Jini wa daraja la Salendar

Jini wa daraja la Salendar

JINI WA DARAJA LA SALENDA......EP.10.


ILIPOISHIA;
“Nawe ulipakwa mafuta yale ambayo hutumia majini wa kike, kujipaka sehemu za siri ambayo huongeza raha ya mapenzi kiasi cha kumfanya mwanaume asikuchoke na yeye kusikia raha ya mapenzi. Hata wewe hukuchoka na kusikia raha muda wote wa kufanya mapenzi na ulipoamka hukusikia uchovu wa mwili. Kwa kutumia mafuta yale unaweza kufanya mapenzi kila siku bila kuchoka.”
“Mmh! Kumbe.”

“Wakati wewe unakula raha ndiyo siku hiyo shoga yako yalimtokea kama yaliyokutokea siku za nyuma za mumeo kupoteza nguvu za kiume. Shogayo alikuja kazini akiamini ungeungana naye kwenye tatizo lake, lakini ilikuwa kinyume kitu kilichomchanganya mwenzako na kuwa njia panda tatizo la nguvu za kiume za mpenzi wake lilitokana na nini.

“Baada ya jini Balkis kuwachanganya wazo la kutafuta ufumbuzi wa tatizo lenu lilifutika. Hali ile mwenzako aliamini huenda itaisha kutokana wewe kumhakikishia huenda tatizo lake likaisha kama lako bila kwenda popote. Naye aliamini na kumpa nafasi jini Balkis kufanya mapenzi na mpenziwe usingizini kufikia hatua ya kutokuwa na hamu naye. SASA ENDELEA...

“Baada ya kuweza kukuchanganyeni akili, penzi mlilofanya na mumeo lilirudisha mapenzi yaliyoanza kutoweka. Kitu kile kilimuudhi sana jini Balkis na kuamua kukukomoa. Najua alichokufanya nikikueleza utaogopa lakini kwa vile umetaka mwenyewe sina budi kukueleza,” kauli ya mganga ilinitisha lakini kwa vile maji nilikwisha yavulia nguo nilikuwa sina budi kuyaoga. Basi mganga akaendelea.

“Usiku mlipokuwa mkifanya mapenzi bila kuzima taa jini Balkis alishindwa kufanya kitu chochote, kosa kubwa mlilofanya japo msingeweza kujua madhara yake. Nina imani mapenzi uliyofanya wakati wa giza na mwanga kuna mabadiliko yalitokea ulipofanya mapenzi?”
“Ndiyo.”

“Mlipokuwa mkifanya mapenzi gizani ulihisi maumbile ya mumeo kuwa makubwa na kusababisha uumie sana badala ya raha ikawa maumivu.”
“Ni kweli kabisa.”

“Basi wakati mlipokuwa mkifanya mapenzi gizani, mumeo aliondolewa juu yako na jini Balkis aliingiza mguu wake uliokuwa na kwato kama mbuzi na kuanza kukusukumia ndani.”
Kauli ile ilinifanya nisijikie vibaya mpaka tumbo likaanza kunikata chini ya kitovu, nikiwa navuja jasho la hofu. Mganga aliendelea kunieleza maneno niliyohisi yananikata maini.

“Basi ulijikuta ukivumilia huku ukiumia, ilifikia hatua kutotamani tena kufanya mapenzi na mumeo kwa kuamini maumbile yake yameongezeka ukubwa. Lakini ulipowasha taa ulishangaa kuyaona ya kawaida uliyoyazoea, kweli si kweli?”

“Kweli,” nilijibu huku nikizidi kumuogopa mganga kuwa na uwezo wa ajabu kuyajua mambo ambayo hakuyaona lakini utafikiri alikuwepo.
“Ajabu hukumwambia mumeo, kwa nini?”
“Hata sijui,” nilimjibu.

“Baada ya kuamua kutofanya mapenzi na mumeo kuogopa kuumizwa badala ya kupewa raha, uliamua kutafuta visingizio ili usikutane naye kimwili, uongo kweli?”
“Kweli.”
“Jana kuna kitu cha ajabu kimekutokea ndiyo sababu ya kumpigia simu Bi mkubwa wako?”

“Ni kweli.”
“Basi, baada ya kuona hufanyi tena mapenzi na mumeo, jana ulipolala uliota ndoto kuna mtu anakuingiza mkono sehemu zako za siri na kuanza kukukoroga kama anavuta kitu toka sehemu zako cha siri na ulipoamka ulijikuta ukitoka damu ambazo uliamini ni za hedhi japo ulishangaa kutokwa na damu ya hedhi mara mbili kwa mwezi kitu ambacho hakikuwahi kukutokea maishani mwako.”
“Ni kweli.”

“Unajua madhara yake?”
“Hapana!.”
“Naomba uwe na moyo mgumu kwa vile alichokifanya kwa tiba ya kubabaisha hutapona milele.”
“Mungu wangu,” kauli ilitushtua mimi na mama na kujiuliza ni ugonjwa gani tena huo Yaillah.

“Baba ni ugonjwa gani tena huo?” Ilibidi mama aulize baada ya mimi kuwa katika wakati mgumu nilishika mikono kifuani, nilimuomba Mungu aniepushe na balaa linalotaka kunikumba.

“Jina Balkis alijiulaumu kwa kuamini alifanya kosa ambalo aliliona limempotezea mapenzi ya mumeo kwake,” mganga alimjibu mama.
“Mapenzi yapi hayo?” Mama aliendelea kuuliza.

“Kosa kubwa alilofanya ni kumpaka mafuta ya kuongeza ladha ya mapenzi mwanao, kumbuka maumbile ya jini na mwanadamu yanatofautiana, kwa vile yako ya kibinadamu baada ya kukupaka ilizidi raha mara dufu na thamani yake kwa mumeo ilishuka. Alichokifanya kilikuwa kukutoa kizazi kitu ambacho ndicho kitakacho vunja ndoa yenu. Katika ndoto ulichokiota ndicho kilichotendeka usiku wa jana. Jini Balkis alikutoa kizazi na sasa hivi huwezi kuzaa tena maishani mwako.”

“Mungu wangu,” kauli ya mganga ilinikata maini.
“Sasa baba utatusaidia vipi?” Mama bado alikuwa na ujasiri kutaka kujua nini hatima ya ukatiri wa jini Balkis kwangu.
“Mmh! Ndiyo maana nikasema ipo kazi tena kazi kubwa sana si ya kitoto na tukifanya mchezo tutapotea wote.”

“Jamani, tupotee kivipi?”
“Vita yake ni kubwa sana, kumdhibiti naweza lakini kama nitakufanyia kinga ya kukufunga huwezi kupona tena. Na kosa lolote linaweza kuhatarisha maisha yetu. Hawezi kukubali kuona anazuiwa kutimiza dhamira yake, kwa kutumia nguvu zake anaweza kututeketeza wote.”

“Unataka kutuambia kuna uwezekano wa kupona?”
“Upo, lakini ndiyo mzame sana.”
“Baba wewe huwezi?” Mama aliuliza tena kwa vile mimi nilikuwa nimechanganyikiwa kwa niliyoyasikia.

“Uongo mbaya, mimi siwezi kukirudisha kizazi chake, si yeye ni wanawake wengi wametolewa na yote kaenda kuiweka chini ya bahari kwenye mwamba wa maji yaliyotulia pia hayafikiwi na kitu chochote kitakachoweza kugusa kizazi kile. Kama utaenda hospitalini wanawake wengi wanasumbuliwa na maradhi ya tumbo na wengi maradhi yao kwa tiba ya kisasa hayaonekani lakini siri ni kwamba wengi wao wameondolewa kizazi na kingine sasa hivi matatizo ya nguvu za kiume yamekuwa mengi ambayo yameweka migogolo lakini mabwana hao wakifanya mapenzi ndotoni na mwanamke mzuri hujikuta hawana hamu na wake zao.”

“Ni kwa sababu gani?” Mama aliuliza.
“Hakuna sababu nyingine ni ya huyo huyo jini Balkis ambaye amekuja duniani kwa sababu ya kuharibu ndoa za watu pia kupata tiba ya tatizo lake la uzazi. Tatizo hili litakwisha akiisha maliza kazi yake ya kupata vizazi mia, ambao walipata bahati ya kutokutana naye. Lakini wengine wote ambao hawatapata tiba mapema ndiyo watakuwa tasa milele.”

Siri nzito za jini Balkis zinazidi kufunguka, nini hatma ya yote je kuna tiba sahihi ya tatizo hilo? Kuyajua yote hayo? Endelea hapa chini







JINI LA DARAJA LA SALENDA.......EP.11


ILIPOISHIA:
Eneo hilo halifikiwi na kitu chochote kinachoweza kugusa kizazi kile. Kama utaenda mahospitalini wanawake wengi wanasumbuliwa na maradhi ya tumbo. Wengi maradhi yao hayaonekani kwa vipimo vya kisasa lakini siri ni kwamba wengi wao wameondolewa vizazi.

Kingine sasa hivi matatizo ya nguvu za kiume yamekuwa mengi ambayo yamesababisha migogoro mikubwa. Wanaume hao wakifanya mapenzi ndotoni na mwanamke mzuri hujikuta hawana hamu na wake zao.”
“Ni kwa sababu gani?” Mama aliuliza.

“Hakuna sababu nyingine zaidi ya huyo huyo jini Balkis ambaye amekuja duniani kwa sababu ya kuharibu ndoa za watu pia kutafuta tiba ya tatizo lake la uzazi. Tatizo hili litakwisha akishamaliza kazi yake ya kupata vizazi mia. Watakaokuwa na bahati ya kutokutana naye watasalimika. Lakini wengine wote ambao hawatapata tiba mapema ndiyo watakuwa matasa milele.” SASA ENDELEA...

“Unafikiri ni mganga gani anaweza kutusaidia?” Nilimuuliza nikiwa nimekata tamaa.

“Mmh! Nendeni Bagamoyo kwa mzee mmoja maarufu sana maeneo ya Mlingotini, anaitwa Ustaadh Sudi Makata.”
“Una uhakika?”

“Japo sina uhakika kwa asilimia mia, lakini yule bwana namwamini sana.”
“Tutamjuaje?”
“Mkifika pale Bagamoyo maeneo ya Mlingotini muulizeni mzee Njiwa Manga.”

“Ni tofauti na ustaadhi Makata?”
“Hapana ndiye huyo huyo Makata, jina la Njiwa Manga kapewa na watoto aliokuwa akiwatuma wamkamatie njiwa manga kwa ajili ya kazi zake za majini. Kila mtoto aliyetumwa akimuona alimwita babu wa njiwa manga. Basi ikawa njiwa manga, njiwa manga mpaka leo.”
“Mmh! Tutajitahidi twende haraka.”

“Wala msiwe na haraka, jipangeni kwani tatizo limekwishatokea,” mganga alitutuliza.
“Sawa tutafanya hivyo.”

“Ila leo nitakupa dawa ya kuoga na kufukiza ndani mwako, lakini hapa naona itakuwa vigumu kwa vile mumeo haamini ushirikina. Kwa hiyo dawa ya kufukiza iache ila utaoga hii ambayo itakusaidia kumfukuza jini Balkis asikusogelee. Pia kuna kitu nilisahau kuwaeleza, leo wakati mnarudi nyumbani kutoka ofisini, mlipofika daraja la Salenda mlimuona mwanamke mmoja mrembo sana akiwa amesimama pembeni ya barabara chini ya mti?”
“Ndiyo.”

“Baada ya hapo gari lilizima ghafla?”
“Ndiyo.”
“Yule mwanamke mlimuona akibadilika mavazi?”
“Ndiyo.”
“Basi yule ndiye jini Balkis, ni mwanamke mzuri sana ambaye hakuna mwanaume yoyote anayemtaka akamkataa. Lakini ana roho mbaya, kwa sababu ana matatizo ya uzazi, dawa aliyoelezwa ni kutafuta vizazi vya wanawake mia moja ili atengenezewe dawa ya kupata mtoto.”

“Mungu wangu, kama ni hivyo unafikiri nitaweza kupona kweli?” Niliuliza kwa sauti ya kukata tamaa.
“Ukiwahi utapona! Mpaka sasa inaonesha ana vizazi ishirini na mbili, bado vingi na havipati kwa urahisi namna hiyo.”
“Mbona mzuri sana, jini gani anavaa nguo kama binadamu, si huwa nasikia wana mabawa?”

“Wenye mbawa si majini bali malaika, wao ni kama binadamu kabisa, wanaishi maisha kama watu ila wamepewa uwezo wa kujibadili kuwa katika umbile lolote watakalo, pia wana nguvu za ajabu walizobarikiwa na Mungu za kuonekana wanapopenda wao.”
“Kumbe!”

“Alifanya vile ili mmuone, baada ya hapo aliondoka na ninyi gari lenu liliweza kuondoka, kitu ambacho kiliwahi kumtokea shoga yako siku aliyohudhuria sherehe ya kuagwa jini Balkis kuja duniani rasmi. Mlipofika nyumbani kwako kuna kitu kimoja kilitokea ambacho shoga yako ilifikia hatua ya kukufikiria vibaya na kuamini huenda na wewe ni jini.”

“Mungu wangu, kitu gani hicho?”
“Alipoingia ndani taswira ya sura ya jini Balkis ilitanda kwenye uso wa mama yako, kitu kilichomshtua sana. Baadaye alijiondoa na bi mkubwa kuwa katika hali yake ya kawaida. Shoga yako aliondoka akiwa hakuamini kabisa. Kama unabisha ukirudi nyumbani muulize kaona nini.”

Basi baada ya maelezo yale tulirudi, huwezi kuamini kidogo gari linishinde kuendesha kutokana na mshtuko nilioupata. Lakini mama alinipa moyo kwa kuniambia ili nipate ukweli wa kile nilichoambiwa na mganga lazima niende kwa waganga zaidi ya mmoja. Lakini nilimweleza mama mbona yote aliyoyasema yana ukweli kwa asilimia mia?

Lakini mama alinieleza inawezekana ni kweli kwa asilimia kumi, mengine tusiyoyajua huwa ni uongo wa waganga ili kujipatia pesa. Nilimueleza mbona hakutaka pesa zaidi ya kutueleza twende kwa mganga mwenye uwezo zaidi yake.

Mama alinikata maini kwa kunieleza kuwa waganga wana tabia ya kutafutiana wagonjwa na kugawana pesa kwa kuufanya ugonjwa uonekane mkubwa usioweza kutibiwa. Tukienda kwa mganga mwenzake tutaambiwa pesa nyingi ambazo hatutaweza kukataa.

“Kwa hiyo mama hata kutolewa kizazi ni uongo?” Nilimuuliza.
“Uongo, nilishindwa kumkatalia angeona namuingilia kwenye kazi yake.”

“Kwa hiyo mama nisiwe na wasiwasi?”
“Ondoa wasiwasi, kitu kama hicho hakipo.”
Basi shoga niliporudi kidogo moyo ulitulia japo maelezo yote kila nilipoyafikiria mwili ulisisimka. Niliporudi hata bila kupumzika nikakupigia simu. Basi shoga habari ndiyo hiyo tumekamatwa na jini sijui Balkis,” Sharifa alimueleza Suzy aliyekuwa ametulia kama sanamu asiamini alichokisikia toka kwa shoga yake.

“Sharifa acha kuligeuza jina lake si umesema anaitwa Balkis.”
“Kweli, Balkis.”
“Mmh! Mbona kama...”
“Kama nini?”

“Sijaelewa basi inaonekana hata mimi ana mengi juu yangu, kuna umuhimu kesho kunipeleka na mimi,” Suzy alimweleza shoga yake huku wasiwasi ukiongezeka moyoni mwake kwa kuamini mpenzi wake anaweza kumuacha kwa penzi la ndotoni na jini Balkis linalotumia dawa ya kuongeza ladha ya mapenzi na yeye kuonekana si mali kitu.

“Sawa tutakwenda.”
Waliagana kwa Suzana kurudi nyumbani kwake kutafakari aliyoelezwa na Sharifa, moyoni alikuwa na mambo mawili; kukubali na kukataa. Akili yake ilikuwa kwenye kukataa na kuamini hakuna vitu kama vile. Etaendelea baadae......................


 
acha saund wewe jombaa...watu daile tuna cruz mitaaa hiyo mida mibovu..lakini hamna udasi..halafu ni very rare cases kwa dereva kusimama kati kati ya barabara...then kuzima gari..bhana..halafu tym hizo magari yanapita mengi tu time hizo..acha saundi...

Sasa we Lyamber ngoja kesho jicheleweshe upite pale Saa 8 usiku utajuta! Ahahahaaaaa usiogope mwana!

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
I like stories. I like this story as well. Sijachoka hata kidogo tangu nilipoanza kuisoma. Thanks!!!

Sure, hata mimi hii story imenivutia sana! Stori za kusisimua hivi ndo huwa nazipenda!

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
JINI LA DARAJA LA SALENDA.......EP.12.



Basi shoga niliporudi kidogo moyo ulitulia japo maelezo yote kila nilipoyafikiria mwili ulisisimka. Niliporudi hata bila kupumzika nikakupigia simu. Basi shoga habari ndiyo hiyo tumekamatwa na jini sijui Bakils," Sharifa alimueleza Suzy aliyekuwa ametulia kama sanamu asiamini alichokisikia toka kwa shoga yake.

"Sharifa acha kuligeuza jina lake si umesema anaitwa Balkis."
"Kweli, Balkis."
"Mmh! Mbona kama..."
"Kama nini?"

"Sijaelewa basi inaonekana hata mimi ana yangu mengi juu yangu, kuna muhimu kesho kunipeleka na mimi." Suzy alimueleza shoga yake huku wasiwasi ukiongezeka moyoni mwake kwa kuamini mpenzi wake anaweza kumuacha kwa penzi la ndotoni na jini Balkis alinalotumia dawa ya kuongeza ladha ya mapenzi na yeye kuonekana si mali kitu.

"Sawa tutakwenda."
Waliagana kwa Suzana kurudi nyumbani kwake kutafakari aliyoelezwa na Sharifa, moyo alikuwa na mambo mawili kukubali na kukataa. Akili yake ilikuwa kwenye kukataa na kuamini hakuna vitu kama vile.
sasa endelea...

Tatizo la Brighton kukosa nguvu za kiume lilimnyima raha na kuamua kwenda hospitali kutafuta ufumbuzi wa tatizo ambalo hata yeye hakuelewa limetokana na nini. Alikwenda hadi katika hospitali ya TMJ kwa rafiki yake, baada ya kumuelezea tatizo lake daktari alitaka kumpima ili ajue tatizo ni nini.

Brighton aliingizwa kwenye chumba maalumu na kuvua nguo zote na kubakia na nguo ya ndani, kisha alielelezwa apande kwenye kitanda nilichokuwa mule ndani na kujilaza kusubiri kufanyiwa uchunguzi. Baada ya daktari kuingia chumbani na boksi la gloves kwa ajili ya kumfanyia uchunguzi wa awali. Alichukua gloves ili aanze kufanya uchunguzi hata kabla hajamgusa sauti ilisikika toka nje.
ilimwita:

"Dokta kuna mgonjwa yupo serious sana."
"Sorry Mr Brington, nakuja mara moja," daktari alisema huku akigeuka na akitoka chumbani kumuwahi mgonjwa.

"Hakuna tatizo," Brighton alijibu akiwa bado amejilaza kitandani.
Baada ya muda mchache alishangaa kumuona muuguzi wa kike akiingia chumbani mule bila hodi. Brighton alishtuka kumuona muuguzi wa kike mwenye asili ya kiarabu akiingia bila hodi wakati yeye amelala kitandani na nguo ya ndani tu.

"Wee vipi?" Brighton alishtuka na kutaka kuziwahi nguo zake.
Lakini muuguzi alikuwa ameishawahi kuingia na kumshika kifuani kumrudisha kitandani.
"Brighton hebu tulia."
Kauli ile ilimshtua Brighton na kujiuliza yule muuguzi amejuaje jina lake, lakini bado alitaka kuamka ili achukue nguo zake.

"Brighton mbona unakuwa si muelewa, nimetumwa nije nikusaidie tatizo lako."
Kauli ilimshangaza sana Brighton na kuamua kutulia, lakini hakupenda mwanamke yule aliyeonekana ni muuguzi kumchunguza matatizo yake. Baada ya kutulia yule muuguzi ambaye alikuwa mrembo kupindukia huku akinukia manukato mazuri sana ambayo hakuwahi kuiyasikia alisema:

"Sikiliza Brighton, tatizo lako si la dawa za kizungu, si lilitokea wakati ukifanya mapenzi na mpenzio?"
"Ndiyo," Brighton alikubali huku akijiuliza taarifa zile nani kamwambia.
"Basi nitakupa dawa ya kupaka, wala usikubali dawa za kizungu italala moja kwa moja."

"Hiyo ni dawa gani?"
"Dawa ya asili ya mafuta mazuri," Alisema huku akitoa kichupa kidogo kwenye matiti na kujipaka mkononi, bila kuvaa gloves alitelemsha nguo ya ndani kidogo na kuanza kumchua sehemu za siri. Ilikuwa ajabu sehemu zake zilisimama na kumfanya Brighton azidi kushangaa.

"Sasa hii dawa nitakuachia, kwa vile muda huu natoka, tutaonana siku nyingine. Ila hapa hospital sitakuwepo naacha kazi."
"Kwa nini mrembo?"

"Nimeamua tu."
"Nikitaka kukuona?"
"Si rahisi, la muhimu umepona kampe raha wifi?"
"Umeolewa?"
"Ukitaka mazungumzo mengi utanikuta nje, sasa hivi vaa nguo zako akija daktari mwambie umekwishapona na usikubali kumjibu zaidi ya kuondoka."

Baada ya kusema vile yule muuguzi mrembo alitoka na kumuacha Brington akivaa nguo. Akiwa anamaliza kuvaa viatu daktari aliingia na kumkuta anataka kuondoka.

"Vipi best, mbona unataka kuondoka, samahani nimechelewa hata mgonjwa mwenyewe nimemuona?"
"Una maana gani?"
"Hata hao wauguzi nawaelewa wanasema alikuja dada mmoja wa Kiarabu, alipofika katikati ya korido alidondoka na kuanza kutoa povu, ndipo waliponifuta ili nikampe msaada wa haraka. Lakini ajabu mgonjwa mwenyewe sikumkuta."

"Sasa kaenda wapi?"
"Hata wanajua."
"Labda kapata nafuu kaondoka."
"Si rahisi kwa hali aliyokuwa nayo si rahisi kuondoka."

"Mmh! Sasa atakuwa amekwenda wapi?"
"Hata najua, hebu tuendelee na matibabu yetu."
"Nimepona," Brighton alijibu kwa mkato.

"Mr Brighton najua nimekuchelewesha, samahani sana hebu rudi nikufanyie uchunguzi."
"Mr Paul nipo sawa."
"Si kweli, najua umekasirika."

"Sijakasirika Mr nipo sawa, nimeshangaa kujiona nipo sawa nikiwa nimelala kitandani, kama itarudia nitakueleza."
"Heri tungejua tatizo ili lisije likarudia tena."
"Halitatokea tena."

"Si kweli najua umekasirika."
"Niamini Mr Paul wewe ni rafiki yangu wa muda mrefu, kwani umetumia muda gani wa kunifanya nikasirike. Na kwa nini nikasirike wakati ulikimbilia kuokoa maisha ya mtu."
"Kama hujakasirika sawa."

Brighton aliagana na Dokta Paulo na kutoka nje ya hospitali, alipofika nje aliingia kwenye gari lake na kuamua kurudi nyumbani. Ili kuiamini dawa yake kabla ya kuondoka alimpigia simu mpenzi wake Suzana.

"Mpenzi naomba leo uje nyumbani nina imani tiba ya tatizo langu imepatikana."
"Tiba ya nini?"
"Kwani nasumbuliwa na nini?"
"Lile tatizo la kitandani?"

Ni kweli Brighton amepona? Yule aliyempa dawa ni muuguzi kweli?








JINI LA DARAJA LA SALENDA........EP.13


Hilo hilo."
"Brighton hebu acha utani."
"Kweli mpenzi wangu, huwezi kuamini ugonjwa ulivyopona."
"Au ulikwenda kwa Babu?"

"Walaa, tukikutana nitakueleza maajabu yaliyonitokea, ilikuwa kama bahati ya mtende."
"Basi leo mtoto hatumwi dukani nina usongo na wewe ile mbaya."

Baada ya Suzana kukata simu alijikuta akizidi kuchanganyikiwa na maelezo ya mganga kuhusu mpenzi wake na taarifa za kupona kwake. Alijikuta akianza kuamini maneno ya mama Sharifa kuwa waganga wengi ni waongo, kazi yao kuwatisha wagonjwa ili wapewe pesa nyingi.

Alijikuta akifuta wazo la kwenda kwa mganga ili na yeye akaangaliziwe mambo yake. Aliona kuna uongo mkubwa kati ya maneno ya mganga na mpenzi wake, alipoambiwa kuwa mpenzi wake hamhitaji tena kwa vile anafanya mapenzi na jini Balkis kwenye ndoto.

Ujumbe wa mpenzi wake kumhitaji kimapenzi ulidhihirisha jinsi mganga alivyowadanganya. Aliona kwenda kwa mganga ni kupoteza muda na kumpa pesa za bure. Muda ule ule alimpigia simu Sharifa kuahirisha safari ya kwenda kwa mganga.

"Shoga, kesho safari ya kwa mganga imekufa."
"Vipi shoga, mbona hivyo?"
"Aah! Basi tu, tutakwenda siku nyingine."
"Mmh! Sawa."

Wakati Suzana akiahirisha kwenda kwa mganga kuangalia matatizo yake, Brighton baada ya kutoka ndani ya hospitali alipepesa macho labda atamuona muuguzi aliyemtibu. Lakini hakumuona, alitaka kwenda kumuuliza ndani ya hospitali, lakini alikumbuka kauli ya yule muuguzi ambaye hata jina lake hakulijua, alimkataza asimuulize mtu yeyote habari zake.

Aliingia ndani ya gari yake na kuondoka huku akiwa na shauku ya kumuona yule dada mrembo mwenye roho ya huruma. Mpaka anaondoka eneo la hospitali hakumuona. Alijikuta akiwa na shauku ya kumuona yule mrembo ambaye alisema mengi wangezungumza nje ya hospitali.

Alipokaribia maeneo ya Makumbusho alishtuka kumuona yule dada akiwa katika vazi refu zuri lenye mvuto, lililoongeza uzuri wake akilipungia mkono gari lake. Alilisimamisha mbele yake kidogo, yule mwanamke mrembo alisogea hadi kwenye gari na kufungua kisha aliingia ndani na kukaa kwenye siti.

Baada ya kukaa na kufunga mlango wa gari, Brighton aliondoa gari bila kujua mrembo anaelekea wapi. Baada ya mwendo mfupi aliitwa jina lake.
"Brighton."
"Naam."

"Za muda?"
"Nzuri."
"Unaelekea wapi?"
"Nilikuwa narudi nyumbani, lakini nitakusikiliza wewe unakwenda wapi."
"Umeoa?"

"Bado."
"Na Suzana?"
"Suzana! Umemjuaje?"
"Jibu swali," yule mwanamke alisema huku akimuangalia jicho lililolegea.
"Ni mchumba wangu, si mke wangu."
"Ina maana ukipata mtu mwingine utakuwa tayari kumuoa na kumuacha Suzy?"
"Itategemea."

"Itategemea nini, wakati tayari Suzana ni mchumba wako?"
"Itategemea uwezo wake katika ufahamu wa maisha, Suzana mchumba wangu pamoja na kunipenda, tatizo lake anapenda sana starehe. Kwangu namuona kama si mwanamke anayefaa kuwa mke wangu."

"Kwa mfano mimi nikitaka unioe itakuwaje?"
"Mmh! Nitakuweza?"
"Kivipi?"

"Unaonekana unatoka katika familia ya watu wenye uwezo."
"Familia yangu ingekuwa na uwezo ningefanya kazi pale hospitali?"
"Hata mimi nashangaa."

"Niambie kweli kama utakuwa tayari kunioa niwe mkeo, kila kitu nitashughulikia mimi, nakuahidi kuyabadili maisha yako."
"Mmh! Nipe muda."
"Brighton sina muda mwingine zaidi ya huu."

"Nimekubali."
"Kama umekubali naomba leo nikalale kwako."
"Mmh! Kwa nini tusifanye siku nyingine?"
"Au kwa vile umemwita Suzana?"
"Umejuaje?" Brighton alishtuka tena.

"Brighton, nimekueleza sitaki maswali ninapokuuliza swali nataka jibu."
"Ni kweli, leo nilimualika aje tulale pamoja."
"Tatizo nini?"
"Sasa itakuwaje wewe uwepo na yeye aje?"

"Wee mwache aje alale, mimi nitalala chumba kingine."
"Si atakuona?"
"Hawezi kuniona, labda umwambie wewe."
"Kwa hiyo utaingia nyumbani saa ngapi?"

"Muda wowote, usiwe na wasiwasi."
Brighton alielekea nyumbani kwake akiwa na wasiwasi wa kugonganisha wanawake.

Brighton anakutana na mtihani mzito wa kuvunja uchumba wake na Suzy, Suzy atakubali kirahisi kumpoteza mpenzi wake?
Etaendelea wakati ujao .......................

 
Aaaaaaaaa, na wewe MziziMkavu vipi? Mbona unatukatisha raha? Funguka mazima bhana!

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
khaaaaaaaaa.........................story inasisimua flani hivi.....halafu.........mhhh...anyway ngoja iishe then ntakuja na maswali yangu. MziziMkavu tiririsha basiiii.............
 
Last edited by a moderator:
Jini la daraja la salenda -14

ILIPOISHIA:
“Kama umekubali naomba leo nikalale kwako.”
“Mmh! Kwa nini tusifanye siku nyingine?”
“Au kwa vile umemwita Suzana?”
“Umejuaje?” Brighton alishtuka tena.

“Brighton, nimekueleza sitaki maswali ninapokuuliza swali nataka jibu.”
“Ni kweli, leo nilimwalika aje tulale pamoja.”
“Tatizo nini?”
“Sasa itakuwaje wewe uwepo na yeye aje?”
“Wee mwache aje alale mimi nitalala chumba kingine.”

“Si atakuona?”
“Hawezi kuniona, labda umwambie wewe.”
“Kwa hiyo tuingia nyumbani saa ngapi?”
“Muda wowote, usiwe na wasiwasi.”
Brighton alielekea nyumbani kwake akiwa na wasiwasi wa kugonganisha wanawake. SASA ENDELEA...

****
Walipofika nyumbani yule mwanamke aligundua wasiwasi wa Brighton, alimgeukia na kumuuliza:
“Mbona una wasiwasi?”
“Bado siamini kama Suzana akija hawezi kukuona, kwa nini nisimzuie asije?”
“Hapana Brighton, kwa vile umemuita, mwache aje tu.”
“Anaweza kuja chumba utachokuwemo itakuwaje?”
“Naomba uwe mwelewa, wee mwache aje na mimi hawezi kuniona.”

“Mmh! Sawa.”
Brighton alikubali kwa shingo upande, lakini moyoni alikuwa na kiburi cha ajabu, kama Suzana atamuona mgeni wake, atakuwa tayari kwa atakachokiamua.
“Brighton bafu lipo wapi?” Mgeni aliuliza.
“Lipo ndani ya chumba cha kulala.”
“Naomba nikaoge.”

“Ruksa.”
Mwanamke mrembo alielekea chumbani ili aende bafuni kuoga, kila hatua aliyopiga kuelekea chumbani ilimchanganya sana Brighton, alijiuliza imekuwaje mwanamke mzuri kama yule kumpenda yeye kwa haraka. Katika maisha yake aliwahi kuona wanawake wazuri lakini yule alikuwa ni zaidi.
Baada ya mgeni kuingia chumbani, wazo la haraka kwa Brighton lilikuwa kumpigia simu Suzana kumzuia asije. Ili mgeni asisikie alitoka nje lakini ilikuwa ajabu simu ya Suzana haikupatikana, kitu kilichozidi kumweka kwenye wakati mgumu wa kuweza kumzuia asifike nyumbani kwake.

Akiwa bado anatafakari jinsi ya kutatua tatizo lile, sauti ndani ilimwita.
“Mpenzi upo wapi?”
“Nipo nje.”
“Njoo basi.”

Brighton aliingia ndani huku akijitahidi kuficha hofu yake, picha aliyoiona mbele yake ilimfanya afikiche macho kujiuliza anachokiona ni kweli au yupo ndotoni. Mbele yake alikuwa amesimama mwanamke mrembo ajabu akiwa amejifunga mtandio mwepesi sehemu ya makalio na kifuani. Sehemu nyingine ya mwili wake ilikuwa wazi. Lilikuwa umbile lenye kumtia msisimko mwanaume yeyote rijali. Alijikuta akipigwa na butwaa kama ameona meli ikitembea barabarani.
“Mbona unanishangaa?” Mgeni alimuuliza.
“Lazima niseme ukweli, wewe ni mwanamke mzuri sana.”

“Asante, hata wewe ni mwanaume mzuri sana.”
“Nashukuru.”
“Brighton mbona unajiweka roho juu, hebu mwache Suzana aje.”
“Umejuaje?” Brighton alishtuka kusikia vile.
“Unaniuliza nimejuaje, ina maana ninachosema ulifanya siri?”
“Hapana, sipendi litokee tatizo lolote, unaweza kuniona sina maana.”
“Aliyekueleza umruhusu Suzana aje nani?”

“Wewe.”
“Sasa tatizo nini, nimekueleza mwache aje kwani chumba nitakachokuwa hawezi kuingia.”
“Wewe unajiamini nini?”
“Utajua baadaye sasa hivi ni haraka, mimi si mkeo mtarajiwa?”
“Ndiyo.”
“Kipi kimekufanya ukubali niwe mkeo?”

“Hata sielewi lakini kitendo chako cha kujitolea kunitibu bila gharama ugonjwa ambao ulinisumbua sana, imeonesha jinsi gani ulivyo muhimu sana kwangu.”
“Kingine?”
“Nimetokea kukupenda na kila dakika mapenzi yangu kwako yanazidi kuongezeka.”
“Nashukuru kusikia hivyo, nina imani kuna vitu umehisi kuvikuta kwenye mwili wangu, basi nakuhakikishia kukufurahisha katika maisha yangu yote.”
“Nitashukuru.”
“Brighton nipo chumbani, Suzana amekaribia kufika.”

“Umejuaje?”
“Brighton mbona kila ninachokizungumza kwako kinakushangaza?”
“Unanishangaza kuzungumza vitu ambavyo kwa mtu yeyote ni vigumu kuvijua.”
“Brighton najua una hamu kunifahamu kwa undani, hata jina langu hulijui?”
“Ni kweli, hebu niambie jina lako unaitwa nani?”
“Sasa mbona mpaka nimekueleza mimi au hukupenda kulijua jina langu?”
“Huwezi kuamini, jinsi nilivyopagawa kukupata, hata kuuliza jina niliona kazi, najiona kiumbe mwenye bahati ya mtende.”

“ Naitwa Balkis Bakilas, naomba nikuache Suzana anaingia sasa hivi, nakusihi usioneshe wasiwasi wowote.”
“Umejuaje?’
“Kuwa mwelewa,” baada ya kusema vile aligeuka na kuelekea chumba cha wageni.
Kila hatua aliyopiga kuelekea chumbani huku akimuachia Brighton sehemu za nyuma ambazo ziliumbwa kwa mpangilio. Alijikuta akimeza mate huku akimsindikiza kwa macho. Hata alivyoingia mpenzi wake Suzana hakumuona, alishtuka alipoulizwa swali.

“Brighton mbona umeshangalia huko hadi naingia wewe huna habari, kuna nini?”
Suzana aliuliza huku macho yake yakiangalia alipoelekea Balkis.
“Aa..aah,” Brighton alibabaika kujibu.
“Brighton kuna nini?”
“Ha..ha..kuna kitu.”

“Au ulifikiri siwezi kuja?” Suzana alisema huku akimbusu na kukaa pembeni yake.
“Wala.”
“Mbona kama haupo sawa?”
“Nipo sawa.”
“Nakuja.”

Suzana alisema huku akinyanyuka na kuelekea chumba alichoingia Balkis, Brighton alijikuta akipatwa na mshtuko, wasiwasi wake ulikuwa huenda Suzana alimuona akiingia hivyo alikwenda kumfumania. Alitaka kumkataza lakini mdomo ulikuwa mzito.

JINI LA DARAJA LA SALENDA-15

ILIPOISHIA RISASI JUMATANO:
Alipiga hatua kuelekea chumbani huku akimtingishia Brighton sehemu za nyuma ambazo ziliumbwa kwa mpangilio. Brighton alijikuta akimeza mate huku akimsindikiza kwa macho. Hata alivyoingia mpenzi wake Suzana hakumuona, alishtuka alipoulizwa swali.

“Brighton mbona umeshangaa huko, hata naingia huna habari, kuna nini?”
Suzana aliuliza huku macho yake yakiangalia alipoelekea Balkis.
“Aa...aah,” Brighton alibabaika kujibu.
“Brighton kuna nini?”
“Ha..ha..kuna kitu.”

“Au ulifikiri siwezi kuja?” Suzana alisema huku akimbusu na kukaa pembeni yake.
“Wala.”
“Mbona kama haupo sawa?”
“Nipo sawa.”
“Nakuja.”
Suzana alisema huku akinyanyuka na kuelekea chumba alichoingia Balkis, Brighton alijikuta akipatwa na mshtuko, wasiwasi wake ulikuwa huenda Suzana alimuona akiingia hivyo alikwenda kufumania. Alitaka kumkataza lakini mdomo ulikuwa mzito.
SASA ENDELEA...

Suzana alikwenda hadi mlango wa chumba cha wageni na kuingia ndani, Brighton mapigo ya moyo yalikuwa makubwa. Alijisogeza hadi kwenye kochi na kujilaza akiwa ameshikilia mkono mmoja kifuani kuizuia presha kutokana na vurugu itakayotokea chumbani.

Siku zote Suzana alimhakikishia Brighton kuwa siku atakayomkuta na mwanamke ndiyo siku atakielewa kichaa chake. Akili nyingine ilimtuma awahi chumbani kabla Suzana hajafanya lolote. Alinyanyuka alipokuwa amejilaza na kwenda chumba cha wageni.

Alipofika alifungua mlango na kuingia ndani, Suzana aliyekuwa akianua nguo yake ya ndani, alishtuka na kumuuliza:
“Vipi mbona umeingia kama unafukuzwa?”

“Aa..aa..,” alijibu kwa kubabaika huku akipepesa macho chumbani kumtafuta Balkis.
“Vipi mbona unatembeza macho chumba kizima kuna nini?” Suzana alimuuliza.
“Walaa, niliweka CD yangu kwenye meza.”
“Sasa ulivyokuja hivyo, umeniona mimi mwizi?”
“Walaaa, nilikuwa najiuliza niliiweka huku au wapi?”
“Brighton, umeanza lini kuweka vitu vyako humu chumbani?”

“Suzana hii ni nyumba yangu, nina uhuru wa kuweka kitu popote.”
“Mbona leo Brighton sikuelewi?”
“Kivipi?”
“Umekuwa mtu mwenye mawazo mengi pia mwenye hasira tofauti na siku zote.”
“Nipo sawa.”
Brighton bado hakuamini kama kweli chumbani hakuna mtu, wasiwasi wake huenda amekwenda choo cha wote kilichokuwa upande wa mwisho wa nyumba ile. Bila kuongeza neno alitoka na kwenda moja kwa moja msalani ili kumuwahi kama Balkis yuko huko asitoke.

Alipofika msalani hakukuta kitu, alijikuta akibaki akilishangaa bafu huku akijiuliza Balkis amekwenda wapi, ikiwa hakuna mlango mwingine wa kutokea. Akiwa bado ameshangaa Suzana alisimama tena nyuma yake na kumuuliza:
“Brighton upo sawa?”
“Nipo sawa.”

“Hapana, kuna kitu kinakusumbua hutaki kuniambia.”
“Suzy, nipo sawa.”
“Hapana Brighton una tatizo unanificha, mimi nani kwako?”
“Mpenzi wangu.”
“Nani wa kumueleza shida zako?”
“Lakini Suzy mimi sina tatizo lolote,” Brighton aliendelea kujitetea japo maji yalikuwa shingoni.

“Sikubali, kuna kitu unanificha, basi mimi nipo chumbani ukimaliza matatizo yako utanikuta.”
Suzana alisema huku akielekea chumba cha kulala, baada ya kuondoka Brighton aliendelea kuelea kwenye bahari ya mawazo juu ya kitu kilichotokea muda mfupi pale alipomshuhudia Balkis akiingia chumba cha wageni na wakati huo Suzana alikuwa anaingia. Bila kupumzika, alikwenda moja kwa moja chumba cha wageni alichoingia Balkis.

Lakini cha ajabu, Balkis hakuwepo chumbani wala msalani, alijiuliza atakuwa wapi? Alijikuta akirudi tena chumba cha wageni kupata uhakika kama kweli Balkis hayumo. Chumba cha wageni hakikuwa na vitu vingi vya kuweza mtu kujificha, kitanda na tivii ndogo. Alipofungua mlango na kuingia, alishtuka kidogo akimbie alipomkuta Balkis akiwa amejilaza kitandani akiwa amepitiwa na usingizi. Kwake aliona kama maruweruwe, alifikicha macho kutaka kupata uhakika wa kile alichokiona mbele yake.

Akiwa bado kapigwa na butwaa, Balkis aligeuka na kufumbua macho, alipomuona Brighton aliachia tabasamu na kusema:
“Mpenzi mbona umeingia bila hodi?”
“Aah! Ulikuwepo?”
“Kuwepo wapi?”
“Chumbani.”
“Chumba gani?”

“Si humu ndani.”
“Ndani wapi?”
“Sijakuelewa, hebu nieleweshe vizuri, nilikuwa wapi kivipi?”
“Muda mfupi ulikuwa wapi?”
“Brighton, swali gani hilo? Nimekuaga nakuja chumbani na umekuja umenikuta, sasa unaniuliza swali gani hilo?”
“Mbona nimekuja chumbani sikukukuta?”

“Hukunikuta! Hapa unazungumza na nani?”
“Suzana alikuja huku, kwa wasiwasi wa kukuona ilibidi nije ili isitokee vurugu lakini sikukuona.”
“Sijui unamaanisha nini, hebu nenda kwa Suzana ukamuondoe wasiwasi, nimekueleza mapema acha kujitia jakamoyo.”

“Umejuaje?”
“Ukirudi nitakuambia, muwahi mchumba wako.”
Brighton alitoka kwenda chumbani kwake na kumuacha Balkis akimsindikiza kwa macho.
Ni kweli Suzana alimuona Balkis? Mbona hakuonekana mwanzo chumbani? Kuyajua yote, tukutane baadae
 
bibie Paloma Ni ndefu sana haiwezi kuisha leo bibie....................

basi wacha nikatafakari kabla ya kuja na makwesheni yangu manake huenda ikawa majibu yapo lakini sikuyaona nikabaki kuzogoa tu.................ila kwa wapenda story ni story inasisimua....tamu kuisoma, ina nata akilini, na inayojenga maswali kadha wa kadha!
 
Ha ha ha ha hadithi za majini!! Du huko nyuma zilitawala maeneo mengi utasikia pale kuna mdudu/jini? Ila ni imani ambazo huwa zipo kwa baadhi ya maeneo!! Tusikatae ukweli wa haya mambo!! Sema siku zinaposonga wanaofuga haya majini wanakufa na wanashindwa kuendelezwa au wengine wanaoachiwa wanakosea sheria na taratibu za kuishi nao na wanaondoka either wenyewe bila any harm au kwa harm kulingana na masharti yake!! Msiseme Zogwale ni mtoto wa Shekhe Yahaya mtabiri wa Nyumba Nyeupe!!
 
Illucinations may be due to use substances like alcohol, canabis,hashish cocanine etc.. It also occurs in case of schizophrenia.
 
basi wacha nikatafakari kabla ya kuja na makwesheni yangu manake huenda ikawa majibu yapo lakini sikuyaona nikabaki kuzogoa tu.................ila kwa wapenda story ni story inasisimua....tamu kuisoma, ina nata akilini, na inayojenga maswali kadha wa kadha!
Ingawa hadithi bado haijakwisha lakini unaweza kutafakari bibie Paloma
 
Last edited by a moderator:
[h=1]Jini la daraja la salenda -16[/h]ILIPOISHIA;
Akiwa bado kapigwa na butwaa, Balkis aligeuka na kufumbua macho yake, alipomuona Brighton aliachia tabasamu na kusema:
"Mpenzi mbona umeingia bila hodi?"
"Aah! Ulikuwepo?"
"Kuwepo wapi?"

"Chumbani."
"Chumba gani?"
"Si humu ndani."
"Ndani wapi?"
"Sijakuelewa, hebu nieleweshe vizuri, nilikuwa wapi kivipi?"
"Muda mfupi ulikuwa wapi?"

"Brighton, swali gani hilo? Nimekuaga nakuja chumbani na umekuja umenikuta, sasa unaniuliza swali gani hilo?"
"Mbona nimekuja chumbani sikukuta?"
"Hukunikuta! Hapa unazungumza na nani?"
"Suzana alikuja huku, kwa wasiwasi wa kukuona ilibidi nije ili isitokee vurugu lakini sikukuona."

"Sijui una maanisha nini, hebu nenda kwa Suzana ukamuondoe wasiwasi, nimekueleza mapema acha kujitia jaka moyo."
"Umejuaje?"
"Ukirudi nitakuambia, muwahi mchumba wako."
Brighton alitoka kwenda chumbani kwake na kumuacha Balkis akimsindikiza kwa macho. SASA ENDELEA...

Brighton alijitahidi kurudi katika hali yake ya kawaida kabla ya kuingia chumbani. Alipoingia alimkuta Suzana amekaa upenuni mwa kitanda akiwa ameshika tama.
"Suzana mpenzi wangu vipi?"
"Vipi nikuulize wewe?"
"Mbona mimi nipo sawa, hebu twende tukaoge mpenzi wangu tuje tulale."

Alimshika mkono na kumnyanyua kisha waliongozana naye bafuni, baada ya kuoga walirudi kitandani. Kwa vile Suzana alikuwa na hamu na mpenzi wake, baada ya kuikosa huduma ya kitandani kwa muda mrefu. Brighton hakujiamini kwa asilimia miamoja kukifanya alichomuitia mpenzi wake.

Lakini ilikuwa kama alivyoelezwa na Balkis kuwa dawa aliyompa inafanya kazi, Suzana aliweza kufurahia mapenzi kwa muda wote, Brighton alijikuta akijisahau kuwa Balkis naye anamhitaji, baada ya kumstarehesha mpenzi wake alipitiwa na usingizi mzito.
Ulipofika usiku wa manane Brighton alishtuka usingizini na kujikuta akifanya mapenzi na Balkis tena chumbani kwake. Baada ya penzi tamu la Balkis ambao aliamini hakuwahi kupewa chini ya jua zaidi ya ndotoni. Alipepesa macho mule chumbani labda atamuona Suzana lakini hakumuona.

Ili kupata uhakika Suzana yupo wapi alimuaga Balkis kwenda msalani, pamoja na kuwa na choo cha chumbani lakini alitoka kwenda cha watu wote. Ajabu Balkis hakumuuliza chochote, alitoka mpaka chumba cha wageni na kukikuta kitupu. Alikwenda hadi msalani pia hakumuona.
Alijiuliza Suzana atakuwa wapi au ameondoka, lakini haikuwahi kutokea Suzana aondoke usiku tena bila kuaga. Alijikuta akijiuliza bila kupata majibu kuwa yupo ndotoni au kweli, alitoka hadi nje ya nyumba lakini hakukuwa na dalili zozote za kuwepo Suzana.

Alimfuata mlinzi wa Kimasai na kumuuliza kama Suzana ametoka.
"Rafiki shemeji yako ametoka?"
"Sijaona yeye ikitoka, niliiona inaingia tu."
"Rafiki lazima ulilala, mbona ndani hayupo?"
"Sijasinzia rafiki, shemeji haijatoka imo ndani."
"Kweli?"

"Kweli kabisa rafiki."
Brighton aliamini kabisa mlinzi alipitiwa usingizi wakati Suzana anatoka, akiwa bado anajiuliza ni kweli Suzana alikuja au ilikuwa ndoto. Lakini akili yake ilimweleza kuwa Suzana alikuja kweli wala haikuwa ndoto na kufanya naye mapenzi na kila mmoja alipitiwa na usingizi mzito.

Lakini aliposhtuka na kujikuta akifanya mapenzi na Balkis tena penzi tamu adhimu, bado alikuwa njia panda kujiuliza kilichotokea ni nini yupo ndotoni au ni kweli. Kwa maelezo ya mlinzi kuwa kweli alimuona anaingia lakini hakumuona anatoka ilizidi kumchanganya.

Hata kama kweli alitoka bado asingeondoka bila kuaga, na kitu kile hakikuwahi kutokea toka waanze uhusiano wao. Akiwa bado yupo njia panda kwa kile alichokuwa akikiwaza juu ya kuyeyuka kwa mpenzi wake . Sauti ya Balkis alimtoa kwenye dimbwi la mawazo.
"Brighton huku ndiko msalani?"
"Aa..aah... nilikuwa napunga upepo."

"Imeanza lini na leo iwe ya pili?"
"Ni kawaida yangu wala si leo."
"Kweli?"
"Kweli kabisa."
"Kwa hiyo nikuache uendelee kupunga upepo?"
"Hapana, wacha turudi ndani."

Brighton alirudi ndani na Balkis, walipofika kitandani bado alikuwa na mawazo, lakini hakutaka kuumia kichwa alimuuliza Balkis.
"Eti Suzana wakati anaondoka ulimuona?"
"Swali gani hilo Brighton?"
"Ooh! Basi."

"Kwanini unaniuliza habari za mpenzi wako mimi zinanihusu mimi?" Balkis alimuuliza kwa sauti kali kidogo.
"Hapana mpenzi, inawezekana ulikuwa ninaota."
"Kuota nini?"

"Kuwa Suzana alikuja leo."
"Kama alikuja yupo wapi?"
"Inawezekana nilikuwa naota."
"Kama ulikuwa unaota basi tulale," Balkis alimkumbatia Brighton, hakuchelewa usingizi mzito ulimpitia.

****
Suzana aliposhituka usingizini hakuamini macho yake alipojikuta yupo nyumbani kwake amelala kitandani. Alirudia kutazama tena ni kweli au alikuwa akiota, akili yake ilimjulisha kuwa jana alipigiwa simu na mpenzi wake Brighton kuwa amepata dawa ya matatizo ya nguvu za kiume na alipokwenda kweli alikuwa amepona.

Alikumbuka Brighton alimpa penzi tamu na kujikuta wote wakipitiwa usingizi, lakini ilikuwa ajabu kuamka asubuhi na kujikuta amelala kitandani kwake. Alijiuliza simu aliyopigiwa alikuwa anaota au kweli, kila alipolazimisha labda ni ndoto akili ilikataa na kuamini kabisa alikwenda kwa Brighton.

Alijiuliza labda baada ya kufanya mapenzi alirudishwa nyumbani, lakini kwa upande wake kitu kama kile hakikuwahi kutokea. Kingine kilichomshangaza hata kama alirudishwa akiwa amelala hakuwa na fahamu. Alikaa kitandani kwa muda na kukumbuka anatakiwa kujiandaa kwenda kazini.
Aliamka na kwenda kujiandaa, alipofika kazini bado akili yake haikumpa alimtafuta Sharifa amueleze kilichomtokea.

Suzana na Brighton kilichowatokea watakigundua? Wakikigundua watachukua hatua gani? Balkis atatimiza dhamira yake?

[h=1]JINI LA DARAJA LA SALENDA-17[/h]
ILIPOISHIA:
Suzana aliposhtuka usingizini hakuamini macho yake alipojikuta yupo nyumbani kwake amelala kitandani. Alirudia kutazama tena ni kweli au alikuwa akiota, akili yake ilimjulisha kuwa jana alipigiwa simu na mpenzi wake Brighton kuwa amepata dawa ya matatizo ya nguvu za kiume na alipokwenda kweli alikuwa amepona.

Alikumbuka Brighton alimpa penzi tamu na kujikuta wote wakipitiwa na usingizi, lakini ilikuwa ajabu kuamka asubuhi na kujikuta amelala kitandani kwake. Alijiuliza simu aliyopigiwa alikuwa anaota au kweli, kila alipolazimisha labda ni ndoto akili ilikataa na kuamini kabisa alikwenda kwa Brighton.

Alijiuliza labda baada ya kufanya mapenzi alirudishwa nyumbani, lakini kwa upande wake kitu kama kile hakikuwahi kutokea. Kingine kilichomshangaza hata kama alirudishwa ni kuwa alikuwa amepoteza fahamu. Alikaa kitandani kwa muda na kukumbuka anatakiwa kujiandaa kwenda kazini.

Aliamka na kwenda kujiandaa, alipofika kazini bado akili yake haikumpa jibu. Alimtafuta Sharifa amueleze kilichomtokea jana.
SASA ENDELEA ...

Alipofika alimkuta ndiyo kwanza anafuta vumbi kwenye kompyuta yake, Sharifa alipomuona Suzana aligundua ana matatizo.
"Karibu shoga."

"Asante," alijibu huku akisogeza kiti na kuketi.
"Mbona uko hivyo?"
"Mmh! Kuna kitu kimenitokea jana sikielewi hata kidogo!"
"Kitu gani hicho?"
"Unakumbuka jana nilikupigia simu?"
"Ndiyo."

"Nikakueleza kuwa nimeahirisha kwenda kwa mganga?"
"Ndiyo."
"Basi, Brighton si aliniita na kunieleza kuwa amepata dawa ya tatizo lake na kukosa nguvu za kiume."
"Ehe?"

"Baada ya kunieleza vile nikaona hakuna sababu yoyote ya kwenda kwa mganga kwa vile dawa imepatikana."
"Ehe!"
"Basi jana saa moja usiku nikaenda kwa mpenzi wangu."
"Lete raha dada."
"Tumekutana kama kawaida, baada ya kuoga tulipanda kitandani, si unajua usongo niliokuwa nao."

"Najua sana."
"Basi shoga, kama alivyonieleza ndivyo ilivyokuwa, mtoto wa kike nikajilia raha nilizozipoteza muda mrefu."
"Alikuwa na nguvu kama kawaida?"
"Tena ziliongezeka mara mbili."

"Mmh! Makubwa, kampata mganga gani huyo?"
"Anasema alikwenda hospitali."
"Jamani ona sasa, kumbe tunakimbilia kwa waganga tiba ipo hospitali, nilikueleza toka awali waganga wengine wanatengeneza ugonjwa, ionekane kweli tuna matatizo makubwa ili tuwape fedha nyingi."
"Shoga bado nakuja sijafika kwenye pointi yangu."
"Ipi tena?"

"Sababu iliyonifanya nisiingie ofisini kwangu na kuja moja kwa moja kwako."
"Una tatizo gani?"
"Tulipomaliza kufurahishana na mpenzi wangu huku nikifurahia mafanikio makubwa baada ya kupona tatizo lake, tulipitiwa na usingizi mzito. Lakini kwa maajabu makubwa nimeamka asubuhi na kujikuta nipo kwangu!"
"Kujikuta kwako kivipi?"

"Kitandani kwangu nimelala!"
"Sasa kipi cha ajabu?"
"Ina maana hujanielewa?"
"Nimekuelewa! Yaani jana baada ya kukutana na mpenzi wako asubuhi ulipoamka ulijikuta umelala, sasa kipi cha ajabu kama ulilala usiku na asubuhi ukajikuta kitandani?"

"Hebu nielewe vizuri nisemayo, jana nilikwenda kwa Brighton kama ilivyo kawaida, ninapokwenda hulala huko huko, hata safari yangu ya kuja kazini huianzia kwake."
"Hilo nalijua, sasa hapo tatizo nini?"
"Jamani huoni tatizo! Nilale kwa Brighton niamke kwenye kitanda nyumbani kwangu tena nikiwa peke yangu."

"Suzana! Unayosema ni kweli au ulikuwa unaota?"
"Sharifa, yaani niote mchana na usiku? Sikukupigia simu?"
"Ulinipigia?"
"Saa ngapi?"

"Mchana"
"Sasa huko kuota gani?"
"Mmh! Basi kama ni kweli usemayo kuna namna lazima tuliangalie kwa macho mawili."
"Yaani toka nimeamka sijielewi kabisa."
"Umempigia simu Brighton kumuuliza?"

"Huwezi amini kila nikipiga simu yake inaonekana anazungumza."
"Basi kuna umuhimu wa wewe kwenda kwake ili ukapate ukweli, japo mimi bado naamini baada ya kunipigia simu inawezekana kabisa ulipitiwa na usingizi na kuota ulikuwa na Brighton na asubuhi ulipoamka ukajishangaa upo kitandani kwako. Lazima utaamini kabisa umetokewa na kitu kisicho cha kawaida."

"Sharifa hiki ninachokueleza ni kweli kabisa si cha kuota, haya ni maajabu."
"Au ndiyo Jini Balkis?"
"Jini Balkis! Kama ni Balkis, Brighton asingeweza kufanya kazi."
"Nimekueleza yule jini ana mambo mengi ya kukuchanganya pale unapokaribia kuujua ukweli."
Suzana anaanza kuingia kwenye mtihani mzito wa Jini Balkis, nini hatima ya yote? Kuyajua yote tukutane baadae leo jioni............
 
Pooowa night imeenda vizuri kwa kusoma hadithi hii na kesho tena mzizi mkavu
 
Back
Top Bottom