Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 25,176
- 48,460
Usistake kujifunza sheria kupitia JF.
Ndio maana nimekupa hizo ibara kutokana na kwamba hakuna ibara ndani ya katiba inayoongelea vyama vya siasa kufanya mikutano.Nimekuuliza "Ibara ya juu ya thread ipi inasema rais ana mamlaka ya kupiga marufuku mikutano ya siasa?"
Ibara ya 29 na 30 hazijamtaja rais kabisa.
Ibara ya 31(4) imeeleza tu kwamba "hali ya hatari" itatangazwa na rais.
Lini rais Magufuli katangaza hali ya hatari? Unafahamu tamko la kutangaza hali ya hatari linakuwaje?
Hii marufuku aliyopiga sasa hivi Magufuli, kaipiga kwa ibara gani ya katiba?
Hujajibu swali langu.Ndio maana nimekupa hizo ibara kutokana na kwamba hakuna ibara ndani ya katiba inayoongelea vyama vya siasa kufanya mikutano.
Serikali ndio iliyopewa mamlaka kuhakikisha watu wanafuata makubaliano yaliyomo kwenye katiba. Na kiongozi mkuu wa serikali ni rais.
Kwa misingi hiyo sasa kwamba kwakuwa hakuna ibara ndani ya katiba inaongelea vyama vya siasa kufanya mikutano isipokuwa tu kutokana na ibara ya 18 inayoongelea uhuru wa kukusanyika. Na ule uhuru na haki ya kukusanyika umepewa limitation kwenye ibara ya 29,30 na 31.
Sasa basi ile mikutano ya kisiasa inabanwa na ibara hizo kwamba haki ya wachache isije ikanyima haki watu wengi. Na serikali pekee ndiyo inayosimamia na kuhakikisha katiba haivunjwi.
Basi kifupi tu niambie ni nani anaye hakikisha ibara ya 29 na 30 hazivunjwi?Hujajibu swali langu.
Hujanionesha ni wapi rais amepewa mamlaka ya kupiga marufuku mikutano ya kisiasa.
Umeweka ibara za 29, 30, 31.
Nimezisoma.
29 na 30 hata hazimtaji rais.
31 imetaja rais katika context ya kuwa hali ya hatari itatangazwa na rais.
Hakuna popote pale kati ya hizo ibara iliposemwa kwamba rais ana mamlaka ya kupiga marufuku mikutano ya siasa kama alivyopiga marufuku sasa.
Watanzania wote wana wajibu wa kuilinda na kuitetea katiba.Basi kifupi tu niambie ni nani anaye hakikisha ibara ya 29 na 30 hazivunjwi?
Hapo umesema vyema lakini tu kunakimoja hujamalizia kwamba serikali ndiyo inayosimamia ili raia waweze kuilinda na kuitetea.Watanzania wote wana wajibu wa kuilinda na kuitetea katiba.
Kweli kazi yake ni nini!Na dawa ya mswaki kazi yake ni nini?
Serikali ni nini ?Hapo umesema vyema lakini tu kunakimoja hujamalizia kwamba serikali ndiyo inayosimamia ili raia waweze kuilinda na kuitetea.
Sasa basi kwa mantiki hiyo ya serikali kusimamia ibara ya 29 na 30 inaipa serikali meno ya kuweka limitation ya haki na uhuru. Na rais ndiye kiongozi wa serikali.
Jifikirie tena,Kwanini unasema hivyo?
Naona sasa bwana Kiranga umeanza kuandika hekaya.Serikali ni nini ?
Unafahamu kwamba wanaoendesha serikali ni vijakazi tu wa wananchi?
Utasemaje housegirl ndiye ana mamlaka ya kuweka limitation ya haki na uhuru wa baba mwenye nyumba atakula nini na nini asile katika nyumba yake mwenyewe?
You have it backwards. Hao viongozi wa serikali wanawajibika kwa wananchi. Wananchi hawawajibiki kwa viongozi wa serikali.
Furahia cku yako mkuu.Ushuri wako unamanisha nini?
Hufahamu kwamba representative democracy ni social contract inayowapa wanaochaguliwa mandate ya kuwa custodians inayotoka kwa wananchi?Naona sasa bwana Kiranga umeanza kuandika hekaya.
Naomba tuongee facts.
Sasa kama rais amezuia wewe kikatiba unatakiwa ufanye nini sasa?Hufahamu kwamba representative democracy ni social contract inayowapa wanaochaguliwa mandate ya kuwa custodians inayotoka kwa wananchi?
Na kwamba kuwa custodian hakuna maana wewe ni mfalme usiye na mipaka, unaamua tu kupiga marufuku mikutano ya kisiasa bila kutumia kifungu chochote cha katiba?
Magufuli katumia kifungu gani cha katiba kupiga marufuku mikutano ya siasa?
Hujanipa hicho kifungu bado.
Impeach his ass.Sasa kama rais amezuia wewe kikatiba unatakiwa ufanye nini sasa?
Wewe naona unahasira zako binafsi. Nimekuuliza kikatiba unatakiwa ufanyenini? Taja kifungu cha katiba kulingana na hicho unachokisema.Impeach his ass.
Kitu ambacho Kibongo hakiwezi kufanyika kwa sababu watu wanamuona rais kama Mungu mtu halafu wanaendekeza maslahi ya watu wachache dhidi ya yawengi.
Twende taratibu ndugu! Ibara ya 17.-(1) inasema: "Kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kwenda kokote katika Jamhuri ya Muungano na kuishi katika sehemu yoyote, kutoka nje ya nchi na kuingia, na pia haki ya kutoshurutishwa kuhama au kufukuzwa kutoka katika Jamhuri ya Muungano."30.-(1) Haki na uhuru wa binadamu ambavyo misingi yake imeorodheshwa katika Katiba hii havitatumiwa na mtu mmoja kwa maana ambayo itasababisha kuingiliwa kati au kukatizwa kwa haki na uhuru wa watu wengine au maslahi ya umma.
Sawa kabisa! Ikiwa inathibitika CHADEMA wanakiuka sheria basi watakuwa wanavunja Katiba kwa kuanagalia Ibara ya 30 (2). Swali: Je, kuna sheria yoyote wanayovunja?(2) Ifahamike kwamba masharti yaliyomo katika Sehemu hii ya Katiba hii, yanayofafanua misingi ya haki, uhuru na wajibu wa binadamu, hayaharamishi sheria yoyote iliyotungwa wala kuzuia sheria yoyote kutungwa au jambo lolote halali kufanywa kwa mujibu wa sheria hiyo, kwa ajili ya -
Hufahamu kifungu cha katiba kinachoongelea impeachment?Wewe naona unahasira zako binafsi. Nimekuuliza kikatiba unatakiwa ufanyenini? Taja kifungu cha katiba kulingana na hicho unachokisema.
Bwana Kiranga sitaki hekaya hapa. I need facts with references from constitution.