Chinga One
JF-Expert Member
- May 7, 2013
- 11,493
- 12,453
Moderators tunaomba huu uzi uwe sticky tafadhali.
Ukweli mtupu....
Tigo nafikiri ndo wahuni wakubwa..
sasa kumbukeni CCM imetunyonya kwa miaka 50.. lakini wapo watu wanaishabikia.. kama tunakataa wizi huu wa mitandao tukumbuke pia kukutaa wizi wa CCM hapo mwakani 2015
Wateja wanapojiunga kwenye vifurushi mbalimabli huletewa taarifa immediately via SMS kwamba wamefanikiwa kujiunga lakini kifurushi kikiisha ama wateja huchelewa kutumiwa meseji ya taarifa au hawatumiwi kabisa. Hili tatizo huwakumba zaidi wale wateja wanaopenda kubaki na salio kubwa kwenye simu zao. Kwa mfano, mtu unanunua vocha ya Tsh 2000 kisha unanunua kifurushi cha Tsh 500 na kubakiwa na Tsh 1500 kwenye simu. Pindi kifurushi cha 500 kikiisha hutatumiwa ujumbe wowote hadi utapokuwa umekausha 1500 zilizosalia kwenye simu. Huu pia ni wizi wa mchana na unaofanywa kwa makusudi na kampuni za simu hapa nchini. Ninao ushahidi usiokuwa na mashaka katika huu wizi wa makusudi
Mungu wa Ibrahim, Isaka ns Yakobo wewe akuhusu nini!!??????????
Ahsante Mkuu kwa kutupa taarifa. Kumbe nilikuwa sahihi kutojiunga kwenye promosheni zao. Ila Mkuu umelea tatizo muda mrefu. Ungetutonya mapema. Miaka kumi mingi sana watanzania tumeumizwa.