naomba msaada wako simu yangu tecno m3 nikiingia facebook inazima halafu pia display inachezacheza ukifungua kitu inatokea kitu kingine, video haiplay kwenye instagram na facebook
Note:
1,kujizima ukifungua facebook-inaweza huwa ni software related problem. (jaribu kuclear data za facebook kwenye settings--aplication)
Iwapo bado inazingua, jaribu ku-uninstall alaf restart then install upya.
Ikikataa fanya SYSTEM RESTORE/RESET.
2, Screen kufungua vitu vingine (sijakuelewa vizur ila note yafuatayo)
A-touch screen imekufa. Ndio mana ukitouch haigus exact point ulipogusa.
B-inaweza ikawa virus action , yaan ukifungua data ukifungua app hoi basi inafeli inafungua mavitu ya ajabu
Swali: je hiyo simu yako ilishaanza kujidownload mavitu ukifngua data tu..? Ushwahi kuona app ambazo hujaweka wewe kwenye simu yako?
3, Kioo kucheza cheza(display kucheza cheza) ni dalili mbaya kwa display ya simu yako. Ni dalili ya kifo cha display
Swali: uliitia maji simu? Je uliidondosha ikaangukia angle kwa mshindo mkubwa? Je tatizo lilianzaje?
4, video kutoplay fb na insta hakikisha yafuatayo
A-una internet bundle(nna uhakika hili si tatizo kwako)
B-mtandao upo vizur(nna uhakika hili si tatizo kwako)
Cha kufanya clear data kama nilivoeleza stage 1, ikikataa uninstall na uinstall tena.
Fanya hayo alaf rudi na majibu, pia ningependa kupata screen shot za app drawer yako. Na screen shot ya kila tatizo lako.
Phillz unlock