi mia ishirini, ukikata fine yake 30 elfu inabaki 90 elfu, nikaona haina shida.
Akafungua Kofia yake (kumbe pesa wanafichia kwenye kofia) akanihesabia change, nikaweka mguu kati nikatimka! Hahahahaha nadhani mpaka kesho atakua ananisubiri wakati nilirudi Dar saa moja kasoro. The issue is, ile simu ukiweka chip haifanyi kazi, hai-detect simcard, nimepeleka kwa mafundi kibao imeshindikana. Ngoja nae apeleke kwa mafundi wake pia. akome kupenda vya dezo na rushwa