Jinsi Kampuni za Simu zinavyowaibia wateja wao!

Jinsi Kampuni za Simu zinavyowaibia wateja wao!

VODA wanaib jameni ...yuuuei.
Ukinunua soda ukaingiza zile namb kwenye kisude ile sms ikiwafikia ndo wsnsanza kuhesabu hizo dk 5, ikifika dk ya 4 ndo unapata sms keamba umefanikiwa kuunganishwa ,ukipiga unaambiwa ushatumi mda wako wa bure.

Hawa share holda watamjibu nn Mungu wa İsrael ?

mkuu, ngoja tu tuendelee kuibiwa. kuna siku nilisikia TCRA wanatetea wizi huu iliniuma sana.
 
Last edited by a moderator:
Hivi mnajua hii mitandao ya simu nchini inakichangia Chama Tawala shs ngapi kwenye Uchaguzi mkuu? Voda ndio partner mkubwa wa CCM.
Mnafikiri hizi Kampuni za simu zitafidia vipi michango mikubwa zinazodaiwa na CCM.?

Mnafikiri TCRA haifahamu huu wizi unaofanywa na hizi Kampuni?
 
Jinsi Vodacom walivyonisumbua kwa takribani miaka mitano(hapo ni baada ya kuhangaika na mitandao mingine pia)...Dawa sasa hivi ninatembea na vocha kwenye wallet tu..nikitaka kutumia ndio ninaweka(natuma sms afu napiga simu) hadi salio liishe.
 
Mkuu kama Mimi simu yangu nikijiunga na kifurushi halafu nikaweka buku lina zurura tu kwenye simu kesho nakuta 250 kesho kutwa nakuta shillings 0 kabisa.ila siku hiz nimeshtuka nawaachia shillings 5 tu kwenye salio wakakate Mbele ya safari huko.

kweli kabisa mkuu, ni bora kuweka vocha 500 maana ukiacha fedha nyingi kwenye simu ndio mwanzo wa kuibiwa.

mimi huwa nanunua vocha nyingi za 500 nakaa nazo na kuziweka tu pale ninapotaka kununua kifurushi.

wakuu, hili ni suluhisho mojawapo ambalo kila mtu anapaswa kulizingatia maana ukitegemea suluhisho la kiufundi kutoka TCRA huwezi kulipata kamwe.kila mtu achukue tahadhari ya fedha zake mwenyewe.
 
Last edited by a moderator:
Mleta uzi hebu uambie kuhusu Zantel? Uliwahi kufanya kazi hapo mimi ni mteja lakini sijawahi kukumbana na matatizo yoyote na sitaki kusikia habar za voda wa Tigo nimewaacha kitambo sana

mkuu, na huko airtel mtindo ni huo huo...ni WEZI wakubwa!
 
Ahsante Mkuu kwa kutupa taarifa. Kumbe nilikuwa sahihi kutojiunga kwenye promosheni zao. Ila Mkuu umelea tatizo muda mrefu. Ungetutonya mapema. Miaka kumi mingi sana watanzania tumeumizwa.

Hata usipojiunga unalazimishwa kuingizwa bila kujua huku wakichukua pesa yako bila maelezo yoyote. We jaribu siku angalia salio asubuhi, siku hiyo usipige simu kabisawala kutuma sms, kesho yake angalia salio asubuhi uone halafu wapigie simu (ukibahatika kupokelewa) usikie majibu yao.
 
Niko njiani ngoja nitafanya screen shot ya kilichotokea jana. tpaul i promise kuweka ushahidi wa picha ngoja nitulie maana imenibidi nizime simu moja yenye hio issue ili wasiendelee kunikata pesa

mkuu Elli hebu tuwekee ushahidi hapa. hv ni lini hawa mafisadi watakoma kutunyonya? nchi hii ni shamba la bibi. tunaishi maisha ya baharini...samaki wadogo ni chakula cha samaki wakubwa!
 
Last edited by a moderator:
mkuu, ushahidi huu sijakaa nao muda mrefu kihivyo...nimeondoka huko mitandaoni mwaka 1 uliopita. hizi kampuni ni wezi wa kutupwa na wanafanya haya kwa sababu ya udhaifu wa nchi yetu. tunazo mamlaka kama TCRA lakini haziwezi kutusaidia walaji tusinyonywe na hawa mafisadi.
sio kwamba tcra na wenyewe ndio walewale tu..
 
Last edited by a moderator:
VODA wanaib jameni ...yuuuei.
Ukinunua soda ukaingiza zile namb kwenye kisude ile sms ikiwafikia ndo wsnsanza kuhesabu hizo dk 5, ikifika dk ya 4 ndo unapata sms keamba umefanikiwa kuunganishwa ,ukipiga unaambiwa ushatumi mda wako wa bure.

Hawa share holda watamjibu nn Mungu wa İsrael ?

yap hilo likinitokea
 
Nimefanya kazi kwenye kampuni mbali mbali za simu hapa nchini kwa muda wa zaidi ya miaka 10, kabla ya kuamua kujiajiri mwenyewe. Katika muda wote huo nimeshuhudia kampuni hizi zikiwaibia wateja kwa namna mbalimbali. Nimekaa na huu ushahidi kwa muda sasa lakini naona roho inanisukuma niuanike hadharani mbele za watanzania ili wafunguke macho na kufahamu UFISADI huu unaofanywa na kampuni za simu hapa nchini. Nitaanika wizi wote kadri nitakavyoweza kuukumbuka hapa:

Huduma za bure
Kuna hizi huduma ambazo wanaziita huduma za “BURE” kana kwamba zinapatikana bure wakati si kweli! Kwa mfano, wateja hutumiwa SMS zinazowadanganya kwamba wanaweza kupata huduma za bure na ili wazipate wanaelekezwa kutuma ujumbe kwenda kwenye namba fulani. Na mteja akisharogwa akatuma ujumbe kwenda kwenye namba husika, imekula kwake! Nyingi ya huduma hizi zinzoitwa za bure hugharimu fedha na mara ujiungapo hujikuta unakatwa salio lako kimya kimya. Ni mara nyingi mtakuwa mmewahi kusikia mtu akilalamika kwamba salio lake limepungua….unaweka airtime ya Tsh 1000 leo bila kuitumia, ikifika kesho unakuta zimebaki sh 350! Tsh 650 zimeenda wapi? Zimekatwa kwenye zile huduma za “BURE” ulizotangaziwa.

Promosheni feki
Promosheni nyingi zinazoanzishwa na makampuni ya simu zinalenga kuwanyonya na kuwakandamzia wateja. Mfano halisi ni pale wateja wanapotangaziwa kwamba huduma ya FESIBUKU inapatika bure! Thubutuuu! Hakuna kitu cha bure nchi hii, ndugu yangu. Huu ni wizi wa mchana! Kupona kwako ni pale utakapotumia hiyo huduma ukiwa hauna salio kwa kuwa huwezi kupata access ya huduma husika (kama vile fesibuku, twita, nk). Ikiwa utafungua huduma hiyo ukiwa na salio, salio lako lote litakombwa sawia! Kuna mtandao mmoja wa simu unajinadi kwamba unatoa huduma ya fesibuku bure wakati ni uongo mtupu. Ingia kwenye hiyo fesibuku uone utakavyoliwa fedha! Aidha kuna mtandao mmoja uliwahi kuwa na fesibuku ya bure siku za nyuma (kama mtakumbuka). Kwa muda fulani huduma hii ilikuwa ikipatikana bure kabisa. Kumbe ilikuwa ni janja ya nyani…..baadaye ile “bure” ilifutwa kimya kimya, wateja wakaendelea kukamuliwa kama kawaida na mpaka leo hawajawahi kuwataarifu wateja wao kwamba hiyo “bure” imesitishwa! Kuna wateja wengi sana, hasa wa kule vijijini, ambao wanaendelea kukamuliwa kwa kujidanganya kwamba huduma ni ya bure hadi leo, kumbe ilishasitishwa kitambo sana!

Ulaghai wa Kimangungo
Kuna wakati ambapo makampuni ya simu hupandisha tariffs kimya kimya bila kuwataarifu wateja wake na kuendelea kuwaibia bila kujua. Mwaka 2006 gharama za kupiga simu, kutuma sms na kutumia data zilipandishwa kinyemela na wateja wakaendelea kukamuliwa fedha kimya kimya hadi pale baadhi yao waliposhtukia dili na kuja juu. Aidha, prosheni fulani zinapoanzishwa, kama vile punguzo la gharama za kupiga simu nyakati za usiku, pindi zinafikia tamati wateja hawapewi taarifa na kujikuta wakitumia fedha zaidi ya matarajio yao. Promosheni inapoisha kampuni hizi huwakataza wafanyakazi wake wasiwaambie wateja ili waendelee kukamuliwa fedha kilaghai. Huu ni wizi, tena wa mchana na hauna tofauti na ufisadi wowote ule.

Kutotoa taarifa kwa wateja kwa makusudi
Wateja wanapojiunga kwenye vifurushi mbalimabli huletewa taarifa immediately via SMS kwamba wamefanikiwa kujiunga lakini kifurushi kikiisha ama wateja huchelewa kutumiwa meseji ya taarifa au hawatumiwi kabisa. Hili tatizo huwakumba zaidi wale wateja wanaopenda kubaki na salio kubwa kwenye simu zao. Kwa mfano, mtu unanunua vocha ya Tsh 2000 kisha unanunua kifurushi cha Tsh 500 na kubakiwa na Tsh 1500 kwenye simu. Pindi kifurushi cha 500 kikiisha hutatumiwa ujumbe wowote hadi utapokuwa umekausha 1500 zilizosalia kwenye simu. Huu pia ni wizi wa mchana na unaofanywa kwa makusudi na kampuni za simu hapa nchini. Ninao ushahidi usiokuwa na mashaka katika huu wizi wa makusudi.

Njia nyingine inayotumika kuiba hapa ni kutotoa call details pindi upigapo simu. Ukimaliza kupiga simu ukiangalia call details unakuta inasoma 00:00:00! Details hizi zinafichwa kwa makusudi ili kujenga mazingira ya wizi. Kwa mfano mtu unaongea kwa dakika 3, wao wanakata dakika 4.30 na kukuibia dakika 1.30! Matokeo yake unakuta muda wa hewani uliopewa wakati wa kujiunga umeibiwa na kampuni kwa maslahi yake binafsi. Lakini pia kuna wizi mwingine huu hapa: – unaponunua kifurushi hupewa dakika ambazo ungetegemea zizotozwe kwa sekunde (per second billing) lakini badala yake hutozwa kwa dakika (per minute billing) kinyume cha mkataba kwa lengo la kumkamua mteja kiujanja. Huu ni wizi na haukubaliki hata kidogo.

Kuvuruga mawasiliano kwa makusudi
Kuna wakati wahandisi wa kampuni husika hupewa jukumu la kuvuruga mawasiliano ya wateja ili watumie muda mwingi na pesa nyingi kwenye maongezi. Inakuwaje hapa? Inakuwa hivi: Ukimpigia mtu yeye anakuwa anakusikia lakini wewe humsikii au vice versa. Hii husababisha kutumia muda mwingi kuelewana wakati huo salio likinyonywa kama kawaida – hata kama mkichukua muda mwingi kuelewana salio hutafunwa sawia! Njia nyingine inayotumika hapa ni kuvuruga access to customer care ili unapokuwa umepatwa na tatizo usiweze kuwafikia watu wa huduma kwa wateja kupata msaada. Hii ndio sababu 90% ya wateja wenye matatizo genuine hawaipati namba 100. Mtu unaweza kupiga siku nzima na usiunganishwe kuongea na mshauri. Hatimaye wengi wao hukata tamaa na kuamua kukubali “kuliwa”!

Hii ni sehemu ya ushahidi ambao nimeukusanya while working with different mobile companies in Tanzania. Siwezi kuwa adui kwa kusema ukweli.

Nawasilisha.

:yield:

mkuu hizi michezo za bahati nasibu....washind wanakuwa n wa kweli au n waku tengenezwa....?
 
Ndiye Mungu aliyeumba mbingu na nchi, huyu ni Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakobo. Jina lake ni Jehova! Barikiwa!

Sa mbona umesema ni Israel? Africa je? Europe? America? Other planets?
 
Back
Top Bottom