Zurie
JF-Expert Member
- Jul 6, 2014
- 1,745
- 4,277
Wakati Yesu anaanza kazi ya kutangaza ufalme wa Mungu Yosefu kuna uwezekano mkubwa alikuwa marehemu. Nasema kuna uwezekano kwa sababu hakuongelewa so hakuna uhakika kutoka biblia(kabla sijaombwa mstari wa kifo chake) lakini kuna viashiria.kwahiyo wakati Yesu anaanza kazi ya kutangaza ufalme wa Mungu akiwa na umri wa miaka 30 Yosefu alikuwa ameshagonga miaka 100?
Yesu akiwa msalabani alimkabidhi Mama yake kwa Yohana (Yohana 19: 26-27) ikimaanisha kuwa Yosefu alikuwa marehemu hivyo mama yake angebaki mpweke. Sababu hii ya kifo cha Yosefu ndiyo hupelekea dhana ya kuwa Yosefu alikuwa mzee hivyo alikufa kutokana na uzee.
Kingine ni kuwa Maria anaaminika kubaki bikra hadi kufa kwake. Hii inaweza kuaminika endapo tu Yosefu alikuwa mzee wa makamo hivyo hakuwa na shauku na mwali wake.
Vilevile Yesu alikuwa na kaka zake kama inavyoelezwa kwenye injili ya Mathayo 13:55-56 wakitajwa kwa majina Yakobo, Yusufu, Simoni na Yuda. Hawa wanaaminika walikuwa watoto wa Yosefu aliwapata kabla ya kuwa na Maria. Hitimisho ni kuwa maandiko japo hayajasema ila yanaashiria Yosefu alikuwa mzee wa makamo.