Jibu hesabu yangu, wengi mtafeli hapo

Jibu hesabu yangu, wengi mtafeli hapo

Jibu ni 90. Kwa ujanja aliruka ile 8+8, ambayo ilikua ni 72.
Kwa anayejua Arithmetic Series, kuna mfanano kidogo na hesabu ya Mzizi Mkavu, kwa sababu Common Difference d=2 kwenye swali hili.
 
  • Thanks
Reactions: GUI
90

Ukifuata trick ya upande wa kushoto:
Ameanza na 4+4=20, ina maana hapa 4 imebeba thamani ya 10
Ikafuatia 5+5=30, hapa 5 imebeba thamani ya 15; Kutoka 10 hadi 15 kuna ongezeko la 5
Ikafuatia 6+6=42, hapa 6 ina thamani ya 21, ambayo ni sawa na 15 jumlisha 6
Kwa maana hiyo kwa kila hatua, inaongezeka thamani ya 1 zaidi ya lile ongezeko husika
Hivyo 7+7, ni sawa na (21+7) + (21+7), 28+28=56
Iliyorukwa 8+8 ni sawa na (28+8)+(28+8) yaani 36+36=72
SASA 9+9 ni sawa na (36+9)+(36+9), yaani 45+45=90

Kwa upande wa kulia (wa majibu)
Tunaanza na 20
Inafuata 30, yaani 20+10
Kisha inafuata 42, yaani 30+12
Kisha inafuata 56 yaani 42+14
Kisha itafuata 72 iliyorukwa yaani 56+16
Mwisho kabisa kwa kufuata trend ya 10, 12, 14, na 16...inayofuata itapata ongezeko la 18, hivyo itakuwa 72+18=90

Hizo ni njia mbili za kufikia jibu la 90, najua zipo nyingi ila mimi nimeonyesha hizo mbili tu.

Mwenye jibu tofauti atuelezee naye kalipataje.
 
Jibu ni 90
Njia zaweza kuwa nyingi ila mimi nimetumia hii.
4 + 4 = 20
Hapo kafanya 4×4 + 4 = 20.
5 + 5 = 30
Hapo kafanya 5 x 5 + 5 = 30.
6 + 6 = 42
Kachukua 6 x 6 + 6 = 42.
7 +7 = 56
Kachukua 7 x 7 + 7 = 56
So
9 + 9 = 90
Yaani 9 x 9 + 9 = 90
 
Back
Top Bottom