Roulette
JF-Expert Member
- Dec 15, 2010
- 5,579
- 5,375
Siku kadhaa zilizo pita kuna member alitoa post kuhusu utaratibu wa ku-manage nyumba ndogo ili asi lete utata. Member huyo anaitwa The Boss.
Pamoja na kumshukuru kwa kutoa maoni na shauri zake kuhusu Nyumba ndogo, mimi kama mwanamke nimeona siwezi kujibu kwenye post lile ila nifungue tu thread mpya sababu mtazamo wangu na wake ni tofauti kabisa.
Kwa kumalizia nataka kukumbusha kama kila mtu ana mtazamo wake wa haya mambo na nina heshimu mtazamo wa kila mtu. Huu hapa ni mtazamo wangu na naomba uheshimiwe pia. Sijakataza kutoa maoni yenye kupinga mtazamo, nimeomba tu tuchangie kwa heshima.
Asanteni.
Pamoja na kumshukuru kwa kutoa maoni na shauri zake kuhusu Nyumba ndogo, mimi kama mwanamke nimeona siwezi kujibu kwenye post lile ila nifungue tu thread mpya sababu mtazamo wangu na wake ni tofauti kabisa.
- Kwanza namlaumu kwa kutoa thread kama hiyo sababu ina halalisha kitu kilicho haram. nikijieleza kwa mfano, ni kama kusema inakatazwa kuua mtu ila kama utaamua kumchinja kumbuka kutoa carpet usilijaze damu. Mtasema hana influence ya kuhalalisha au kuharamisha kitu, na ni kweli, ila yeye ndie alitoa mwelekeo wa thread na kila alie changia kwa kumsupport (na kila alie like thread yake) ameongeza sauti lake kwenye mada na hivo msomaji wa kawaida (mimi na wewe) tunahisi kuna watu wengi sana wanamtazamo huo. Kwa mtu alie kua na nia ya kwenda nje, au Yule tayari anatembea nje ya ndoa, ni ruhsa tosha ya kuendelea katika njia hiyo.
- Pili, kama ikitokea mtu aanguke na atoke nje ya ndoa, shauri la kumpa sio namna gani aifanya hali hiyo iwe shwari na idumu, bali nikumshauri namna gani anaweza kujitoa katika mtego huo. maada ya thread hii sio kutoa huo ushauri, labda nitarudi baadae.
- La tatu na lililo nikwaza zaidi ni heshima ndogo ya utaratibu mzima kwa wanawake, iwe nyumba kubwa au nyumba ndogo. Kwa namna nilisoma thread (kama nilikosea naomba anikosoe) kila kitu kina husisha kugawa hela kati ya nyumba kubwa na nyumba ndogo (material distribution) na heshima/mtazamo wa ndugu na rafiki. sikuona katika thread hiyo mapenzi yanawekwa wapi, heshima ya muhusika kwa nyumba kubwa, au nyumba ndogo, watoto, tegemeo za watu wengine na kadhalika vikija katika hesabu.
Kwa kumalizia nataka kukumbusha kama kila mtu ana mtazamo wake wa haya mambo na nina heshimu mtazamo wa kila mtu. Huu hapa ni mtazamo wangu na naomba uheshimiwe pia. Sijakataza kutoa maoni yenye kupinga mtazamo, nimeomba tu tuchangie kwa heshima.
Asanteni.