Emc2
JF-Expert Member
- Sep 26, 2011
- 16,808
- 16,951
- Thread starter
- #261
Ehee sasa hapa tunaanza kwenda pamoja.Na rais akiondoa haki bila ya kuwepo maslahi ya umma inakuwaje?
Maslahi ya umma ni nini?
Nani anaamua haya ni maslahi ya umma na haya si maslahi ya umma?
Utajuaje hapa haki imeondolewa kwa maslahi ya umma na hapa haki imeondolewa kwa maslahi ya chama au wanene wachache?
Kama kuwanyima wapinzani kuandamana kunaweza kuleta kinyongo kitakachosababisha mpasuko katika jamii, na kuwaachia waandamane hakuna hasara yoyote ilimradi wanaandamana kwa Amani, na wapinzani wameahidi kuandamana kwa amani, rais kuwanyima kuandamana ni kulinda maslahi ya umma kivipi?
Maslahi ya umma yana julikana kwenye mamlaka na kiongizi wa mamlaka ni rais.
Kwa hiyo basi mwenye kujua haya ni maslahi ya umma na haya siyo maslahi ya umma ni mamlaka.
Sasa basi haki na uhuru upo chini ya mamlaka kutikana na hekima na uzalendo sio shinikizo la maandamano.