TheDreamer Thebeliever
JF-Expert Member
- Feb 26, 2018
- 2,490
- 3,534
Habari wadau poleni sana na msiba wa jemedari Hayati Magufuli.
Leo nimeamua kuwaletea simulizi ya kweli inayoitwa "jinsi teseka miaka mingi na kunusurika kufa baada ya kurogezewa uchawi wa bundi".
Kwanza niwaombe samahani kwa mwandiko mbaya maana simulizi hii ninapoanza kuiandika inaweza kuonekana fupi ila inaweza ikawa ndefu hivyo basi mniwie radhi kama kutakuwa na kukatishwakatishwa.
Wahusika wa story ni watu wa kweli kabisa wala sio watu wa kufikirika na maeneo ni ya kweli sio ya kufikirika,ila ningeomba kutumia majina ya kufikirika maana sio vizuri kutumia majina yao halisi.
Lengo la kuleta story ni watu wajifunze wajue uchawi na uganga dunia upo na waganga wa kweli wapo,pia kuburudisha hilo ndio lengo.
Twende kwenye story yenyewe...
Ilikuwa mwaka 1975 katika kijiji cha Bunduki kata ya Bunduki wilayani Mvomero mkoa wa Morogoro ndipo simulizi ilipoanzia.
Nakumbuka kipindi hicho nilikuwa darasa la tano katika shule moja ya msingi kijijini hapo ambayo sitopenda kuitaja jina.Siku hiyo nilirudi nyumbani mishale ya saa 8 mchana nikiwa nimechoka sana na nilipofika nyumbani nikakuta kuna kasherehe ka kumtoa mwali, kama unavyojua tamaduni zetu za kiafrika hivyo watu walikuwa wamejaa sana huku wakipiga ngoma ijulikanayo kama Mbeta hii ni ngoma maarufu sana kwa wenyeji wa mkoa wa Morogoro hususa wa kabila la waruguru.
Nilifika nyumbani nikaingia ndani kubadilisha nguo za shule ambazo zilikuwa chafu zilizochakaaa na udongo wa kijijini kama wengi tunavyojua udogo wa Morogoro nakukimbia fasta kwenye ngoma.
Mwanamwali alikuwa ni dada yangu aliyenitangulia kwa sasa ana kama miaka 75 (watu wa zamani sana wengi wao hawajui miaka yao halisi ,hususa wale ambao hawakuenda shule .Huwa wanaweza kukutajia tu kipindi ,msimu au matukio ww ndio utang'amua umri wa makadilio wa mtu huyo kama haufahamu kuhusu matukio au vipindi hivyo vilitokea lini unaweza kushindwa hata kukadiria umri halisi).Hivyo basi umri wa dada kama miaka 75 katika simulizi hii ni kama makadirio tu wala visikupe shaka juu ya ukweli na uhalisia wa simulizi hii..
Basi baada ya kubadilisha nguo na kuingia moja kwa moja kwenye uwanjani ambapo mwanamwali ambaye ni dada yangu anachezwa hapo ndipo story, visa, mkasa, simanzi zilipoanzia.
Hapo kutakuwa na mambo ya kuvunja nazi, makafala ya wanyama kama mbuzi au ng'ombe na shughuri zingine pamoja na kufukia vitu au dawa kwenye makabuli au miti mikubwa kama ni matambiko.
Kwa wenyeji wa Pwani wanatambua utamaduni wetu kama kawaida ngoma inapowekwa uwanjani siku au wiki kabla haiawekwa uwanjani lazima watu waende kwa mganga kuzindika au wanaweza wakawaita wazee kufanya matambiko. Matambiko au mazindiko lazima yatanuwiwa kwamba yeyote atakayekuja kwa ubaya siku ya sherehe au shughuri ya kumtoa mwanamwali wetu basi haondoke kwa ubaya.
Nasi tulifuata taratibu zote za zindiko na matambiko kama utamaduni wetu lakini sasa siku hiyo mambo yalikuwa tofauti yaani chuma kilikutana na chuma.
Tukumbuke tupo mwaka 1975 kipindi hicho dini na imani hazikuwa zimeenea sana kivile hivyo hatukuwa na budi katika kuamini mizimu ,matambiko,mazindiko na vinginevyo.
Inandelea...
Leo nimeamua kuwaletea simulizi ya kweli inayoitwa "jinsi teseka miaka mingi na kunusurika kufa baada ya kurogezewa uchawi wa bundi".
Kwanza niwaombe samahani kwa mwandiko mbaya maana simulizi hii ninapoanza kuiandika inaweza kuonekana fupi ila inaweza ikawa ndefu hivyo basi mniwie radhi kama kutakuwa na kukatishwakatishwa.
Wahusika wa story ni watu wa kweli kabisa wala sio watu wa kufikirika na maeneo ni ya kweli sio ya kufikirika,ila ningeomba kutumia majina ya kufikirika maana sio vizuri kutumia majina yao halisi.
Lengo la kuleta story ni watu wajifunze wajue uchawi na uganga dunia upo na waganga wa kweli wapo,pia kuburudisha hilo ndio lengo.
Twende kwenye story yenyewe...
Ilikuwa mwaka 1975 katika kijiji cha Bunduki kata ya Bunduki wilayani Mvomero mkoa wa Morogoro ndipo simulizi ilipoanzia.
Nakumbuka kipindi hicho nilikuwa darasa la tano katika shule moja ya msingi kijijini hapo ambayo sitopenda kuitaja jina.Siku hiyo nilirudi nyumbani mishale ya saa 8 mchana nikiwa nimechoka sana na nilipofika nyumbani nikakuta kuna kasherehe ka kumtoa mwali, kama unavyojua tamaduni zetu za kiafrika hivyo watu walikuwa wamejaa sana huku wakipiga ngoma ijulikanayo kama Mbeta hii ni ngoma maarufu sana kwa wenyeji wa mkoa wa Morogoro hususa wa kabila la waruguru.
Nilifika nyumbani nikaingia ndani kubadilisha nguo za shule ambazo zilikuwa chafu zilizochakaaa na udongo wa kijijini kama wengi tunavyojua udogo wa Morogoro nakukimbia fasta kwenye ngoma.
Mwanamwali alikuwa ni dada yangu aliyenitangulia kwa sasa ana kama miaka 75 (watu wa zamani sana wengi wao hawajui miaka yao halisi ,hususa wale ambao hawakuenda shule .Huwa wanaweza kukutajia tu kipindi ,msimu au matukio ww ndio utang'amua umri wa makadilio wa mtu huyo kama haufahamu kuhusu matukio au vipindi hivyo vilitokea lini unaweza kushindwa hata kukadiria umri halisi).Hivyo basi umri wa dada kama miaka 75 katika simulizi hii ni kama makadirio tu wala visikupe shaka juu ya ukweli na uhalisia wa simulizi hii..
Basi baada ya kubadilisha nguo na kuingia moja kwa moja kwenye uwanjani ambapo mwanamwali ambaye ni dada yangu anachezwa hapo ndipo story, visa, mkasa, simanzi zilipoanzia.
Hapo kutakuwa na mambo ya kuvunja nazi, makafala ya wanyama kama mbuzi au ng'ombe na shughuri zingine pamoja na kufukia vitu au dawa kwenye makabuli au miti mikubwa kama ni matambiko.
Kwa wenyeji wa Pwani wanatambua utamaduni wetu kama kawaida ngoma inapowekwa uwanjani siku au wiki kabla haiawekwa uwanjani lazima watu waende kwa mganga kuzindika au wanaweza wakawaita wazee kufanya matambiko. Matambiko au mazindiko lazima yatanuwiwa kwamba yeyote atakayekuja kwa ubaya siku ya sherehe au shughuri ya kumtoa mwanamwali wetu basi haondoke kwa ubaya.
Nasi tulifuata taratibu zote za zindiko na matambiko kama utamaduni wetu lakini sasa siku hiyo mambo yalikuwa tofauti yaani chuma kilikutana na chuma.
Tukumbuke tupo mwaka 1975 kipindi hicho dini na imani hazikuwa zimeenea sana kivile hivyo hatukuwa na budi katika kuamini mizimu ,matambiko,mazindiko na vinginevyo.
Inandelea...