Jiji la Dar kufumuliwa, Kupangwa upya

Jiji la Dar kufumuliwa, Kupangwa upya

Master plan tu bila kuzingatia na kutekeleza yalio ndani ya master plan bila upendeleo au visingizio hapo itakuwa kazi bure.Siasa za Bongo za kubandirika badirika na ugeugeu wa mitazamo ya viongozi hilo nalo ndio tatizo kuu.Sitashangaa kuona wanatumia masterplan kama kulipa visasi,japo waliobolonga ndio hao hao watakokuwa wanaadhibu wakosaji.Ugeto na miundo mbinu mibovu ni makosa ya serikali kwa asilimia mmoja bila ubishi.Hivi miaka 50 na zaidi ndio mnashtuka?
 
Yah... ni good project ingawaje ni very expensive. Hata hivyo, nadhani kwa NSSF ya Dau na JK wangefanya lakini hii NSSF ya sasa na JPM, I doubt if they will! Kwanza hata Mawaziri wataogopa ku-approve larger investment ideas!
Miradi mingi ya NSSF ilikuwa white elephant,mingi ilikuwa ya kipiga deal na 10% ,bei kubwa ya mradi ambazo sio halisi,labda kipindi hiki wanaweza wakatekeleza.....Ni fedha nyingi lakini tunaweza kutekeleza tukiipa long term plan,Kama watu wanainstall vifaa hewa na wanalipwa bilioni karibia 83 hatuwezi kushindwa kuwalipa fidia wakazi wa tandale,manzese,bonde is mpunga,mkwajuni,kigogo etc.
 
Kuna mikoa kibao imechoka sana hii pesa wana taka kugawa tu majengo yatagarimu Pesa nyingi nusu ina ingia mifukoni mwao au wana andaa ufisadi wa namna nyingine!

Sent from my BlackBerry 9360 using JamiiForums
Ufisadi ni asili ya viongozi Wa CCM, hapo panaandaliwa ulaji hakuna LA zaidi
 
Miradi mingi ya NSSF ilikuwa white elephant,mingi ilikuwa ya kipiga deal na 10% ,bei kubwa ya mradi ambazo sio halisi,labda kipindi hiki wanaweza wakatekeleza.....Ni fedha nyingi lakini tunaweza kutekeleza tukiipa long term plan,Kama watu wanainstall vifaa hewa na wanalipwa bilioni karibia 83 hatuwezi kushindwa kuwalipa fidia wakazi wa tandale,manzese,bonde is mpunga,mkwajuni,kigogo etc.
Ah! Amalinze, asikudanganye mtu wangu! Kwenye miradi mikubwa kama hii watu LAZIMA watapiga tu hata hiki kipindi cha JPM labda serikali yoooooote hadi na taasisi zake iongozwe na malaika!

Miradi mikubwa ni ulimbo wa ufisadi sehemu nyingi duniani na kwa Africa utakuta watu wanagawana na mradi haujengwi vilevile
 
Hapo dar kuna Maji ? Labda kwako na mitaa 2 au 3.
Naona kama viongozi wetu wameishiwa uwezo wa kufikiri. Kuna haja gani ya kupoteza hela nyingi kuvunja na kujenga upya, kwanini wasitoke nje ya jiji la Dar, wanaweza kwenda Pwani, Tanga, mtwara ama Lindi wakajenga jiji lingine la kisasa na kuliacha jiji la Dar baadae litageuka kuwa jiji la kihistoria na kubaki na sura yake ya asili. Nimefika London, hakuna majengo marefu kama yalivyo Dubai lakini wana majengo mengi ya kale na ni masafi sana kwani yanatunzwa vizuri. Huko vijijini watu hawana maji wao wanalazimisha kutengeneza hapohapo Dar wanaposhinda hao wanaosema wacheza pooltable.
 
Hela za kuwalipa fidia wanao wazvunjia wanazo au ni muendelezo wa ubabe uliopo? Kwani lazima jiji liwe katikati hapo kwa nini wasitoke nje ya jiji? Kwa mtindo huu wa kuifanya Dar es salaam ni posta ndio maana foleni haziishi, wawa ache wananchi waishi mbona serikali haitaki kwenda Dodoma ili kupunguza msongamano Dar?
 
Wanataka watz wote wahamie dar
Kwa nini msijenge mji mpya nje ya Dar maeneo kama Bagamoyo au kuendeleza miji mingine na kuepuka hii gharama na usumbufu kwa serikali na wakazi wa Dar?
Mnakwenda nje kila siku lakini hamjifunzi kwa majiji kama Delhi?
Mimi napata shaka kama kweli viongozi wetu mmekosa weledi au ni makusudi tu mnacho mnachokitafuta Dar manake hii awamu ya 5 inatawala Dar tu!
Kila siku Dar hiki,Dar kile Dar Dar..Dar...mji una population growth ya kutisha among the top five in Africa badala ya kufikiri kuutanua bado mnang'ang'ana na Manzese wee..mnachokitafuta mtakipata.
Dar itageuka zigo la misumari kwenu very soon!
 
Kuna kampuni inaitwa Moladi ya SA hawa wanatengeneza nyumba za plastic na linamwagiwa cement ni siku mbili tu, na baada ya wiki 2 unahamia na bei ni rahisi sana.

Kwa slams zetu labda wangetengenezewa nyumba za hivyo na bila kusahau drainage system maana huwa tunafikiria kula tu pa kushusha hatukumbuki oops sorry.
1460789956096.jpg
1460789713547.jpg
 
Kupanga jiji upya inawezeka lakini gharama yake ni kubwa sana na sithani kama serekali hii ya kazi tu imeshajipa tayari kwa gharama hizo
 
Ndoto za Wilium Lukuvi..! Indoto ichingi bwana!!!
 
Kiu kweli inauma sana kusikia watu hawatumii Akili tena, na niviongozi tunao waamini, Leo kiongozi a nafikiri watu 40m wamesahau mihemko waliopewa kuhusu kigamboni na mapicha kibao walio kuwa wamebandika bale wizarani na zingine Kwenye mitandao. Tukaambiwa kigamboni itakuwa kama Dubai Leo kigamboni iko vile vile, alafu viongozi wale wale Leo wanatuambia wanataka kufumua jiji Zima. Wkt kigamboni tu I me washinda. Nimshauri tu waziri akamalize kwanza mradi wa kigamboni ndio aanza kufikiria kulifumua jiji lote.
 
hela ya ufufua viwanda shida ndio itakua ya kufumua Dar>
 
Naona kama viongozi wetu wameishiwa uwezo wa kufikiri. Kuna haja gani ya kupoteza hela nyingi kuvunja na kujenga upya, kwanini wasitoke nje ya jiji la Dar, wanaweza kwenda Pwani, Tanga, mtwara ama Lindi wakajenga jiji lingine la kisasa na kuliacha jiji la Dar baadae litageuka kuwa jiji la kihistoria na kubaki na sura yake ya asili. Nimefika London, hakuna majengo marefu kama yalivyo Dubai lakini wana majengo mengi ya kale na ni masafi sana kwani yanatunzwa vizuri. Huko vijijini watu hawana maji wao wanalazimisha kutengeneza hapohapo Dar wanaposhinda hao wanaosema wacheza pooltable.
Tindo, tatizo ni hao aliokuwa akiongea nao. Wangepasa kumuuliza afafanue maana ya kulifumua jiji. Sasa hivi kila mtu anatafasiri anavyojua yeye!
 
Kiukweli itakuwa Poa sana

Vunja vipagala NA majengo yoote yaliopo shaghala bagala
Maana mji imekuwa NA hadhi kubwa kwa sasa
 
Naona kama viongozi wetu wameishiwa uwezo wa kufikiri. Kuna haja gani ya kupoteza hela nyingi kuvunja na kujenga upya, kwanini wasitoke nje ya jiji la Dar, wanaweza kwenda Pwani, Tanga, mtwara ama Lindi wakajenga jiji lingine la kisasa na kuliacha jiji la Dar baadae litageuka kuwa jiji la kihistoria na kubaki na sura yake ya asili. Nimefika London, hakuna majengo marefu kama yalivyo Dubai lakini wana majengo mengi ya kale na ni masafi sana kwani yanatunzwa vizuri. Huko vijijini watu hawana maji wao wanalazimisha kutengeneza hapohapo Dar wanaposhinda hao wanaosema wacheza pooltable.

Nami niliwahi kufikiri hivyo. Nina hakika kabisa kukianzishwa mji mpya mfano maeneo ya Rufiji na ukapangwa vizuri halafu Dar ikapunguziwa baadhi ya functions kama maofisi ya serikali n.k. Dar itapunguziwa presha na mwishowake itabaki ni mji wa kawaida tu bila foleni na matatizo mengine. Hata hivyo, ukifikiri zaidi kidogo unagundua hili haliwezekani. Dar ni mji maarufu na muhimu sana kwa biashara kutokana na location yake.

Ttz ni kuwa karibia asilimia kama 70 ya Dar haijapimwa. Hakuna mitaro, barabara wala miundombinu ya maji taka. Maeneo mengine ni hatarishi lkn yamejaa makazi ya watu. Kuna ttz kubwa la mgawanyo na uwiano wa functions za mji, mf. kila asubuhi lazima watu karibia asilimiazaidi ya 60 waingie mjini na jion watoke hivyo kusababisha foleni kubwa asubuhi na jion.

Kwahiyo hakuna namna ni kuifumua na kuipanga upya. Hili litasaidia kutawanya functions, kuweka miundombinu na kuondoa makazi katika maeneo hatarishi. Mifano ya miji mingine iliyofumuliwa na kupangwa upya ni Addis Ababa. Ukienda Addis sasa kama ulitembelea miaka 10 iliyopita utaona tofauti. mji mwingine ni Kigali.
 
Maendeleo yana gharama zake
kweli kabisa hata ukiona miji iliyopangika kama Tokyo au Washington haikuanza hivyo kuna kipindi yalifanyika maamuzi magumu ikiwa ni pamoja na kubomoa nyumba watu waliathirika na hata kufa lakini miji hiyo sasa ipo smart na kwa dar lazima maamuzi magumu lakini sahihi yachukuliwe
 
Makosa mengi yamefanyika katika master plan zilizopita. Eneo kama la Mbezi Beach viwanja vingi vya wazi na vya taasisi za serikali waliuziwa wenye pesa wakajenga majumba na shule binafsi. Miundo mbinu ya maji machafu hakuna kabisa matokeo yake maji machafu yanatiririshwa kwenye mitaro ya maji ya mvua!
Watueleze wanachotaka kufanya katika mpango wao ili wananchi tuwaeleze hali halisi. La sivyo wananchi watanyanyasika wajanja wachache watafaidi na mji mpya hautaonekana!
 
Sio siri Willium Lukuvi anajitahidi sana kupiga kazi kwa maendeleo ya watanzania.
 
Back
Top Bottom