Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

EPISODE 26

“A TRUE STORY BY INSIDER”

Jumatatu ya Pasaka asubuhi nilifanya mawasiliano na yule constructor wa Mzee na nikamwambia baada ya lisaa nitakuwa Mbweni na yeye alisema yuko njiani ndo anaelekea.

Kwa upande mwingine yale materials ya kununua nilimtumia picha Mzee Mollel na alinisaidia kunitajia bei na kunipa connection kwa sehem yanakopatikana, alinitumia namba za baadhi ya masupplier akanambia nikiwapigia simu niwaambie yeye ndo amenikonekti.

Baada ya kufika Mbweni nilikuta kazi zikiendelea na mimi niliwasalimia Mafundi na Jamaa alikuwa amefika tayari.

Sababu alikuwa anajua kinachoendelea pamoja na ujio wangu, hata hakuwa na maswali zaidi alisema nimpe pesa akanunue materials.

“Kwenye kununua materials tutakwenda wote mkuu usiwe na wasiwasi.”

Na muda huu nilifanya kuwasiliana na baadhi ya supplier na tukapata mmoja pale Africana ndo alikuwa na bei nzuri.

Tulikwenda wote na Jamaa mpaka Africana kuna duka kubwa sana pale lipo mataa ya Africana, mkono wa kushoto kama unakwenda Juliana.

Tulifanya manunuzi ya materials mbalimbali na tukarudi Mbweni, vifaa vyote nilisimamimia manunuzi. Jamaa kama alimind hivi kwanza, pia hakuwa akiamini kuona nayajua maduka vile, kumbe nyuma ya Pazia alikuwepo mzee Mollel anayenipa CODE.

Sababu hii siku nilikuwa na miadi na Mama wa2, nilimwaga jamaa na nikaondoka. Nilitoka pale Mbweni kuelekea Mbezi Beach na muda huo ilikuwa saa 6 kasoro za mchana.

Hii siku tulikuwa tunakwenda kumpokea mdogo wake Airport na kuhusu kwenda kuangalia nyumba yake alisema tutakwenda siku nyingine.

Mama wa2 alitumia dakika 30 kutoka ndani na tukaelekea Airport.

“Insider Unaendeleaje.”

“Safi tu, mgeni ataingia sangapi?”

“Saa 8 atakuwa amefika tayari.”

Tuliwasili pale JNIA na tulikwenda moja kwa moja mpaka Terminal 2 ndo tukapark gari. Tuliamua kwenda kukaa kwenye kimgahawa tukimsubiri mgeni.

“Insider leo jioni nataka twende Masaki na wanangu tukatembee.”

“Sawa haina shida mimi nipo free leo.”

“Nilipata taarifa Uber wanasitisha huduma zao vipi kwako utafanyaje?.”

“Kwa wateja wa Card na kampuni bado wanaendelea ila wanaotumia card ni wachache sana, wateja wa cash ndo wengi kwa bongo hapa. Sio mbaya sana lakini maana Bolt bado wapo japo imeniathiri sana.”

“Pole sana ndo changamoto hizo naamini watarudi soon.”

“Ni mambo yanayohusisha serikali acha tuone itakuwaje.”

Suala la Uber kusitisha huduma zao kwa upande wa magari ni kutokana na LATRA kuwataka kupunguza kamisheni zao kutoka 25% mpaka 15%. Madereva wa Tax mtandao wolilamika kwa mamlaka husika kuwa hizi kampuni zinatoza kamisheni kubwa sana. Uber hawakuwa tayari kupunguza kamisheni zao kwani walisema wanatozwa kodi na tozo kibao hivyo wangeendesha biashara kwa hasara.

Tuliendelea kukaa pale na Mama wa2 huku story zikiendelea maana ndege ilichelewa kutoka KIA kwa taarifa ambazo Mama wa2 alizipata.

Saa 9 kasoro ndege iliwasili na na baada ya dakika 15 mamdogo alitoka na wakakumbatiana na dada yake pale. Walionekana kumisiana sana.

Nilimsaidia kubeba bag lake na tulikwenda parking tulikokuwa tumepark gari na tukaanza safari ya kurudi Mbezi Beach.

MAMA WA2: “Insider huyu ndo mdogo wangu wa mwisho anaitwa Joana.

MIMI: “Nimeona pia mmefanana sana, Joana karibu sana Dar es Salaam.”

“Ahsante.”

MAMA WA2: “Huyu anaitwa Insider ni mtu wangu wa karibu sana.”

MIMI: “Mama mkwe hujawai kunambia kuwa una mdogo mzuri hivi.”

Na wote waliishia kucheka muda huu na walikuwa wamekaa siti za nyuma.

Njiani walikiwa busy sana wakiongea mambo yao na tulitumia kama dk40 kufika nyumbani maana hakukuwa na foleni kabisa.

Tuliingia ndani muda ule na mimi nikatoa bag la mgeni nikaingiza ndani.

Baada ya kuingia ndani mamdogo alisalimiana na kina Rachel na Pili na mimi muda huu nilikuwa nawaza msosi maana njaa ilikuwa inanigonga balaa, toka asubuhi nilikuwa sijaingiza chochote tumboni.

Mama wa2 alitukaribisha dining kwaajili ya lunch na mimi ndo nilikuwa wakwanza kufika pale. Nilikuwa nimeshapazoea kwa Mama wa2 ilikuwa kama niko nyumbani tu.

Na wakati tuko dining Mama wa2 aliwaambia bint zake wajiandae kwaajili ya kutoka out. Mama wa2 alikuwa busy sana na mdogo wake hii siku hata nilipomaliza kula nilimshukuru kwa chakula na mimi nikaenda kukaa seblen.

Joana pia alikwenda kujiandaa na wakati huo bint zake walikuwa wako tayari wamejiandaa.

MAMA WA2: “Insider tunakwenda wapi eti?”

PILI: “Mama twende Slip way.”

MIMI: “Kama watoto wanataka kwenda huko tuwapeleke haina shida.”

MAMA WA2: “Bhasi tutakwenda huko.”

Na muda huu akina Pili na Rachel walionekana kufurahia sana kwenda huko.

Baada ya dakika 20 mamdogo alikuwa naye kajiandaa na ametoka hao tukaanza safari na muda huo ilikuwa saa 11 jioni.

Tulitumia dakika 25 kufika eneo lile na hii siku palionekana kuwa busy sana na tulikwenda upande wa chini wa Restaurant.

Tulitafuta sehemu nzuri ya kutosha watu sita na tukakaa, kwenye hii meza mimi pekee ndo nilikuwa mwanaume pale na hii ilikuwa ikinipa ufahari flani hivi.

Kila mtu aliagiza anachotaka kwa upande wangu sikutaka kuagiza chakula maana nilikuwa nimeshiba, niliagiza heineken 3 tu maana sikutaka kulewa hii siku. Kwa upande mwingine mama wawili aliagiza bucket ya Savanna kwaajili yake na mdogo wake.

Story zilikuwa zimetawala meza yetu tukicheka na mimi nilikuwa nimekaa karibu na Pili nampigisha story sana,

Sasa wakati dada analeta vinywaji Pili alishangaa sana kuona dada kaniwekea heineken pale mezani.

PILI: “Uncle Insider na wewe unakunywa kumbe?”

MIMI: “Nakunywa kwaajili yako hapa.”

PILI: “Toka hapa! mimi situmii pombe”

MIMI: “Wewe ni mchaga soon utaanza kutumia, muulize mama yako alianzaje kutumia. Unataka sikuonjeshe kidogo?”

PILI: “Aku sitaki mimi. Kwanza Baba yangu sio Mchagga”

Pili alikuwa kashanizoea kwa muda mfupi hata Mama wa2 alishangaa sana kuona Pili kanizoea haraka vile.

Mida ya saa moja usiku wakati tukiendelea kunywa na kupiga story, Prisca alinipigia simu, nikaamua kutoka eneo lile ili nikaongee naye mbali na pale.

PRISCA: “Hello baby how you doing?”

MIMI: “Niko poa za toka jana.”

PRISCA: “Safi tu, nimekumiss”

MIMI: “Jana ulinambia mnatoka as family nipe ripoti.”

PRISCA: “Insider ungekuwa unanijali ungekuwa ulinipigia simu na ukajua kinachoendelea.”

MIMI: “Aisee, nijue kinachoendelea kwenye mambo ya familia yenu?, naona kama unanikosea.”

PRISCA: “Sasa unataka ripoti ya nini?”

MIMI: “Ripoti niliyotaka mimi nijue ulirudi sangapi, Jana sikutaka kukutafuta maana nilijua utakuwa busy na Familia.”

PRISCA: “Okay we had funny yesterday, inshort we enjoyed.”

MIMI: “Nice na uko wapi kwa sasa?”

PRISCA: “Niko home nimelala on bed. Nimekumiss nataka nikuone.”

MIMI: “Acha uongo unanimisije na upo period?”

PRISCA: “Insider unataka kumaanisha kwasababu niko period siwezi onana na wewe? You only want sex from me that's all you care about.”

MIMI: “Prisca mimi naona hayo ni mawazo yako, ila naomba utambue kitu kimoja. Usifikiri mimi kama napenda sana kumchepuka Mama Junior na ninampenda sana. Unapaswa kunipa vile navyokosa kwa Mama Junior na sio kulalamika, kumbuka ulichagua mwenyewe na hukulazimishwa na kama unaona nakuumiza unaweza kuniacha na maisha yangu.”

PRISCA: “Leo ndo nimeprove upo na mimi kwasababu ya shida zako na huna hata tone la upendo kwangu, Ahsante nashukuru.” Akakata na simu.

Mimi sikutaka kumpigia tena simu niliamua kumpotezea na nikasema hasira zake zitakuwa sababu ya Period.

Wakati nimerudi pale mezani Mama wa2 aliniangalia afu akatabasamu

“Insider naona ulikuwa kujenga matofali”

Na mimi niliishia kucheka tu muda huu.

Tulikaa mpaka saa4 usiku ndo tukatoka pale na muda huu Mama J alikuwa akisumbua sana kwa kupiga simu.

Baada ya kuwashusha akina Mama wa2 alinipa malipo yangu na mimi nikaelekea nyumbani.

Nilimkuta wife yuko seblen anaangalia movie na mimi niliwasalimia na nikaunganisha bafuni kuoga.

Wakati nimetoka bafuni nilimkuta wife yuko kitandani amejilaza kizembe.

MIMI: “Nambie swahiba toka jana hatujaongea kabisa, hujanambia sikukuu ilikwendaje.”

WIFE: “Ilikuwa poa tu, Mama anakusalimia pia amesema uache tabia mbaya. Kwanini hupendi kujumuika na sisi?”

MIMI: “Usijali mwambie nitakwenda msalimia, na vipi kuhusu Mzee ulifanikiwa kuongea naye?”

WIFE: “Ndio alisema mwisho wa mwezi huu atanipa hizo hela.”

MIMI: “Wow nice umetisha sana swahiba, nafanya haya mambo kwaajili yako na hii bajaji tutatumia jina lako.”

WIFE: “Sawa haina shida, twende ukale maana leo nimekupikia vitamu.”

MIMI: “Sawa tangulia nakuja.”

Muda huu nilikaa kitandani maana nilikuwa nafuraha sana kuona jambo limefanikiwa tayari.

**********

Hii week baada ya Pasaka nilikuwa nashinda tu kule kwa Mzee Pama Mbweni. Asubuhi nikishawapeleka wateja wangu Posta naunganisha moja kwa moja mpaka Mbweni. Sikutakaa kaa mbali kabisa na eneo la tukio nilitaka kusimamia kila hatua kwenye ile nyumba.

Kazi ilikuwa inakimbia balaa na kwa upande mwingine mtu wa bustani alikuwa amekuja tukakubaliana bei na nikamwambia miti na maua tutakwenda nunua wote.

Mpaka kufikia jumapili nyumba ilikuwa imekamilika kila kitu kwa ndani na ilibaki vitu vidogo nje vya kumalizia kama kuweka tank na kumalizia pavings. Jumatatu ndo tulimalizia kila kitu na nikatafuta mtu wa kufanya usafi mle ndani, nje na kutengeneza barabara inayokwenda kwenye ile nyumba maana ilikuwa mbovu sana.

Kufikia jumatatu kila kitu kilikuwa kimekamilika vilibaki vitu vichache sana ambavyo sio vya lazima, lakini nyumba ilikuwa tayari kwaajili ya kuhamia.

Katika zile Pesa ambazo alinikabidhi mzee nilibakiwa na kama 3,200,000/= na hapo ndo nikajua jamaa alimpiga mzee japo pia nilipata discount kwenye mizigo ila kulikuwa na balance kubwa sana.

Niliitamani sana hii pesa lakini niliogopa jamaa anaweza kunisnitch kwa Mzee akampa hesabu za vitu na gharama zote afu nikapoteza trust kwa Mzee. Palepale nikachomoa million moja nikasema hii nitaitolea maelezo kwa Mzee ila hii amount inayobaki nitamrudishia.

***********

Kwa upande mwingine Jumapili ndo siku ambayo Pili alikuwa ana rudi shule hivyo Mama wa2 aliomba kampani yangu.

Nilitoka Mbweni kuelekea Mbezi Beach kwa Mama wa2 na saa 7 mchana nilikuwa pale.

Saa 8 mchana ndo tulitoka kuelekea Bagamoyo shuleni. Tulitumia saa moja na nusu kufika Bagamoyo shuleni na Mama wa2 alikwenda kumkabidhi.

Na hii siku walionekana Wazazi wengi wakiwarudisha watoto wao shule.

Baada ya kumuandikisha kuna sehemu tulikaa tukiwa tunaongea na mimi nilimshauri sana Pili asome kwa bidii na akae mbali na wanaume. Ilibidi nimchane ukweli ajitunze Mafisi “wazee wa kula kimasihara” sio watu wazuri Kabisa awe makini.

Pili alionekana kuwa makini sana akisikiliza ushauri wangu na nilitoa laki moja nikampa itamsaidia kama pocket money.

Niliona aibu kumwacha bila kitu afu mama yake alikuwa kanisaidia mkopo wa Pesa nyingi, niliamua kurudisha shukrani kwa njia hiyo.

Pili alishukuru na alifurahi sana, akasema next time nikamchukue na Mama yake pia alimpa Matron namba yangu incase kama kuna lolote wanaweza kunipigia na mimi. Na mama wa2 alininiandikisha mimi kama Uncle wa Pili.

Tuliondoka pale shuleni na kuanza safari ya kurudi Dar na njiani tulikuwa tukiongea mambo mengi sana na Mama wa2.

MAMA WA2: “Insider mwanangu Pili amekuzoea haraka sana, the way ambavyo unaongea naye nilikuwa najiskia faraja sana. Baba yake hajawai hata siku moja kumpa ushauri binti yake nashukuru sana kwa leo.”

MIMI: “Pili ni kama mdogo wangu lazima nihakikishe anafikia malengo yake na kama unajambo lolote usisite kunambia.”

MAMA WA2: “Next time utamfata wakifunga shule.”

Tulitumia lisaa kufika Mbezi Beach nikamwacha kwake na mimi nikarudi zangu home mapema sana.

Usiku mzee alinicheki akanambia kesho nikamchukue Airport ndo anarudi na anatarijia kuingia saa 7 mchana na alinisisitiza sana kuwa ontime, maana tungeenda na kukagua nyumba kule Mbweni.

Asubuhi nilimka mapema na nikafanya usafi wa gari mwenyewe na baada ya kumaliza nilirudi ndani ili nipate kifungua kinywa.

*********

Tarehe 26 ndo siku ambayo mzee alirudi kutoka safari na ilikuwa ni siku ya Muungano. Na mimi mapema sana nilikuwa pale Terminal 3 nikimsubiri.

Nilimcheki dada Tyna akanambia yuko busy atanichek mida kidogo, na muda huu nilikuwa nikipiga story na yule jamaa yangu mlinzi.

Saa 8 kasoro ndo muda ambao mzee Pama aliwasili pale JNIA na nilimpokea na baada ya dakika chache tuliondoka maeneo yale.

Safari yetu ilikuwa ni kwenda moja kwa moja mpaka Mbweni ili afanye ukaguzi wa nyumba. Na tulitumia saa moja na nusu kufika pale

Mzee alifanya ukaguzi wa nyumba na aliridhika kuona jinsi ujenzi ulivyokuwa umekamilika vizuri tena kwa viwango vya hali ya juu. Pia alishangaa kuona nimetengeneza ile Barabara na imekaa vizuri, alishangaa kuona nimetengeneza bustani mpaka nje ya geti na palikuwa pamejengwa vizuri. Mzee pia alinisifu kwa kufanya usafi wa nyumba nje na ndani.

Mzee alimjengea mchepuko wake mjengo mkali sana tena wa kisasa, nyumba ilikuwa kubwa ya vyumba vinne.

MIMI: “Mzee naona unataka kuwa na Familia kubwa vyumba ni vingi sana.”

MZEE: “Nataka anizalie watoto wa3 hata pale tayari ni mjamzito.”

MIMI: “Hongera sana Mzee ni jambo la neema hilo.”

MZEE: “Kabisa, Kijana niseme Ahsante kwa kazi nzuri uliyofanya umenifurahisha sana, materials ni zenyewe hakuna ulichokosea.”

MIMI: “Mzee nilikuwa namsimamia Fundi mwanzo mwisho nilikuwa nakuja asubuhi nashinda na Mafundi jioni narudi nyumbani. Ndomana unaona kila kitu kimeenda vizuri na kwa wakati sahihi.”

MZEE: “Hii nyumba nimejenga kwa siri sana hakuna anayejua kabisa hili suala.”

MIMI: “Sasa suala la watoto vipi hutaki wajuane?”

MZEE: “Hao hakuna shida watajuana tu ila sitaki ifahamike kama mke mdogo anakaa huku italeta shida.”

MIMI: “Sawa mzee hapo nimekuelewa”

Mzee Pama alikuwa ni mzee wa umri wa miaka 60-65 alikuwa anacheza humu ila alikuwa ni dizaini ya wale wazee wajanja au wahuni.

Tulitoka pale Mbweni saa 11 jioni na Mzee alinambia nimpeleke kwake Ununio.

Wakati tumeingia kwenye gari nilifungua drow na nikatoa invoices za manunuzi na nikamkabidhi, na alianza kuzitizama muda ule.

MIMI: “Mzee na hii Pesa ndo ilibakia kwenye manunuzi.”

MZEE: “Kijana kama pesa imebaki ni yako, umefanya kazi kubwa sana. Bila kumsimamia Fundi vizuri angenipiga yule mshenzi.”

Nilimshukuru Mzee na nikawasha gari ili tuondoke eneo lile. Nilimpeleka Mzee kwake ununio na akaniahidi kunitafuta kwani kuna vitu vya kununua vingi anataka nimsaidie kusimamia.

Muda huu nilijikuta nam-miss sana Iryn kwakweli, kwani ndo ilikuwaga mida ya kwenda kwa Iryn kumchukua. Licha ya yote Iryn alikuwa ni moja ya watu wangu wa karibu sana na ilitokea kuelewana sana.

Tulikuwa tunakwenda karibu mwezi bila mawasiliano yoyote na nilikuwa sijui maendeleo yake, kipindi hiki.

Kwasababu mwisho wa mwezi ulikuwa umekaribia nikawaza muda ule niende kwake Kijitonyama. Na lengo langu ilikuwa nijishushe nimwombe msamaha kama kuna sehemu nilimkwaza.

Niliona sometimes ni bora kuwa mjinga ili mambo yako yaende ila kwa upande mwingine niliwaza hivi nikijishusha sana si ataniona mimi bwege? Yaani bila yeye maisha yangu hayaendi? Niliwaza pale ataweza kunisumbua sana huko mbeleni. Pia nilikuwa nawaza ni jambo gani ambalo limemkera mpaka kuchukua maamuzi yale?. Iryn ni mwanamke ambaye ni hatabiriki “UNPREDICTABLE”.

Saa 12 jion nilikuwa pale kwa Iryn Kijitonyama na hata sikumpigia simu niliamua kwenda bila kutoa taarifa, nilitaka iwe saprize.

Nilipark gari nje ya geti na nikafungua geti maana nilikuwa tayari mwenyeji kwenye zile apartments. Niligonga mlango wake na baada ya dakika kadhaa alitoka kufungua.

IRYN: “Ooh Insider karibu na nilikuwa nawaza nikupigie simu toka jana ili uje tumalizane maana namzigo wako.”

MIMI: “Ooh sawa ila mimi sijaja kwaajili ya hilo, nimekuja kukuona na kukujulia hali maana ni muda kidogo toka unitumie ile text ya kuterminate mkataba, pia nilitaka kujua sababu ni nini mpaka ukaamua vile.”

IRYN: “Insider hakuna sababu yoyote na hakuna jambo lolote baya ambalo umefanya, ila nataka kufocus na masuala ya mama kwa sasa.”

MIMI: “Kama hakuna jambo nililokukosea ungenipigia simu na tungekaa chini tukaongea. Iryn mimi ni binadamu sijakamilika kwa asilimia mia, kama kuna sehemu nilikukosea nisamehe. Iryn naomba utambue mimi ni Mwanaume ambaye nakuheshimu sana na bado utaendelea kuwa mtu muhimu sana kwenye moyo wangu.”

IRYN: “Insider hakuna shida mimi naona wewe ndo una wasiwasi.”

MIMI: “Hapana mimi nimekuja kukuomba msamaha pale ambapo sikuwa sawa na nimekukosea. Sijaja hapa kuomba unirudishe kazini, masuala ya kazi ni yako na ni maamuzi yako wewe.”

Na muda huu Iryn hakuongea kitu bali alifunga laptop yake na kuingia chumbani na mimi nilikaa pembeni ya coach. Na baada ya dakika 3 Iryn alitoka akiwa ameshika bahasha ndogo ya kaki

IRYN: “Insider pesa zako hizi nimeweka na fine ya kuvunja mkataba na wewe.”

Na muda huu alinikabidhi ile bahasha na mimi nikasimama nikaipokea ile bahasha pale na nikaiweka mfuko wa nyuma.

MIMI: “Ahsante but nishaelewa tatizo ni nini.”

IRYN: “What do you mean?”

Na muda uleule nikamshika mikono yake miwili na nikapandisha mikono yangu kuzunguka kiuno chake na nikamvuta upande wangu kwa nguvu, kilikuwa kitendo cha ghafla sana. Nikampa ulimi wangu na yeye akanipa wake haraka bila kizuizi na tulichezeshana pale kwa sekunde kadhaa na palepale tulishtuka tukaacha ule mchezo.

MIMI: “I mean hiki ndo ulichokuwa unakitaka, Iryn thank you for everything, I have missed you so much. Mimi naondoka nikutakie maisha mema ila kama utahitaji msaada wangu never hesitate to call me. Byee.!

Nilimwacha pale Iryn katika sintofahamu kwani hakuweza kuongea neno lolote muda ule na alikuwa akiniona nikipotea machoni mwake live.

Na wakati niko kwa gari nilikuwa mtu mwenye furaha sana na kama nilikuwa nimepata Nguvu mpya na nikajisemea pale “When one door closes another opens.”

TO BE CONTINUED
Duh aseee utamu kunoga kesho tunayo
 
Na muda uleule nikamshika mikono yake miwili na nikapandisha mikono yangu kuzunguka kiuno chake na nikamvuta upande wangu kwa nguvu, kilikuwa kitendo cha ghafla sana. Nikampa ulimi wangu na yeye akanipa wake haraka bila kizuizi na tulichezeshana pale kwa sekunde kadhaa na palepale tulishtuka tukaacha ule mchezo.
Huwezi amin hichi kipande mafisi tumekielewa kinyama, ilibaki kudumbukiza mtwangio Kwa kinu alafu unasepa na 💯 dadeki
Mafisi oyeeere!!
 
Kuishi kama inside inahitaji mtu jinsi alivoumbwa na haya yake usoni , kiufupi ni kipaji ndio amejaaliwa ni wengi humu wanaume hatuwezi , kiufupi jamaa ni mtu wa kujichanganya ,kwa lugha lahisi ni mtu wa shobo sana ,kwa mfano mimi siwezi ingia jikoni nikaanza kupika hata kama awe mpenzi wg ,au kisa ni mteja wg nikaanza kukaanga mayai ni ngumu kabisa , yaani na ndevu zg kabisa nikaanza kujipikilisha , kwa hio shobo zinamsaidia jamaa , ni wengi humu hatuwezi
 
Toka mwanzo Hadi ulipofikia nimeona Kuna kitu, Kua kuchepuka wakati mwingine hakuzuiliki kabisa kutokana na mazingira na uhalisia kama ilivyokua kwako

Lakini nawaza je wanawake nao wakikutana na mazingira kama haya wakaliwa, wanaweza kusameheka kweli?
Tukijua hawasameheki
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom