Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

EPISODE 03

Baada ya siku 3 akanicheki ghost akanambia account yako ipo tayari, akanipa password akanambia download bolt driver app kwa istore then anza kazi. Kweli nikafanya nikaona mambo yako supa nikaona sehem ya kwenda online kama unataka request, nika touch pale nikaona inasearch nikazima data nikalala, nikaplan kuingia mzigoni jioni.

Inaendelea

“Unajua biashara ya Uber ni nzuri sana kwa kijana ambaye anataka kujiajiri, inalipa sana kama utakua makini. Niko kwenye hii biashara toka 2017 nina uzoefu wa kutosha sana, nimepitia mishale mingi sana. Mdogo wangu nakuomba sana zingatia haya, 1. Focus na malengo yako, 2. Acha tamaa, 3. Fanya kazi kwa bidii chukulia kama ni kazi nyingine. Acha tamaa na wanawake, utakutana na mademu wengi sana kuna ambao watataka uwale sababu hana nauli, kuna wamama watu wazima “mashangazi” watakutaka nakuona so HB mdogo wangu wamama wengi watavutiwa sana wewe. Kuwa mkarimu kwa wateja, Ipende ofisi yako “gari yako” hakikisha unafanya usafi muda wote liko safi, kuwa makini sana wakati wa usiku sio kila sehemu ya kwenda. Utakutana na watu wa kila aina chamsingi wewe kuwa humble usipende kugombana na wateja kabisa. Ukizingatia haya utafika mbali na pia gari yako utaiona pesa trust me. “Hayo yalikua maneno ya Dullah akinipa changamoto za biashara hii ya Tax mtandao.”

Niliamka saa 11 jioni nikaingia bafuni nikajiandaa chap nikaweka mazingira mazuri ya gari. Nilianza hii kazi ya Uber mwishoni October 2021, bhasi nikapitia filling station nikajaza mafuta full tank huyo nikaenda kupark gari pale mbezi Beach kwa zena. Hapo nilikua nimeswitch online so dizaini kama App ilikua inasearch requests.

Nimekaa kama nusu saa hollaaa hakuna hata request nikaanza pata wasiwasi au sababu mimi mpya??. Nikampigia simu Dullah kumwambia sipati request, Dullah akanambia vumilia tu zitaita usiwe na wasiwasi.

Baada ya dk 10 hivi nikaskia kitu kinaita “nke nke nkee nkeeke nkeee” uyo chap ni accept, ukweli nilikua bado na kaushamba wa kutumia hii App lakini Dullah alinielekeza namna ya kutumia map na vitu vingine muhimu akanambia vingine utamasta taratibu.

Baada ya kuaccept mteja akapiga simu akanambia fata ramani, nikamjibu sawa, (“kwa mara ya kwanza App lazima itakuchanganya”). Nikaanza kwenda uelekeo wa kawe akapiga simu nakuona unapotea “Oasisi” unakujua?… nikamjibu ndio, mteja akanambia sasa huko unakwenda wapi??. Oasisi nilikua najua kabla hujafika round about ya kwenda whitesand kuna kibarabara cha lami kinakunja kushoto, chap nikageuka nikafika mpaka kwa mteja nikamchukua alikua anakwenda mbweni.

Baada ya kumshusha mteja Mbweni sikukaa sana nikapata request nyingine nika accept mteja alikua anakwenda mbezi beach- shamo tower. Nilipiga kazi mpaka saa 6 usiku nikaingiza 59,000, nikapitia sheli nikajazia mafuta tena yaliyotumika nikabaki na 39,000, nikaona pesa nzuri kwa muda wa masaa 6 tu niliyofanya ikanipa morare sana.

Asubuhi nikaamka 06:00 am nikaanza kazi kama kawaida siku hiyo nilipiga kazi mpaka muda wangu wa kudrive ukaisha. So nilirud home kama 23:00 pm, pesa nilizoingiza sio haba kwenye App ubao ulikua unasoma 153,000/= bado zile pesa nilizokua naingiza nje na App. Ukitoa gharama za wese na cost nyingine faida yangu ilikua kama 80,000 hivi.( “Uber/Bolt kuna driving limit, hutakiwi kudrive zaidi ya masaa 12 kwa siku, ukidrive masaa 12 wanakufungia App ukapumzike kwa masaa 6 then urudi mzigoni tena, kwa mtu anayetafuta pesa hii ni changamoto sana, hapo ndo utaona umuhimu wa kuwa na App zote mbili Uber/Bolt”)

Niseme ukweli kwa muda mfupi ndani ya week nilitengeneza pesa ndefu sana. Mpaka nikaona hakuna haja ya kuajiriwa kama Bolt tu inaniingizia pesa hivi kuna haja gani ya kutafuta kazi??.

Baada ya week 2 kukata “ghost”akanicheki akanambia account yangu ya Uber ipo tayari. Nikaanza kuitumia Uber aisee huku ndo nilianza kupata deals nyingi sana na pesa upande wa nauli zilikua juu tofauti na bolt, huku nikaanza pata connections nyingi na kukutana na foreigners.

*******
Nataka kidogo niwape utofauti wa Uber na Bolt. Uber wako vizuri sana upande wa fares na usalama, kwanza wanaotumia Uber wengi ni foreigners pia ni watu wenye pesa au matajiri. Abiria wa uber akirequest wanajua kwenda na muda itoshe kusema abiria wa Uber ni smart sana. Ukija kwa ndugu zetu wa Bolt abiria wao ni pasua kichwa sana, wateja wa bolt wengi ni wanachuo, wale low income earners ndo unawakuta huku sasa. Abiria wa Bolt ni wanamaneno balaa, ana request usafir anakuweka hata nusu sometimes mpaka one hour afu akija anakupa majibi rahisi nilijua upo mbali. Nauli ikiongezeka kidgo atalalamika balaa, madereva wa Tax mtandao wanakwambia bolt ni kwa maskini na Uber ni kwa matajiri. Pia raha ya Uber hata kama mteja atakuweka baada ya dk 5 inaanza kucharge waiting fee, tofauti na Bolt.

Baada ya kuanza kutumia Uber nikaona nitaendana sana na wateja wa Uber kuliko Bolt hata kimaslahi yapo Uber nikaamua kuachana na Bolt, japo nilikua naitumia kwa nadra sana na baadhi ya mazingira.

“Kuna uhusiano mkubwa sana kati ya uber na wateja wake kama nilivyosema huko juu. “

Nilivyoanza kutumia Uber nilianza kupata sana hela sio hivyo tu bali niliweza kupata dili nyingi sana. Niliweza kukutana na foreigners wengi sana wa nchi mbalimbali pamoja na matajiri, viongozi wakubwa wa serikali, na celebrities mbalimbali. Niliweza kujuana na watu wengi sana mpaka leo kuna foreigners nachat nao sana hata wakija bongo lazima wanicheki.

Siwezi kusimulia matukio yote maana ni mengi kwakweli nitagusia baadhi. Muda wangu wa kazi ulikua naamka 06:00 am mpaka usiku, kama biashara siku iyo mbaya bhasi mapema niko home kucheza na Junior. Siku za weekend nilikua nakesha siku zingine narudi late night. Nilikua nazingatia sana usafi wa gari, usafi wangu binafsi, yaani siku za kazi nilikua nachomekea kama officer nakwenda kazini kumbe ni Uber tu, hii kitu ilepelekea kupendwa sana na watu na wateja wangu wengi walikua wanawake.

*******

Nikiwa barabarani kama kawaida nilikua Posta nimepaki gari yangu pale, mida ya saa10 jion nikapata request ya kwenda Airport. Nikampeleka yule mteja alikua ni dada, akanambia ameipenda gari yangu atakua ananicheki, baada ya kumdrop pale tukabadilishana namba.

Nilikua pale Terminal 2 nimechili nasubiri request ilikua nishakaa almost dk 45, nikakumbuka Dullah alinambia kwakua unatumia vibao vya njano make sure uko makini sana maana pale Airpot wakijua wewe ni Uber then gari yako haina vibao vyeupe watakupiga fine, hata wale madereva wa tax mle Airpot ni wanaa sana.

Mnajua kwanini madereva wa Tax mle Airpot hawawapendi Uber? Ujio wa Tax mtandao umewaharibia sana biashara afu Tax nyingi mle ndani ni za wafanyakazi wa mle ndani. Mfano kutumia tax ya Airport mpaka Masaki utalipia 50,000-70,000 wakati kwa Uber haizidi 25,000, hapo utaona kama Tax mtandao ikawa msaada sana.

Baada ya 1 hr hivi nikapata request mteja alikua anakwenda Sea cliff hotel, chap aka nitext kupitia App “Are you coming”, nikamjibu ASAP. Yaani “As soon as possible”

Ofcourse nilikua mgeni na Airpot na kwa mara ya kwanza lazima uchanganye kama sio mzoefu wa zile barabara za mle ndani, na pia hakuna barabara ya kutoka Terminal 2 kwenda Terminal 3 ya shortcut “sio kwamba shortcut haipo ila wameiziba tu makusudi”, so pale unavyotoka lazima ulipie then uwe kama unatoka ndo uzunguke ile round about kama unatoka ndo uelekee Terminal 3.

Kama ulikua Terminal 2 unataka kwenda terminal 3 lazima ulipie 2,000 utoke pale terminal 2 then kuingia terminal 3 lazima uchukue card inamaana lazima ulipie tena utakavyotoka terminal 3 (lazima ulipie mara 2). “Hapo jamaa alikua ananielekeza pale terminal 2 maana nilikua sijui na ukichanganya hata barabara tu unalimwa fine, nilisikiliza maelezo vizurii sana nikamasta.”

Message ikaingia kwenye App “I am near the Arrival door” huyu alikuwa mteja.

Nikahisi huyu atakua foreigner tu, nikafika pale wakati nasogea akawa kashasogea barabarani akanipa ishara, nikampakia hao tukasepa. “Wazungu wako chap sana huwa hawapotezi muda kabisa, akirequest labda wewe uzingue, ila wabongo wanaringa sana”. Safari yetu ilikua ni kuelekea Sea cliff hotel kule Masaki, bhasi tukiwa njiani tukaanza story…..

MZUNGU: Bro your Car is very clean

MIMI: Thanks bro! It’s my office, how was the journey??

MZUNGU: Wow was amazing bro and I’m very happy being here in Tanzania .

MIMI: So it’s your first time being here?

MZUNGU: , no bro!, it’s my second time.

MIMI: Welcome bro! so your nationality?

MZUNGU: I’m Swiss bro!

MIMI: Wow nice bro! So What do you do for a living?.

MZUNGU: I am working for WORLD VISION.

Tuliongea mengi sana na Mzungu akanambia kule hotelini ana workmates hivyo atanicheki niwapeleke Morogoro na watakua Tanzania kwa week 2. Tukafika pale Sea cliff hotel nikamdrop tuka exchange contacts.

Jumatano nikiwa mzigoni kama kawaida yangu, alinipigia simu kama nitakua around maeneo ya Sea cliff nimcheki tuongee, jioni nikamcheki akanambia tukutane pale Karambezi cafe.

Tutakutana pale tukaanza story so ishu mezani ilikua ni alikua anatarajia kwenda Morogoro Ijumaa na ndugu zake( jumla watakua 4). Akaniambia tutarudi jumapili hivyo nimpe gharama zangu, nikamwambia badae nitamcheki nikiwa na cost zote. Tuliongea mambo mengi sana ya kimaisha inshort ndani ya muda alikua ametokea kunikubali sana. Bhasi tukaagana pale, katika story zetu nilimwambia na mke na mtoto mmoja hata yeye pia alinambia kaoa ana watoto 2, akanambia Msalimie Junior, before sijaondoka nitakuja kumwona.

Ile night nikamcheki huyu mzungu alikua anaitwa “MANUEL” ni jina lake halisi, nikampa mchanganuo wa gharama zangu nikamwambia hesabu ya jumla kila kitu kitakua chini yangu tukakubaliana $500 kwa zile siku tutakazokua kule Moro. Akanipa kazi nifanye booking ya hotel nzuri kwa ajili ya watu 4 kwa siku 2, that time Morena Hotel ndo ilikua imefunguliwa nika book hotel pale.

Ijumaa asubuhi na mapema nikaenda pale kuwabeba tukaenda Morogoro, nikawadrop pale Morena Hotel, tulifika Morogoro saa5 na dakika kadhaa, siku ileile tukaenda Mzumbe University sijui walikua na Agenda gani pale tukarudi hotelini jion saa11. Manuel akasema “Lets have dinner together” tukaingia hotelini tukaenjoy pale story zilikua nyingi sana, tukapiga na wine za kutosha sana.

Ilikua ishafika saa3 nikawaaga,

“So where are you going to sleep??, hilo lilikua ni swali kutoka kwa Manuel.

Wote wakawa wananitizama wakisubiri jibu. Kuna dada mmoja mzungu akasema , “he doesn’t want to sleep with us here”.

MIMI: No I have my friend here so don’t worry about me guys.

Mimi nilikwenda kwa jamaa yangu anakaa paleple around kihonda stand, nilimpanga mapema. Nilikua nakwepa gharama za hotel,

Asubuhi mapema nikapanda hotelini kuwabeba walikua wanakwenda SUA chuoni sijui walikua na agenda gani, Pale SUA tulitoka mchana ikabidi turudi tena Mzumbe jioni tukarudi hotelin. Kama kawaida have dinner, tukaplan tukirudi dar niwapeleke moja ya viwanja maarufu vya bata.

Jumapili mida ya saa6 mchana tukaanza safari ya kurudi Dar kitu kama kumi kasoro tukawa tumefika. Nikawarudisha pale Sea cliff hotel,

So bro badae tutakwenda wapi? Aliuliza Manuel,

Nikamjibu “Saprise”. Akanambia Ok bro I trust you!!, nikamwambia by 07:00 PM ntakua around kuwachukua, Na mimi nikarudi zangu home. Palepale akanilipa Pesa zangu ambayo tulikubaliana nikapokea, kuja kuhesabu ilikua jumla $550. Nikatabasamu.

Tukiwa parking nilitamani kumwuliza kuhusu wale dada 3 ni nani kwake? lakini nikapotezea nikapanga kumwuliza siku nyingine.” Kweli wale dada walikua ni visu sana kuna mmoja alikua mdogo mdogo hivi nilimwelewa sana.

Nilivyoingia home nikawaza hawa nawapeleka wapi ukicheki leo Jumapili, kwa jumapili sehemu yenye vibe ni Kidimbwi tu ndo watavibe na wale wote pombe wanatumia, so sikupata ukakasi sana.

“Kwa jumapili kidimbwi huwa inajaa sana tuseme ndo kiwanja pekee kwa Jumapili huwa kina vibe hapa mjini”.

Nikapata wazo nifanye booking kabisa “reservation”, maana tukichelewa tutakosa space then niko na hawa wazungu tutaanza hangaika kupata nafasi, sikutaka kupoteza point 3 kwenye vitu vidogo kama hivi.

Nikaingia Instagram nikachukua namba zao nikawapigia simu chap, dada akapokea nikamwambia dhumuni langu akanambia table bado zipo ila I have to make payment before. Nikamwambia dada sikia tuko 5 hawa wengine ni foreigners, sisi tunakuja by 08:00 PM tutakua hapo on time. Dada akawa haelewi hivi akanambia wengi huwa wanapiga simu hawatokei na hii ni biashara huu ndo utaratibu wetu, nikamwambia nakurudia ASAP.

Nika mcall Manuel kumpanga akaniambia good bro! you can proceed. Nikamrudia Dada tena akanambia cost za table kwa VIP inaanzia 500,000 na kuendelea pia akanambia kuna table zingine ili ukae lazima uwe unatumia 200k na kuendelea. Nikaona option 2 ndo nzuri zaidi, akanambia ana reserve ila ikifka muda huo bila taarifa yoyote atawapa watu wengine.

“Bro! tunatoka out, tunakwenda kunywa na kulewa, acha gari tu home kwa usalama zaidi sisi, tunakuja na Uber, nitumie location” ilikua mesage ya Manuel. Nikaona ni jambo jema sana.

By 07:00 PM ontime nikawa nimefika pale Kidimbwi ili kuweka mambo sawa na kuchagua location nzuri. Nikiwa njian nilikua nishampanga dada niko njiani, nilivyofika pale dada Ofcourse akanipeleka moja kwa moja upande wa chini kwa mbele unaona mandhari ya bahari.

Kwenye mbili kasoro Manuel na ndugu zake nao walikua wamefika pale Kidimbwi, ofcourse walikuwa wamependeza sana, niliona jinsi wabongo wakiwatolea macho wale dada waswiss. Walifurahi sana na walipapenda sana pale na yale mazingira walipagawa sana.

Hawa dada 3 wa kizungu ngoja niwape majina yao
“Dada 1, Jina lake Alex, huyu alikua ndo mkubwa age yake ni around 30’s+ hivi”

“Dada 2, jina lake Olivia, huyu alikua around 25-28s”

“Dada 3, jina lake Sophie, huyu alikua mdogo kwa wote age yake 22”. Huyu nilipata muda wa kuzungumza naye vizuri tukiwa Moro,alinitamkia mwenyewe age yake, alikua anasoma bado. Ukweli alikua mzuri sana “kisu”.

*********
Baada ya kuingia ndani wahudumu walikua wanatukimbilia sana, all Eyes on US.

Kila mtu akaagiza anachojua yeye kwa waiter pale, wakati dada anatoka kwenda kufata, Manuel akamnong’eza dada japo alionekana kuelewa alichoongea Manuel.

Baada ya dakika kadhaa dada akaja na Vodka chupa kubwa, mimi niliagiza heineken ila zikaja bucket 2, ikaja backet ya desperados na Corona beer. “Nikajua Manuel alimwambia dada kwa kila order alete backet. Tuka agiza na mishikaki 50 “ yaani kila mtu mishikaki 10”.

*********
Tulianza gambe mapema sana so kadri muda unavyokwenda na watu walizidi kumininika kwa wingi na kufanya mandhari ile izidi kupendeza.

Kuna kitu ambacho nili kinotice kutoka kwa Manuel, nikahisi uwepo wa wale ndugu zake 3 ni kama kuna uhuru anakosa, huko mbele mtakuja kufahamu ni mtu wa namna gani.

Kadri muda unavyozidi kwenda na pombe zilizidi kukolea japo kwa yale mazingira ya upepo wa bahari mwanana wa Kidimbwi ulifanya pombe kuchelewa sana kuchanganya mwilini.

Zikashuka backets zingine tukaendelea kupiga pombe, ukweli wazungu wapo vizuri sana kwenye masuala ya pombe wanakimbiza balaa. Manuel alimaliza ile chupa ya Vodka na alikua ngangari akaagiza nyingine, this time alikua anakunywa na Alex kama wanashare.

Mida ya Saa 9 usiku tukaondoka pale Manuel aka request Uber kurudi Sea cliff na mimi nikarequest kurudi home mbezi beach.

ITAENDELEA KESHO.
Hapa!!!!!!
 
Aise umejua kunifanya mtumwa hapa kwenye hii thread yako. halafu unajua namna ya kumlaizia episode yani inakuweka attention kusubiri the next. We jamaa ni genuis.

Kama sio yale majinga yaliyotuvuruga humu tungekuwa tushapata uhondo wote.
 
EPISODE 21

“Insider……. Nimekubali option ya kwanza kwa zile mbili ulizonipa.”

ENDELEA……..


Na muda huu nilitumia kusogea pale kitandani na kumsogelea karibu maana alikua amekaa kitandani.

“Prisca kwahiyo umekubali kuwa mchepuko?”

Prisca alijibu kwa kutingisha kichwa kuonesha yuko tayari kufanywa kuwa mchepuko wa Insider.

“Kwanini unataka nikufanye mchepuko? Nafikiri option 2 ingekua nzuri zaidi, tuwe washikaji tu.”

“Ulinipa choice sasa nimechagua option ya 1. Nimeridhika hivyo kwa maamuzi yangu.”

“Okay haina shida kama umeamua hivyo ila…..” Prisca alinikatisha wakati nikiendelea kuongea.

“Insider, nioneshe picha za mke mkubwa bhasi nimjue hata kwa picha na mtoto wangu.”

Nilichukua simu ambayo ilikua mezani na nikaanza kumwonesha picha za Mama Junior, pamoja na zile za Junior.

“Insider umefanana sana na mwanao copyright.”

“Risasi zangu mimi ni genuine grade A”

“Hivi na mimi nikipata mimba si tutapata mtoto mzuri sana, tena atakuwa wa kike.”

Yaani tuseme Prisca alikua tayari karidhika kuwa mchepuko kiukweli nilishangaa sana, na bado akaanza kuleta story za kushika mimba, nilimwona mwanamke wa ajabu sana.

“Upate ujauzito na mme wa mtu, are you serious?”

“Insider najikuta natamani kupata mtoto, Junior ni mzuri sana. Najikuta natamani na mimi nipate mtoto.”

“Embu nenda kaoge tuondoke maana ulisema unataka kurudi mapema home au tulale hapahapa?”

“Natamani ila Mzee Mapembe yupo leo, acha nikaoge tuondoke.”

Ile anashuka kitandani nika muwasha kibao cha kalioo “Paaah”

Nilijiona Alpha kwakweli nikasema sasa huyu nitampa sheria zangu ili asije kuleta sintofahamu huko mbeleni, lazima nimcontol kama remote, maana nikifanya makosa tu itakula kwangu.

Na muda huu niliwaza asajili namba mpya ila kwa jina lingine, na pia nitampa ratiba za kuwasiliana naye pamoja na kuchat na mimi.

Na wakati huo alikuwa katoka kuoga kajifunga taulo kuanzia usawa wa matiti kushuka chini, na mimi nilivyomwona tena akiwa vile nikaanza kusisimuka. Na palepale nikamsogolea nikampiga kingine cha kuondokea nyumbani.

Nilimrudisha kwao saa 6 usiku na mimi nikaondoka kurudi kulala.

**********

Asubuhi Muajemi alinipigia simu na akaniomba niende kwake saa4 asubuhi kuna sehemu twende wote, na mimi niliikubali ile offa sikutaka kumkatalia Tajiri.

Saa4 ilipowadia nilikwenda kwa Muajemi na yeye alikua anakaa msasani unaingilia kushoto kabla hujafika Tanesco Mikocheni. Na alikuwa hakai mbali sana na maeneo yale.

Nilifanikiwa kufika pale anapoishi maana alikuwa kanitumia location kupitia Telegram, Muajemi alikua anatumia sana huu mtandao sijui kwanini.

Ilikua ni nyumba ya ghorofa 2 na ilikua nzuri sana na alikua anakaa na mke wake (Mke mdogo) na alikuwa amezaa naye watoto wawili (2).

Mlinzi alinifungulia geti na nikapark gari langu, alitoka dada wa kazi kunikaribisha, na ndani ya dakika chache Muajemi alikua ametoka na tulikaa garden.

MUAJEMI: “Bro! Hapa ndo naishi, jiskie upo nyumbani.”

MIMI: “Ahsante sana”

MUAJEMI: “Dada tuletee chai tunywee hapahapa na Insider.” Nilishangaa kuona dada anajua kuongea kiingereza.

MIMI: “Bro! shemeji yuko wapi?”

MUAJEMI: “Yuko mishemishe anachacharika”

MIMI: “Na watoto?”

MUAJEMI: “Watoto wako shule”

Tulikaa pale na Muajemi tukipiga story mbalimbali na moja kubwa alilisema ana mpango wa kufungua Filling stations hapa Tanzania, ila bado anakutana na upinzani mkubwa sana hasa kutoka kwa wenye mamlaka.

Saa 5 ndo muda tuliotoka pale na tulitumia gari yake Range sport nyeusi. Mimi nilikua sijui tunakwenda wapi lakini tulikwenda mpaka Kigamboni “South Beach hotel”.

Aliniacha na alikwenda kuonana na watu wake na alitumia masaa 3 wakatoka. Baada ya hapo tulikwenda Kurasini kwenye ofisi za Puma, na tukaondoka pale tukarudi Posta.

Tulikwenda kwenye duka moja kubwa la simu ambalo ni la mke wake alinambia hivyo, tukaenda mtaa wa India kwenye maduka ya Jewerly na tukaingia moja ya duka kubwa pale, alinambia nalo ni la mke wake.

“Insider ukitaka pete ya uchumba, pete za harusi, necklaces kila kitu kipo hapa”

“Bro! hizi bei mimi siwezi kwakweli.”

“Wewe utapewa discount usijali.”

Hapo ndo nikajua kumbe zile zawadi alizompa kwa Iryn alizichukua madukani.

Tulitoka hapo tukaenda pale Holliday inn tukapata chakula japo ilikua jion tayari. Na wakati tuko pale tulikuwa tukizungumza mambo mengi sana.

MIMI: “Tanzania una muda gani toka umeanza kuja?”

MUAJEMI: “Bro! Tanzania nimeanza kuja since 2008, kampuni yetu inafanya kazi karibu nchi zote za Africa, tunauza hizo pumps za mashine za sheli, tunauza lubricants za aina zote. Kwa upande wa mafuta kampuni yetu ina deal kama middle man, kwa ufupi tunaingia mikataba na serikali na makampuni mbalimbali hasa kwa Africa.”

MIMI: “Na kuhusu lubricants?”

MUAJEMI: “Bro! sisi ni exporter ila kila nchi tuna Madalali wetu tunaofanya nao kazi, ndo biashara zinavyokwenda hapa duniani, middle man huwezi wakimbia. Mfano tuna export contena 20 za lubricants kuja Tanzania kwa Agent yetu (middle-man) yeye anasupply kwa agents zake.”

Muajemi aliniambia siri nyingi sana hasa kwenye mafuta alisema watu wanapiga sana hela hasa hawa viongozi wa serikali, sitaki kufungua code kabisa. Muajemi alisema viongozi wa Africa wengi ni ma middle man wanakula sana hela huko, invoice zinachezewa balaa, ila mnaoumia ni nyinyi watumiaji wa mwisho.

MIMI: “Vipi mnawasiliana na Iryn?”

MUAJEMI: “Bro hata jana nimempigia simu, nikamwambia mzigo wake umefika tayari, aliniambia nimtumie account yangu anitumie pesa. Nimeshangaa sana na nimeona dharau sana kwangu.”

MIMI: “Hahahaha wewe ulifanyaje?”

MUAJEMI: “Nilimwambia nimempa offa tu, alinambia pia hakuna cha bure hapa duniani”

MIMI: “Unajua nini, we fanya kumwomba mtoke out, uendelee kumsogeza karibu.”

MUAJEMI: “Badae nitaongea naye, ukisha mpelekea mzigo wake.”

Tulitumia kama nusu saa pale na tulielekea Upanga na kuna mtu tulikutana naye ambaye ni Muajemi alikuwa, akatutolea ile mizigo kwenye Box, na zilikua box 7.

Kijana alipanga kwenye buti vizuri na tukaondoka kurudi Msasani, na muda huo ilikua giza limeanza kuingia.

Tuliwasili pale kwake na akanambia jumapili anakwenda Saudi Arabia hivyo lazima aonane na Iryn haraka iwezekanavyo. Mlinzi alikuja akatoa ile mizigo kwenye gari na akaipanga kwnye gari yangu.

Nilimuaga Muajemi pale na alitoa hela mfukoni akanikabidhi mkononi, alizitoa bila kuhesabu. Nilimshukuru pale na nilivyofika kwenye gari na kuhesabu zilikua ni 420,000/=.

Niliwasiliana na Iryn muda ule akasema nitamkuta kwake, nilifika pale nikafungua geti nikaingiza gari ndani. Na muda huo jirani alikua pale nje amekaa kibarazani.

MIMI: “Jirani nakuona umepumzika huna baya.”

JIRAN: “Jirani nimechoka tu.”

MIMI: “Huonekani siku hizi, ulikuwa umesafiri nini?”

JIRANI: “Mimi au wewe? Maana mimi nipo wewe ndo umetutenga bhana.”

MIMI: “Ngoja nikasalimie ndani, badae bhasi.”

JIRANI: “Wahi baba, atakua amekumiss.”

Niliishia kucheka tu nikasema lait Jirani angelijua hata asingesema hivi.

Niliingia ndani nikamkuta Iryn kalala kizembe pale seblen, maana alikua kavaa vile vibukta vifupi sasa mimi nikawa namwangalia pale kwa macho ya kifisi.

IRYN: “Insider vipi mbona sikuelewi?”

MIMI: “Unalalaje kizembe hivo.”

IRYN: “Sasa ulitaka nilalaje?”

MIMI: “Na mizigo yako kutoka kwa Muajemi ipo kwenye gari.”

IRYN: “Wow jana alinambia imefika, ila hataki nimtumie hela yake.”

MIMI: “Muajemi amekupa offa wewe unaleta habari za malipo”

IRYN: “There is no free meal in this world”

MIMI: “What do you mean?”

IRYN: “Twende tukatoe kwenye gari.”

Tulitoka nje na yeye alikuwa na kibukta chake vilevile tukasaidiana kutoa ile mizigo na tukaweka pale nje kibarazani. Na muda huo Jiran alikuwa akituangalia sana.

MIMI: “Hivi hapa kibarazani hawawezi kuiba?”

IRYN: “I don’t think so.”

Bhasi baada ya kumaliza kuweka zile box pale ambazo zilikua no vifaa vya saloon, kutokana na Iryn alisema zile mashine ni advanced kwenye upande wa saloon pia ni ghali. Na alisema zile mashine zimecost $24,000 mpaka kodi pale bandarini na zitakwenda Masaki.

Na wakati huo muda ulikuwa umekwenda sana, ilikua usiku tayari.

“Insider kesho uje mapema twende Posta nikanunue nguo maana nina hitajika kwenda kwenye ofisi ya mama.”

“Unakwenda muda gani?”

“Saa 7 mchana.”

Bhasi na mimi sikukaa pale kabisa nikaaga nikaondoka kurudi home maana nilitaka kurudi mapema nikaongee na Mzee Mollel nijue hata Ujenzi unakwendaje kule Dodoma.

*********

Ratiba zangu za asubuhi zilikuwa vilevile lazima nikawachukue wateja zangu lakini hii week ilikua tofauti kidogo toka nitoke Dodoma. Mtoto wa Mama wa2 naye alikuwa kaanza likizo ya Easter, hivyo nilikua namchukua Maggy tu.

Baada ya kumpeleka Maggy Posta ilibidi niende Kijitonyama mapema kwa Iryn kama tulivyokubaliana. Nilifika pale kwake na alikuwa bado kalala, nilimpigia simu na akatoka kunifungulia mlango.

Tulisalimiana pale na yeye akasema anakwenda kuoga ili tuwai kwenda mapema Posta.

Baada ya kuwasili Posta kuna duka tuliingia la nguo “special”. Iryn alinunua nguo nyingi tu pale za kiofisi ikiwemo suti ya suruali na alikua anajaribisha palepale.

Tulirudi haraka Kijitonyama na alijiandaa pale kwa haraka na alitoka akiwa amependeza sana. Alikuwa kavaa suti ya dark blue na ilionekana kumpendeza sana mrembo Iryn.

Tukaondoka kuelekea Masaki kwenye hio Organization. Muda huo ilikua saa 7 mchana na nilimshusha nje ya geti la Organization.

“Insider nitakupigia nikiwa tayari sawa?” na yeye akaingia ndani.

Mimi nilitoka hapo na nikatafuta chimbo kwa mbele nikapark gari langu.

Lengo kubwa la kwenda kwenye hii Organization ni kufanyiwa interview na kusaini forms, Iryn alisema wanamfanyia interview ili wajue zile pesa atazifanyia nini maana ni nyingi sana kwa umri wake.

Wakati niko kwenye gari nilikua nikiperuzi peruzi kwenye social medias nikiangalia mambo yanayoendelea na kutrend. Na muda huo Mary alinipigia simu, nilishangaa sana kuona akipiga simu.

MIMI: “Mary mambo.”

MARY: “Salama za kunisusa?”

MIMI: “Mimi au wewe ndo umenisusa?”

MARY: “Mimi sijakususa ila uliniboa, na unajua sababu.”

MIMI: “Ok am sorry, sindo unataka kusikia hivi?

MARY: “Insider juzi ulikuwa na Prisca?”

MIMI: “Why?”

MARY: “Insider ulikuwa na Prisca, don’t lie”

MIMI: “Afu Mary mimi sikuelewagi ujue, you keep asking me everyday. Mdogo wako akichelewa kurudi unaniuliza mimi badala umbane Prisca, this behavior has to stop”

MARY: “It’s okay, upo wapi?.”

MIMI: “Niko masaki now, unahitaji usafiri?”

MARY: “Kama utakuwepo Posta, jioni utanambia.”

MIMI: “Sawa Bossy wangu”

Na muda huo alikata simu

Ukweli ni kwamba nikizurura hivi na Iryn nilikuwa naingiza pesa nyingi tu, sikosi laki, laki2 itadepend na yeye hio siku ana mood gani, japo kuna baadhi ya trip nilikua nakataa pesa zake.

Nilisubiri pale kwa almost saa zima nikimsubiri atoke na muda huo ndo alinipigia nisogee ili tuondoke.

Wakati nimesogea pale karibu nilimwona akiwa na Mama Janeth na wakapanda kwenye gari.

“Insider twende Levant tukale nafikiri ni sehem nzuri ambayo imetulia.”

Kutoka kwnye ile Organization hata sio mbali na ndani ya muda mfupi tulikuw pale Levant.

Na kila mmoja aliagiza msosi anaojua yeye na Mama Janeth na Iryn waliendelea kuongea, maana toka tukiwa kwenye gari walikuwa wakiongea sana, ni kama walikuwa wanaendeleza mazungumzo yao.

IRYN: “Mama ndo hivyo kama nilivyokwambia zile mashine zimefika tayari, utaziona ni nzuri sana na zitatusaidia.”

MAMA JANETH: “Na suala la massaji tutapata wataalamu na wakuaminika?”

IRYN: “Mama hata mimi nitawafundisha niko vizuri sana.”

MAMA JANETH: “Sawa mwanangu uwepo wako umekuwa baraka sana.”

IRYN: “Director muda ule alikuwa anasema Organization itanipa sponsorship ya Postgraduate, ni muda gani ita expiry?”

MAMA JANETH: “Hio ni wewe tu sidhani kama ina kikomo, vipi kwanini hutaki kufanyia kazi Organization?”

IRYN: “Mama si nitabanwa sana, na biashara zikayumba?”

MAMA JANETH: “Mbona mama yako alikuwa busy na mambo yalikuwa yanakwenda vizuri tu.”

IRYN: “Mama labda baadae kwa sasa hapana.”

MAMA JANETH: “Pale home unaishije? Maana sijaja na muda.”

IRYN: “Salama ila nafikiri mwezi ujao niondoke, ili uweke mtu ile ni biashara yako. Kipindi kile nilikuwa mgeni ila sasa nishayazoea mazingira, Insider ananisaidia sana.”

MAMA JANETH: “Hata mimi nakuona kuna utofauti mkubwa sana ulikuwa unajifungia tu ndani. Ila pale ni nyumbani unaweza kuendelea kukaa tu mwanangu hata usiwe na wasiwasi.”

IRYN: “Nataka nibadilishe mazingira pia.”

MAMA JANETH: “I understand.”

Tulitumia kama dakika 45 pale Levant na tukaondoka pale, tulimrudisha Mama Janeth kazini na sisi tukaondoka kurudi Kijitonyama.

Na wakati tunarudi tulitumia Kimweri Ave Road, hii barabara inakuja kutokea pale Mikocheni, Mwaikibaki road.

MIMI: “Iryn muda ule nilisikia mkiongea na Mama Janeth kuhusu kuhama pale Kijitonyama.”

IRYN: “Ndio Insider nataka kuhama pale, sikukwambia kama zile Apartments ni za mama Janeth?.”

MIMI: “Hapana hujawai kunambia.”

IRYN: “Ni Apartment zake, wakati nimerudi Tanzania kutoka Ufaransa nilifikia kwa Mama Janeth. Niliona nakosa uhuru wa kutoka usiku na kufanya kazi zangu, ndo nikamwambia nataka kupanga ndo akanionesha apartments mbili ya Mikocheni na hii ya Kijitonyama. Mimi niliipenda ya Kijitonyama ndo akaninulia vitu vyote unavyoviona mle ndani.”

MIMI: “Aisee kumbe”

IRYN: “Insider kukutana na wewe ni kama Baraka kwangu maana nilikuwa mtu wa kujifungia ndani tu.”

MIMI: “Nilikuahidi kukupeleka kula kitimoto na pia nitakupeleka ukale Biriani la selebonge.”

IRYN: “Week tayari hujatimiza ahadi.”

MIMI: “Better late than never.”

IRYN: “Don’t make Promises you can’t keep.”

MIMI: “Sema tumekula tayari, tena leo Ijumaa ningekupeleka pale kwa Selebonge tukale biriani.”

Tulitumia muda mchache kufika pale kwake baada ya kupark gari yeye aliingia ndani na mimi nikaenda kufunga geti.

Niliingia seblen na nikakaa kwenye coach na kwenye meza kulikuwa na kitabu kama magazine tuseme, kilikuwa ni cha mambo ya fashion, nilikuwa nakipitia nakiangalia yaliyomo ndani.

Wakati nikiendelea kuangalia picha za mle ndani nilisikia Iryn akiniita kutoka chumbani kwake,

IRYN: “Insider………”

MIMI: “Nambie mummy”

IRYN: “Come in please.”

MIMI: “In your room?”

IRYN: “Yes are you afraid? Njoo bhasi haraka.”

MIMI: “Okay am coming.”


TO BE CONTINUED

Sunday: 19:00
q
 
EPISODE 21

“Insider……. Nimekubali option ya kwanza kwa zile mbili ulizonipa.”

ENDELEA……..


Na muda huu nilitumia kusogea pale kitandani na kumsogelea karibu maana alikua amekaa kitandani.

“Prisca kwahiyo umekubali kuwa mchepuko?”

Prisca alijibu kwa kutingisha kichwa kuonesha yuko tayari kufanywa kuwa mchepuko wa Insider.

“Kwanini unataka nikufanye mchepuko? Nafikiri option 2 ingekua nzuri zaidi, tuwe washikaji tu.”

“Ulinipa choice sasa nimechagua option ya 1. Nimeridhika hivyo kwa maamuzi yangu.”

“Okay haina shida kama umeamua hivyo ila…..” Prisca alinikatisha wakati nikiendelea kuongea.

“Insider, nioneshe picha za mke mkubwa bhasi nimjue hata kwa picha na mtoto wangu.”

Nilichukua simu ambayo ilikua mezani na nikaanza kumwonesha picha za Mama Junior, pamoja na zile za Junior.

“Insider umefanana sana na mwanao copyright.”

“Risasi zangu mimi ni genuine grade A”

“Hivi na mimi nikipata mimba si tutapata mtoto mzuri sana, tena atakuwa wa kike.”

Yaani tuseme Prisca alikua tayari karidhika kuwa mchepuko kiukweli nilishangaa sana, na bado akaanza kuleta story za kushika mimba, nilimwona mwanamke wa ajabu sana.

“Upate ujauzito na mme wa mtu, are you serious?”

“Insider najikuta natamani kupata mtoto, Junior ni mzuri sana. Najikuta natamani na mimi nipate mtoto.”

“Embu nenda kaoge tuondoke maana ulisema unataka kurudi mapema home au tulale hapahapa?”

“Natamani ila Mzee Mapembe yupo leo, acha nikaoge tuondoke.”

Ile anashuka kitandani nika muwasha kibao cha kalioo “Paaah”

Nilijiona Alpha kwakweli nikasema sasa huyu nitampa sheria zangu ili asije kuleta sintofahamu huko mbeleni, lazima nimcontol kama remote, maana nikifanya makosa tu itakula kwangu.

Na muda huu niliwaza asajili namba mpya ila kwa jina lingine, na pia nitampa ratiba za kuwasiliana naye pamoja na kuchat na mimi.

Na wakati huo alikuwa katoka kuoga kajifunga taulo kuanzia usawa wa matiti kushuka chini, na mimi nilivyomwona tena akiwa vile nikaanza kusisimuka. Na palepale nikamsogolea nikampiga kingine cha kuondokea nyumbani.

Nilimrudisha kwao saa 6 usiku na mimi nikaondoka kurudi kulala.

**********

Asubuhi Muajemi alinipigia simu na akaniomba niende kwake saa4 asubuhi kuna sehemu twende wote, na mimi niliikubali ile offa sikutaka kumkatalia Tajiri.

Saa4 ilipowadia nilikwenda kwa Muajemi na yeye alikua anakaa msasani unaingilia kushoto kabla hujafika Tanesco Mikocheni. Na alikuwa hakai mbali sana na maeneo yale.

Nilifanikiwa kufika pale anapoishi maana alikuwa kanitumia location kupitia Telegram, Muajemi alikua anatumia sana huu mtandao sijui kwanini.

Ilikua ni nyumba ya ghorofa 2 na ilikua nzuri sana na alikua anakaa na mke wake (Mke mdogo) na alikuwa amezaa naye watoto wawili (2).

Mlinzi alinifungulia geti na nikapark gari langu, alitoka dada wa kazi kunikaribisha, na ndani ya dakika chache Muajemi alikua ametoka na tulikaa garden.

MUAJEMI: “Bro! Hapa ndo naishi, jiskie upo nyumbani.”

MIMI: “Ahsante sana”

MUAJEMI: “Dada tuletee chai tunywee hapahapa na Insider.” Nilishangaa kuona dada anajua kuongea kiingereza.

MIMI: “Bro! shemeji yuko wapi?”

MUAJEMI: “Yuko mishemishe anachacharika”

MIMI: “Na watoto?”

MUAJEMI: “Watoto wako shule”

Tulikaa pale na Muajemi tukipiga story mbalimbali na moja kubwa alilisema ana mpango wa kufungua Filling stations hapa Tanzania, ila bado anakutana na upinzani mkubwa sana hasa kutoka kwa wenye mamlaka.

Saa 5 ndo muda tuliotoka pale na tulitumia gari yake Range sport nyeusi. Mimi nilikua sijui tunakwenda wapi lakini tulikwenda mpaka Kigamboni “South Beach hotel”.

Aliniacha na alikwenda kuonana na watu wake na alitumia masaa 3 wakatoka. Baada ya hapo tulikwenda Kurasini kwenye ofisi za Puma, na tukaondoka pale tukarudi Posta.

Tulikwenda kwenye duka moja kubwa la simu ambalo ni la mke wake alinambia hivyo, tukaenda mtaa wa India kwenye maduka ya Jewerly na tukaingia moja ya duka kubwa pale, alinambia nalo ni la mke wake.

“Insider ukitaka pete ya uchumba, pete za harusi, necklaces kila kitu kipo hapa”

“Bro! hizi bei mimi siwezi kwakweli.”

“Wewe utapewa discount usijali.”

Hapo ndo nikajua kumbe zile zawadi alizompa kwa Iryn alizichukua madukani.

Tulitoka hapo tukaenda pale Holliday inn tukapata chakula japo ilikua jion tayari. Na wakati tuko pale tulikuwa tukizungumza mambo mengi sana.

MIMI: “Tanzania una muda gani toka umeanza kuja?”

MUAJEMI: “Bro! Tanzania nimeanza kuja since 2008, kampuni yetu inafanya kazi karibu nchi zote za Africa, tunauza hizo pumps za mashine za sheli, tunauza lubricants za aina zote. Kwa upande wa mafuta kampuni yetu ina deal kama middle man, kwa ufupi tunaingia mikataba na serikali na makampuni mbalimbali hasa kwa Africa.”

MIMI: “Na kuhusu lubricants?”

MUAJEMI: “Bro! sisi ni exporter ila kila nchi tuna Madalali wetu tunaofanya nao kazi, ndo biashara zinavyokwenda hapa duniani, middle man huwezi wakimbia. Mfano tuna export contena 20 za lubricants kuja Tanzania kwa Agent yetu (middle-man) yeye anasupply kwa agents zake.”

Muajemi aliniambia siri nyingi sana hasa kwenye mafuta alisema watu wanapiga sana hela hasa hawa viongozi wa serikali, sitaki kufungua code kabisa. Muajemi alisema viongozi wa Africa wengi ni ma middle man wanakula sana hela huko, invoice zinachezewa balaa, ila mnaoumia ni nyinyi watumiaji wa mwisho.

MIMI: “Vipi mnawasiliana na Iryn?”

MUAJEMI: “Bro hata jana nimempigia simu, nikamwambia mzigo wake umefika tayari, aliniambia nimtumie account yangu anitumie pesa. Nimeshangaa sana na nimeona dharau sana kwangu.”

MIMI: “Hahahaha wewe ulifanyaje?”

MUAJEMI: “Nilimwambia nimempa offa tu, alinambia pia hakuna cha bure hapa duniani”

MIMI: “Unajua nini, we fanya kumwomba mtoke out, uendelee kumsogeza karibu.”

MUAJEMI: “Badae nitaongea naye, ukisha mpelekea mzigo wake.”

Tulitumia kama nusu saa pale na tulielekea Upanga na kuna mtu tulikutana naye ambaye ni Muajemi alikuwa, akatutolea ile mizigo kwenye Box, na zilikua box 7.

Kijana alipanga kwenye buti vizuri na tukaondoka kurudi Msasani, na muda huo ilikua giza limeanza kuingia.

Tuliwasili pale kwake na akanambia jumapili anakwenda Saudi Arabia hivyo lazima aonane na Iryn haraka iwezekanavyo. Mlinzi alikuja akatoa ile mizigo kwenye gari na akaipanga kwnye gari yangu.

Nilimuaga Muajemi pale na alitoa hela mfukoni akanikabidhi mkononi, alizitoa bila kuhesabu. Nilimshukuru pale na nilivyofika kwenye gari na kuhesabu zilikua ni 420,000/=.

Niliwasiliana na Iryn muda ule akasema nitamkuta kwake, nilifika pale nikafungua geti nikaingiza gari ndani. Na muda huo jirani alikua pale nje amekaa kibarazani.

MIMI: “Jirani nakuona umepumzika huna baya.”

JIRAN: “Jirani nimechoka tu.”

MIMI: “Huonekani siku hizi, ulikuwa umesafiri nini?”

JIRANI: “Mimi au wewe? Maana mimi nipo wewe ndo umetutenga bhana.”

MIMI: “Ngoja nikasalimie ndani, badae bhasi.”

JIRANI: “Wahi baba, atakua amekumiss.”

Niliishia kucheka tu nikasema lait Jirani angelijua hata asingesema hivi.

Niliingia ndani nikamkuta Iryn kalala kizembe pale seblen, maana alikua kavaa vile vibukta vifupi sasa mimi nikawa namwangalia pale kwa macho ya kifisi.

IRYN: “Insider vipi mbona sikuelewi?”

MIMI: “Unalalaje kizembe hivo.”

IRYN: “Sasa ulitaka nilalaje?”

MIMI: “Na mizigo yako kutoka kwa Muajemi ipo kwenye gari.”

IRYN: “Wow jana alinambia imefika, ila hataki nimtumie hela yake.”

MIMI: “Muajemi amekupa offa wewe unaleta habari za malipo”

IRYN: “There is no free meal in this world”

MIMI: “What do you mean?”

IRYN: “Twende tukatoe kwenye gari.”

Tulitoka nje na yeye alikuwa na kibukta chake vilevile tukasaidiana kutoa ile mizigo na tukaweka pale nje kibarazani. Na muda huo Jiran alikuwa akituangalia sana.

MIMI: “Hivi hapa kibarazani hawawezi kuiba?”

IRYN: “I don’t think so.”

Bhasi baada ya kumaliza kuweka zile box pale ambazo zilikua no vifaa vya saloon, kutokana na Iryn alisema zile mashine ni advanced kwenye upande wa saloon pia ni ghali. Na alisema zile mashine zimecost $24,000 mpaka kodi pale bandarini na zitakwenda Masaki.

Na wakati huo muda ulikuwa umekwenda sana, ilikua usiku tayari.

“Insider kesho uje mapema twende Posta nikanunue nguo maana nina hitajika kwenda kwenye ofisi ya mama.”

“Unakwenda muda gani?”

“Saa 7 mchana.”

Bhasi na mimi sikukaa pale kabisa nikaaga nikaondoka kurudi home maana nilitaka kurudi mapema nikaongee na Mzee Mollel nijue hata Ujenzi unakwendaje kule Dodoma.

*********

Ratiba zangu za asubuhi zilikuwa vilevile lazima nikawachukue wateja zangu lakini hii week ilikua tofauti kidogo toka nitoke Dodoma. Mtoto wa Mama wa2 naye alikuwa kaanza likizo ya Easter, hivyo nilikua namchukua Maggy tu.

Baada ya kumpeleka Maggy Posta ilibidi niende Kijitonyama mapema kwa Iryn kama tulivyokubaliana. Nilifika pale kwake na alikuwa bado kalala, nilimpigia simu na akatoka kunifungulia mlango.

Tulisalimiana pale na yeye akasema anakwenda kuoga ili tuwai kwenda mapema Posta.

Baada ya kuwasili Posta kuna duka tuliingia la nguo “special”. Iryn alinunua nguo nyingi tu pale za kiofisi ikiwemo suti ya suruali na alikua anajaribisha palepale.

Tulirudi haraka Kijitonyama na alijiandaa pale kwa haraka na alitoka akiwa amependeza sana. Alikuwa kavaa suti ya dark blue na ilionekana kumpendeza sana mrembo Iryn.

Tukaondoka kuelekea Masaki kwenye hio Organization. Muda huo ilikua saa 7 mchana na nilimshusha nje ya geti la Organization.

“Insider nitakupigia nikiwa tayari sawa?” na yeye akaingia ndani.

Mimi nilitoka hapo na nikatafuta chimbo kwa mbele nikapark gari langu.

Lengo kubwa la kwenda kwenye hii Organization ni kufanyiwa interview na kusaini forms, Iryn alisema wanamfanyia interview ili wajue zile pesa atazifanyia nini maana ni nyingi sana kwa umri wake.

Wakati niko kwenye gari nilikua nikiperuzi peruzi kwenye social medias nikiangalia mambo yanayoendelea na kutrend. Na muda huo Mary alinipigia simu, nilishangaa sana kuona akipiga simu.

MIMI: “Mary mambo.”

MARY: “Salama za kunisusa?”

MIMI: “Mimi au wewe ndo umenisusa?”

MARY: “Mimi sijakususa ila uliniboa, na unajua sababu.”

MIMI: “Ok am sorry, sindo unataka kusikia hivi?

MARY: “Insider juzi ulikuwa na Prisca?”

MIMI: “Why?”

MARY: “Insider ulikuwa na Prisca, don’t lie”

MIMI: “Afu Mary mimi sikuelewagi ujue, you keep asking me everyday. Mdogo wako akichelewa kurudi unaniuliza mimi badala umbane Prisca, this behavior has to stop”

MARY: “It’s okay, upo wapi?.”

MIMI: “Niko masaki now, unahitaji usafiri?”

MARY: “Kama utakuwepo Posta, jioni utanambia.”

MIMI: “Sawa Bossy wangu”

Na muda huo alikata simu

Ukweli ni kwamba nikizurura hivi na Iryn nilikuwa naingiza pesa nyingi tu, sikosi laki, laki2 itadepend na yeye hio siku ana mood gani, japo kuna baadhi ya trip nilikua nakataa pesa zake.

Nilisubiri pale kwa almost saa zima nikimsubiri atoke na muda huo ndo alinipigia nisogee ili tuondoke.

Wakati nimesogea pale karibu nilimwona akiwa na Mama Janeth na wakapanda kwenye gari.

“Insider twende Levant tukale nafikiri ni sehem nzuri ambayo imetulia.”

Kutoka kwnye ile Organization hata sio mbali na ndani ya muda mfupi tulikuw pale Levant.

Na kila mmoja aliagiza msosi anaojua yeye na Mama Janeth na Iryn waliendelea kuongea, maana toka tukiwa kwenye gari walikuwa wakiongea sana, ni kama walikuwa wanaendeleza mazungumzo yao.

IRYN: “Mama ndo hivyo kama nilivyokwambia zile mashine zimefika tayari, utaziona ni nzuri sana na zitatusaidia.”

MAMA JANETH: “Na suala la massaji tutapata wataalamu na wakuaminika?”

IRYN: “Mama hata mimi nitawafundisha niko vizuri sana.”

MAMA JANETH: “Sawa mwanangu uwepo wako umekuwa baraka sana.”

IRYN: “Director muda ule alikuwa anasema Organization itanipa sponsorship ya Postgraduate, ni muda gani ita expiry?”

MAMA JANETH: “Hio ni wewe tu sidhani kama ina kikomo, vipi kwanini hutaki kufanyia kazi Organization?”

IRYN: “Mama si nitabanwa sana, na biashara zikayumba?”

MAMA JANETH: “Mbona mama yako alikuwa busy na mambo yalikuwa yanakwenda vizuri tu.”

IRYN: “Mama labda baadae kwa sasa hapana.”

MAMA JANETH: “Pale home unaishije? Maana sijaja na muda.”

IRYN: “Salama ila nafikiri mwezi ujao niondoke, ili uweke mtu ile ni biashara yako. Kipindi kile nilikuwa mgeni ila sasa nishayazoea mazingira, Insider ananisaidia sana.”

MAMA JANETH: “Hata mimi nakuona kuna utofauti mkubwa sana ulikuwa unajifungia tu ndani. Ila pale ni nyumbani unaweza kuendelea kukaa tu mwanangu hata usiwe na wasiwasi.”

IRYN: “Nataka nibadilishe mazingira pia.”

MAMA JANETH: “I understand.”

Tulitumia kama dakika 45 pale Levant na tukaondoka pale, tulimrudisha Mama Janeth kazini na sisi tukaondoka kurudi Kijitonyama.

Na wakati tunarudi tulitumia Kimweri Ave Road, hii barabara inakuja kutokea pale Mikocheni, Mwaikibaki road.

MIMI: “Iryn muda ule nilisikia mkiongea na Mama Janeth kuhusu kuhama pale Kijitonyama.”

IRYN: “Ndio Insider nataka kuhama pale, sikukwambia kama zile Apartments ni za mama Janeth?.”

MIMI: “Hapana hujawai kunambia.”

IRYN: “Ni Apartment zake, wakati nimerudi Tanzania kutoka Ufaransa nilifikia kwa Mama Janeth. Niliona nakosa uhuru wa kutoka usiku na kufanya kazi zangu, ndo nikamwambia nataka kupanga ndo akanionesha apartments mbili ya Mikocheni na hii ya Kijitonyama. Mimi niliipenda ya Kijitonyama ndo akaninulia vitu vyote unavyoviona mle ndani.”

MIMI: “Aisee kumbe”

IRYN: “Insider kukutana na wewe ni kama Baraka kwangu maana nilikuwa mtu wa kujifungia ndani tu.”

MIMI: “Nilikuahidi kukupeleka kula kitimoto na pia nitakupeleka ukale Biriani la selebonge.”

IRYN: “Week tayari hujatimiza ahadi.”

MIMI: “Better late than never.”

IRYN: “Don’t make Promises you can’t keep.”

MIMI: “Sema tumekula tayari, tena leo Ijumaa ningekupeleka pale kwa Selebonge tukale biriani.”

Tulitumia muda mchache kufika pale kwake baada ya kupark gari yeye aliingia ndani na mimi nikaenda kufunga geti.

Niliingia seblen na nikakaa kwenye coach na kwenye meza kulikuwa na kitabu kama magazine tuseme, kilikuwa ni cha mambo ya fashion, nilikuwa nakipitia nakiangalia yaliyomo ndani.

Wakati nikiendelea kuangalia picha za mle ndani nilisikia Iryn akiniita kutoka chumbani kwake,

IRYN: “Insider………”

MIMI: “Nambie mummy”

IRYN: “Come in please.”

MIMI: “In your room?”

IRYN: “Yes are you afraid? Njoo bhasi haraka.”

MIMI: “Okay am coming.”


TO BE CONTINUED

Sunday: 19:00
Umeenda kumpa joto wewe
 
Hii story siipendi natoa sababu.
1.unataka tujue umepiga hatua sijui unawatu wakubwa sijui wa njee yaani kuna vitu vinaonyesha unajionyesha au upo kwenye matangazo,either ya kibiashara au yakinini. Yaani haupo real kuhadithia story ya huyu demu ,jingine kwenye hii story lazima ujue hili haihiitaji utuanzie undani wa maisha yako sana ingekuwa imeisha unatoa na prove yanini siuende kwenye point ya huyo msichana na baadhi ya vitu vyako vya muhimu pale mwanzo ni sawa katikati ulipoanza kujielezea undani wa biashara basi hujanivutia tena inaboa
 
Hii story siipendi natoa sababu.
1.unataka tujue umepiga hatua sijui unawatu wakubwa sijui wa njee yaani kuna vitu vinaonyesha unajionyesha au upo kwenye matangazo,either ya kibiashara au yakinini. Yaani haupo real kuhadithia story ya huyu demu ,jingine kwenye hii story lazima ujue hili haihiitaji utuanzie undani wa maisha yako sana ingekuwa imeisha unatoa na prove yanini siuende kwenye point ya huyo msichana na baadhi ya vitu vyako vya muhimu pale mwanzo ni sawa katikati ulipoanza kujielezea undani wa biashara basi huja

Hii story siipendi natoa sababu.
1.unataka tujue umepiga hatua sijui unawatu wakubwa sijui wa njee yaani kuna vitu vinaonyesha unajionyesha au upo kwenye matangazo,either ya kibiashara au yakinini. Yaani haupo real kuhadithia story ya huyu demu ,jingine kwenye hii story lazima ujue hili haihiitaji utuanzie undani wa maisha yako sana ingekuwa imeisha unatoa na prove yanini siuende kwenye point ya huyo msichana na baadhi ya vitu vyako vya muhimu pale mwanzo ni sawa katikati ulipoanza kujielezea undani wa biashara basi hujanivutia tena inaboa
Mkuu, binadamu hatufanani ndo maana HUWEZI kumridhisha kila mtu. Mimi huo undani wa maisha yake na watu aliokutana nao kwangu raha Sana. Kuna vitu vingi navipata kupitia hizo details. Pole mkuu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom