Jicho langu la tatu na biashara ya bodaboda

Jicho langu la tatu na biashara ya bodaboda

Jamaa anaongea kirahisi tu. Maisha yamekuwa magumu sana mkuu yani usiombe ukose shughuli yeyote rasmi ya kufanya mjini.

Graduates wasio na ajira ama wale waliowahi kufukuzwa kazi ghafla wakaonja utamu wa kushindwa kutimiza majukumu ya mjengoni baada ya hela zote kukata ndio wataelewa uzito wa kazi yeyote inayoweza kukupa hata 10K tu kwa siku! Hata ikiwa kuzoa mavi ilimradi inaingiza pesa.

Kuna nyimbo moja ya Zilipendwa sijui ni ya somebody Daudi kabaka inaimbwa:
"Ikiwa kama wewee ni kijanaa, ukikosa kazi tabu nyingi utazipata"
Ame address issue nzito lakini ambayo ufikiria kuna ukweli kiasi. Tatizo ni hajatoa solution tu
 
Bodaboda ni suluhisho la ajira kwa vijana (kisiasa ni mtaji)

Tatizo hatuangalii athari zake
- Matatizo ya ulemavu kwa vijana kutokana na ajali
- Gharama za kutibu na kuhudumia walemavu hao kwa Serikali na Jamii kwa ujumla
- tatizo la maumivu ya mgongo kutokana na vibration ya muda mrefu
- tatizo la uraibu wa pombe na ngono zembe (vijana hawana nidhamu ya matumizi ya fedha)
- kero za ajali za mara kwa mara
- Tatizo la kumaliza nguvu kazi (vijana wanakimbia kazi zinazotumia nguvu nyingi)
Dah...umesahau na ongezeko la magonjwa ya kisukari, shinikizo la damu na unene kupita kiasi.... Watu wengi hawatembei kwa miguu tena...sehemu walizokuwa wanatembea kwa miguu wakifanya mazoezi bila kujua ....sasa wanapanda bodaboda....ni hatari kwa taifa [emoji2960]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimeona majibu na hoja za wenzangu pia ni mawazo na asanteni kwa michango yenu katika mada hii,nadhani wengi hamjaielewa vizuri mada yangu lakini pia nimelielezea tatizo na aya ya mwisho nimetoa suluhisho la mada yangu nini kifanyike na pia hii ni kwa kuongea nao moja moja wao wenyewe na asilimia kubwa wana afikiana na mawazo yangu kwamba ndoto zao zinakufa sababu kuna kubweteka na mzunguko wa 5000 hadi 10,000 na starehe ambapo ikitokea na familia ikaingia ile 10000/ inakuwa ndogo mara 2 hiyo inamaanisha tayari maisha yameanza kuwa magumu japo anaenda kazini na boda yake.

lakini pia hata mimi mwenyewe sijaajiriwa nimejiajiri hivyo nnaujua vizuri mziki wa mtaani na ugumu wake,lakini pia nnajua vitu gani vinatufelisha malengo sababu wote tumepitia hiyo hatua sema kwa njia tofauti,ishu kubwa nnayoiangalia ni baada ya miaka 15 - 20 hawa madreva boda wa leo watakuwa wapi na familia zao zitakuwa wapi,sababu asilimia kubwa ni vijana.

Tunahitaji kubadilisha mitazamo sana na kujitambua ili kuweza kuwanusuru,SA ishu ilianza hivi hivi kwa wazawa kuwa vibarua na wageni kuwa na kazi nzuri mwisho wake wote tunafahamu,vitu huanza pole pole vikiwa vinaoenakana vya kawaida ila madhara yake yanaweza kuwa ya muda mrefu,ni sawa na kupanda boda hiyo hiyo halafu ukawa unaendesha kwa kasi bila tahadhari ukifika salama unashukuru ila ukipata ajali ni kilema cha maisha.

Kujitambua ni neno kubwa na pana sana kuliko maana yake.
 
Back
Top Bottom