Setfree
JF-Expert Member
- Dec 25, 2024
- 5,527
- 7,121
Wanaofanya mazingaombwe huwa wanadai kwamba, maonesho yao yanatokana na ujanja na maarifa fulani ya hali ya juu. Hata hivyo, Mtumishi mmoja wa Mungu, amethibitisha wazi kuwa baadhi ya mazingaombwe huwa yanafanywa kwa kutumia nguvu za giza!
Siku moja Mtumishi huyo alipita mahali akakuta mwana mazingaombwe anafanya "show" zake. Kulikuwa na kikundi kikubwa cha watu wanatazama. Mtumishi huyo, alisimama katikati ya watazamaji wengine, kisha kimya kimya, bila kutamka maneno, akakemea "show" hizo zisifanyike. Mwana mazingaombwe, alijaribu kutumia mbinu na maarifa yake yote, lakini hakuweza tena kufanya yale aliyotamba kwamba atayafanya. Baadaye akasema: "hapa kuna mtu anazuia mazingaombwe yangu yasifanyike!" Lakini hakuweza kujua ni nani.
Mtumishi huyo akathibitisha kuwa ni kweli baadhi ya mazingaombwe huwa yanafanywa kwa kutumia nguvu za giza au uchawi, ndio sababu mwana mazingaombwe huyo hakuweza kuendelea na "show" zake, mara tu Mtumishi huyo wa Mungu alipoyakemea kwa Jina la Yesu.
Hakika Jina la Yesu ni Jina lipitalo majina yote. Likitamkwa kwa sauti ndogo au kubwa au kimoyo moyo na mtu aaminiye kuwa Jina la Yesu lina nguvu, kazi za shetani zinavunjika, mapepo yanatoroka na shetani mwenyewe anakimbia. Anza leo kulitumia Jina la Yesu ku-solve matatizo unayokutana nayo maishani mwako. Wachawi wakija kwako, wakemee kwa Jina Yesu watakimbia. Watu wakikutishia kwamba wataloga biashara yako, zuia mipango yao kwa Jina la Yesu. Ukiona ndoa yako imeingiliwa na mapepo yanayosababisha unafarakana na mwenzi wako wa ndoa, kemea mapepo hayo, utaona chuki na mafarakano vinaisha!
Siku moja Mtumishi huyo alipita mahali akakuta mwana mazingaombwe anafanya "show" zake. Kulikuwa na kikundi kikubwa cha watu wanatazama. Mtumishi huyo, alisimama katikati ya watazamaji wengine, kisha kimya kimya, bila kutamka maneno, akakemea "show" hizo zisifanyike. Mwana mazingaombwe, alijaribu kutumia mbinu na maarifa yake yote, lakini hakuweza tena kufanya yale aliyotamba kwamba atayafanya. Baadaye akasema: "hapa kuna mtu anazuia mazingaombwe yangu yasifanyike!" Lakini hakuweza kujua ni nani.
Mtumishi huyo akathibitisha kuwa ni kweli baadhi ya mazingaombwe huwa yanafanywa kwa kutumia nguvu za giza au uchawi, ndio sababu mwana mazingaombwe huyo hakuweza kuendelea na "show" zake, mara tu Mtumishi huyo wa Mungu alipoyakemea kwa Jina la Yesu.
Hakika Jina la Yesu ni Jina lipitalo majina yote. Likitamkwa kwa sauti ndogo au kubwa au kimoyo moyo na mtu aaminiye kuwa Jina la Yesu lina nguvu, kazi za shetani zinavunjika, mapepo yanatoroka na shetani mwenyewe anakimbia. Anza leo kulitumia Jina la Yesu ku-solve matatizo unayokutana nayo maishani mwako. Wachawi wakija kwako, wakemee kwa Jina Yesu watakimbia. Watu wakikutishia kwamba wataloga biashara yako, zuia mipango yao kwa Jina la Yesu. Ukiona ndoa yako imeingiliwa na mapepo yanayosababisha unafarakana na mwenzi wako wa ndoa, kemea mapepo hayo, utaona chuki na mafarakano vinaisha!