Jinsi Bikra Maria alivyompa mtihani kiongozi wa Kanisa, Nabii Zakaria..

kwahiyo wakati Yesu anaanza kazi ya kutangaza ufalme wa Mungu akiwa na umri wa miaka 30 Yosefu alikuwa ameshagonga miaka 100?
Wakati Yesu anaanza kazi ya kutangaza ufalme wa Mungu Yosefu kuna uwezekano mkubwa alikuwa marehemu. Nasema kuna uwezekano kwa sababu hakuongelewa so hakuna uhakika kutoka biblia(kabla sijaombwa mstari wa kifo chake) lakini kuna viashiria.

Yesu akiwa msalabani alimkabidhi Mama yake kwa Yohana (Yohana 19: 26-27) ikimaanisha kuwa Yosefu alikuwa marehemu hivyo mama yake angebaki mpweke. Sababu hii ya kifo cha Yosefu ndiyo hupelekea dhana ya kuwa Yosefu alikuwa mzee hivyo alikufa kutokana na uzee.

Kingine ni kuwa Maria anaaminika kubaki bikra hadi kufa kwake. Hii inaweza kuaminika endapo tu Yosefu alikuwa mzee wa makamo hivyo hakuwa na shauku na mwali wake.

Vilevile Yesu alikuwa na kaka zake kama inavyoelezwa kwenye injili ya Mathayo 13:55-56 wakitajwa kwa majina Yakobo, Yusufu, Simoni na Yuda. Hawa wanaaminika walikuwa watoto wa Yosefu aliwapata kabla ya kuwa na Maria. Hitimisho ni kuwa maandiko japo hayajasema ila yanaashiria Yosefu alikuwa mzee wa makamo.
 
Wakati Yesu anaanza kazi ya kutangaza ufalme wa Mungu Yosefu kuna uwezekano mkubwa alikuwa marehemu. Nasema kuna uwezekano kwa sababu hakuongelewa so hakuna uhakika kutoka biblia(kabla sijaombwa mstari wa kifo chake) lakini kuna viashiria.

Yesu akiwa msalabani alimkabidhi Mama yake kwa Yohana (Yohana 19: 26-27) ikimaanisha kuwa Yosefu alikuwa marehemu hivyo mama yake angebaki mpweke. Sababu hii ya kifo cha Yosefu ndiyo hupelekea dhana ya kuwa Yosefu alikuwa mzee hivyo alikufa kutokana na uzee.

Kingine ni kuwa Maria anaaminika kubaki bikra hadi kufa kwake. Hii inaweza kuaminika endapo tu Yosefu alikuwa mzee wa makamo hivyo hakuwa na shauku na mwali wake.

Vilevile Yesu alikuwa na kaka zake kama inavyoelezwa kwenye injili ya Mathayo 13:55-56 wakitajwa kwa majina Yakobo, Yusufu, Simoni na Yuda. Hawa wanaaminika walikuwa watoto wa Yosefu aliwapata kabla ya kuwa na Maria. Hitimisho ni kuwa maandiko japo hayajasema ila yanaashiria Yosefu alikuwa mzee wa makamo.
Aisee
 
Wakati Yesu anaanza kazi ya kutangaza ufalme wa Mungu Yosefu kuna uwezekano mkubwa alikuwa marehemu. Nasema kuna uwezekano kwa sababu hakuongelewa so hakuna uhakika kutoka biblia(kabla sijaombwa mstari wa kifo chake) lakini kuna viashiria.

Yesu akiwa msalabani alimkabidhi Mama yake kwa Yohana (Yohana 19: 26-27) ikimaanisha kuwa Yosefu alikuwa marehemu hivyo mama yake angebaki mpweke. Sababu hii ya kifo cha Yosefu ndiyo hupelekea dhana ya kuwa Yosefu alikuwa mzee hivyo alikufa kutokana na uzee.

Kingine ni kuwa Maria anaaminika kubaki bikra hadi kufa kwake. Hii inaweza kuaminika endapo tu Yosefu alikuwa mzee wa makamo hivyo hakuwa na shauku na mwali wake.

Vilevile Yesu alikuwa na kaka zake kama inavyoelezwa kwenye injili ya Mathayo 13:55-56 wakitajwa kwa majina Yakobo, Yusufu, Simoni na Yuda. Hawa wanaaminika walikuwa watoto wa Yosefu aliwapata kabla ya kuwa na Maria. Hitimisho ni kuwa maandiko japo hayajasema ila yanaashiria Yosefu alikuwa mzee wa makamo.

Asante sana kusaidia kunyoosha maelezo. Umeshiba neno. Nikifungua kanisa utakuwa mama mchungaji (kidding).

Kwa kujazia tu, Mzee Yosefu (nimezoea Joseph au Yusuf) alikuwa na hekima sana. Nadhani alitumiwa ujumbe wa kutomnajisi bibie Maria kwa sababu za kiungu ambazo pengine hazijajulikana bado.

Hiyo line ya mwisho hapo ni mawazo yangu binafsi
 
Mtaendelea kudanganyana hadi mtaingia kaburini aliye kuwambia Zakaria alikuwa Padri nani
 
Mtaendelea kudanganyana hadi mtaingia kaburini aliye kuwambia Zakaria alikuwa Padri nani
Ila mie siwezi mbishia mleta mada kuna wengine wanae yesu mwingine labda ndiye
anamsimulia sio huyu Yesu Kristo aliye sulubiwa msalabani
 
Wadau wa fikra,

Nafahamu kuwa muongozo wa Jukwaa hili unatutaka tuweke serious reports & discussions on Corruption, Politics na etc kwa ajili ya mijadala yakinifu. Tofauti na Jukwaa la Dini ambalo lengo lake kuu ni kuhamasishana kuhusu masuala ya kiimani na kufundishana yale yaliyo mema.

So, uzi huu hauna lengo la kuhamasishana kuhusu imani bali kujadiliana kwa kina kuhusu mambo ya kale (historical facts) yanayoingiliana kidogo na dini/imani. Naamini nimejaribu kuweka utofauti ili isionekane naleta mjadala wa kidini kwenye jukwaa hili makini.

Kupitia historia fupi ya Maria, nitaeleza mtihani wa Bikra Maria kwa Mkuu wa Kanisa/Hekalu alimolelewa, ambaye alikuwa ni Nabii Zakaria. Ni matarajio yangu tutaulizana maswali na kurekebishana kwa uungwana ili sote tuweze kuelimika na kufahamishana mambo mengi tusiyoyajua.

Hebu tuipitie historia hiyo kidogo..

Wazazi wake
Maria alizaliwa na Mzee Joachim na Bi. Anna ambao walikuwa ni wachamungu haswa. Kama ilivyokuwa kwa baadhi ya wachamungu wa enzi hizo, Mungu aliwapa mtihani wa ugumba Mr. & Mrs Joachim kiasi cha kudharaulika katika jamii kabla ya kuwainua kwa kuwapatia msichana mtakatifu Maria, baada ya kuzidisha kwao ibada na maombI.

Malezi yake
Watakatifu zamani walikuwa wakiweka nia kwa watoto wao watakaowazaa. Familia hii ya mzee Joachim na mkewe waliweka nadhiri kwamba endapo Mungu atawajaalia mtoto, basi watamtoa wakfu - yaani atatumika kwenye kazi za Mungu (utumishi). Hivyo, baada ya uzao wa Maria na kufikisha umri wa miaka 2/3 baada ya kuacha ziwa, walitekeleza ahadi yao kwa kumpeleka hekaluni kulelewa na Kiongozi wa hekalu ambaye alikuwa ni mzee Zakaria, mume wa Elizabeth (mama yake Yohana Mbatizaji).

Hekaluni palikuwa pakilelewa mabinti bikra kwa kuwa walizingatiwa kuwa wasafi na watakatifu zaidi. Kwahiyo binti Maria aliishi humo pamoja na mabinti bikra wengine na kufundishwa maadili mema pamoja na sheria za Mungu. Wazazi wake walikuwa wakimtembelea mara kwa mara mpaka alipofikia umri wa miaka 10 wakafariki dunia.

Ndoa
Alipofikisha umri wa miaka 13, yaani miaka mitatu baada ya wazazi wake kufariki, uongozi wa Kanisa uliamua Maria atoke hekaluni ili aweze kupata mume. Kwa mila na desturi za hekalu enzi hizo, binti akishavunja ungo anakuwa sio msafi tena hivyo hahitajiki kubaki hekaluni kwa sababu atalichafua. Hata hivyo, Maria alijenga hoja kwamba yeye wazazi wake waliamua kumtoa wakfu hivyo ameamua ataitunza bikra yake na kumtumikia Mungu maisha yake yote.

Jambo hili lilileta mtihani kidogo kwa mzee Zakaria kwa sababu ni unprecedented. Akalazimika kuitisha baraza la ushauri namna ya kudeal nalo ambapo uamuzi ulifikiwa kuwa aende altareni akiwa pekee aombe hekima ya Mungu. Usiku wake, alifanya hivyo na Malaika akamtokea na kumpa Muongozo kwamba aitishe mkutano wa wagane wachamungu ambapo mmojawapo atateuliwa na Mungu kwa ishara kwa kuwa bado Mungu ana kusudi maalum na Maria.

Basi, ndipo katika kusanyiko la wanaume hao wagane, alikuwemo mzee wa miaka takribani 80 aitwaye Joseph. Fundi seremala mchamungu haswa, ambaye mkewe Salome alifariki mwaka mmoja uliopita na alijaaliwa naye watoto 7.

Kufupisha story, mzee huyo alifanikiwa kuteuliwa kwa ishara ya mng'ao wa kitambaa. Naye binti Maria (13) hakuwa na pingamizi kwenye uamuzi wa Muumba. Akakubali kuolewa.

Na historia maarufu ya Bikra Maria sasa inaanzia hapo na kuendelea. Kuna haja ya kuisimulia zaidi?!
Hivi anakuwaje bikra maria na wakati umeshasema aliolewa na joseph ??

Au mimi ndio sijakuelewa??
 
Nabii Zakaria na kanisa wapi na wapi

Zakariya alikuwa Kuhani Mkuu wa Hekalu katika kipindi chake. Kipindi hicho halikuwa linaitwa Kanisa bali Hekalu ambalo ni Jumba la Ibada sawa tu na useme Kanisa kwa sasa. Na ndiye mlezi wa Bikra Maria..
 
Hivi anakuwaje bikra maria na wakati umeshasema aliolewa na joseph ??

Au mimi ndio sijakuelewa??
Joseph hakumuingilia. Roho Mtakatifu alitangulia akavuruga mipango. Ndio maana kuna wengine wanagoma kuiita ndoa bali uchumba tu.
 
Ila mie siwezi mbishia mleta mada kuna wengine wanae yesu mwingine labda ndiye
anamsimulia sio huyu Yesu Kristo aliye sulubiwa msalabani
Sawa tu. Masuala ya imani hayataki kulazimishana. Na nilishasema sio lengo langu kujadili imani.
 
Mtoto wa wa Zakaria na Elizabeth ni Yohana mbatizaji aliyekatwa kichwa na mfalme kabla hatavya Yesu kusurubiwa
Naam. Na ndiye niliyemtaja hapo awali. Aliyeenda kuishi msituni akila asali na nzige baada ya wazee wake kufariki dunia ili kujitenga na maovu ya walimwengu..
 
Duh
Kwahiyo Yusuph (Joseph) aliye mposa Maria alikuwa ni mzee mwenye watoto 7? Kisha akataka kumuacha kwa siri ili asimtie aibu baada ya kugundua kuwa Maria ni mja"mwepesi"?
Aloo, Tunaomba na kitabu cha rejea (reference book) ya hii maandiko yako
Hii itakuwa ni Injili mpya sana kwangu
Hapo ndipo kanisa katoliki linawaacha na kubakia kanisa lenye weledi na hazina kubwa sana duniani.

Wengine vyanzo vya habari za Mungu ni biblia tu.
 
Hapo ndipo kanisa katoliki linawaacha na kubakia kanisa lenye weledi na hazina kubwa sana duniani.

Wengine vyanzo vya habari za Mungu ni biblia tu.
Biblia pekee haitoshi. Yameandikwa yale machache muhimu tu, very selective.

Na sidhani kama Bible inakataza kutumia taarifa kutoka vyanzo vingine kwa maana itakuwa ajabu kwamba yote yatoshe mule. Haiwezekani!
 
Hivi anakuwaje bikra maria na wakati umeshasema aliolewa na joseph ??

Au mimi ndio sijakuelewa??
Na utaendeleaje kuwa bikira angali umeshazaa hata kama aliyekupa mimba ni njiwa ukweli utabaki kwamba tupu yako imefunguka kwa hiyo swala LA ubikira ni ngonjera na mbembwe za kiimani.
 
Na utaendeleaje kuwa bikira angali umeshazaa hata kama aliyekupa mimba ni njiwa ukweli utabaki kwamba tupu yako imefunguka kwa hiyo swala LA ubikira ni ngonjera na mbembwe za kiimani.
Bikra ya kutoingiliwa na bikra utepe. Maria alibakiza Bikra ya kutoingiliwa, utepe ulikatika punde tu alipomzaa Jesus. Simple logic.
 
Bikra ya kutoingiliwa na bikra utepe. Maria alibakiza Bikra ya kutoingiliwa, utepe ulikatika punde tu alipomzaa Jesus. Simple logic.
Sio kweli! Maria alikuwa mke halali wa Mzee Joseph. Kugundulika kwa mimba changa ya Yesu hakukuzuia mahusiano ya kindoa baina ya Maria na Joseph. ..Jiongeze!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom