JF miaka 50 ijayo akili bandia itakapokuwa ndio kila kitu

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,634
697,916
Hii kitu si ramli wala utabiri wa kubahatisha bali ni mchakato wenye matokeo yasiyozuilika wala kushindwa.. Ni mchakato unaoipeleka dunia na ulimwengu mahali ambako binadamu, mimea na viumbe hai vv yote vitakuwa si vitu vya asili tena bali vya kupangwa na kutokea kwa kutumia akili bandia tuu

Mifano ni mingi kutokea ujima zama za mawe mpaka hapa tulipo leo.. Kuna mabadiliko mengi mno makubwa na madogo yametokea na yanazidi kutokea
Kwasasa Mmarekani anafanya majaribio ya ndege ambazo zinaweza kukupeleka popote duniani kwa masaa mawili tuu.. Lakini huko tuendako muda utapungua mpaka kufikia dakika chache
Inawezekana kabisa kufikia kufumba na kufumbua umefika utakapo ama bila hata kusogeza mguu sehemu uitakayo itakuwa mbele yako at a click

Tukiachana na mifano migumu na ya mbali unakumbuka namna vile Shule za msingi tulivyokuwa tunakariri table ya 1 hadi ya 12? Leo ni watoto wetu wangapi wanaweza? Vikokotoo vimechukua akili zao
JF hii ya sasa ya kuumiza kichwa ili mtu aandike mada. Afikirie sana, awe na simu yenye network na chaji halafu iwe na bundle.. Kisha aanze kuandika heading halafu maudhui.. Na wakati wa kuandika akosee hapa na pale .. Aandike afutd.. Andike afute.. Hii tabu yote haitakuwepo tena!

Kwa kujua ama kutojua JF ya sasa inatengeneza kitu kikubwa sana ambacho vizazi vijavyo miaka 50 mbele havitakuwa na uwezo wa kutengeneza na vitaiona JF na wanachama wake watu waliokuwa na akili kubwa za kipekee na za ziada

Haya mabadiliko yameshaanza kutokea kwenye taaluma ya sanaa ya picha.. Hakuna ubunifu wa kuchora tena kwa kutumia akili binafsi na mikono.. Unaiamrisha tu akili bandia kupitia application maalum kile utakacho nayo ndani ya sekunde chache inakuletea vilevile ulivyotaka
Nimeliona hili pia kwenye vitu vingine vidogo vidogo lakini ndio hivyo akili zetu asilia zinaliwa taratibu na kirusi kibaya cha akili bandia
Huko tuendako hakutakuwa na haja ya kutumia muda mwingi, kuwaza kuumiza kichwa na kuandika mada .. Itakuwa ni mwendo wa kuamrisha akili bandia ikuandikie nayo ndani ya dakika mada kwa idadi ya maneno utakayo utakuwa tayari.. Na hili wala haliko mbali
1525c37b7f67f319327f6030cf2b202b.jpg
 
Hakuna ubunifu wa kuchora tena kwa kutumia akili binafsi na mikono.. Unaiamrisha tu akili bandia kupitia application maalum kile utakacho nayo ndani ya sekunde chache inakuletea vilevile ulivyotaka
Sidhani. Wachoraji wapo.. tena za kuchorwa na mkono zina bei sanaaaa kuzidi hizo za kuprint/ kuchora na akili bandia.
 
Hii kitu si ramli wala utabiri wa kubahatisha bali ni mchakato wenye matokeo yasiyozuilika wala kushindwa.. Ni mchakato unaoipeleka dunia na ulimwengu mahali ambako binadamu, mimea na viumbe hai vv yote vitakuwa si vitu vya asili tena bali vya kupangwa na kutokea kwa kutumia akili bandia tuu

Mifano ni mingi kutokea ujima zama za mawe mpaka hapa tulipo leo.. Kuna mabadiliko mengi mno makubwa na madogo yametokea na yanazidi kutokea
Kwasasa Mmarekani anafanya majaribio ya ndege ambazo zinaweza kukupeleka popote duniani kwa masaa mawili tuu.. Lakini huko tuendako muda utapungua mpaka kufikia dakika chache
Inawezekana kabisa kufikia kufumba na kufumbua umefika utakapo ama bila hata kusogeza mguu sehemu uitakayo itakuwa mbele yako at a click

Tukiachana na mifano migumu na ya mbali unakumbuka namna vile Shule za msingi tulivyokuwa tunakariri table ya 1 hadi ya 12? Leo ni watoto wetu wangapi wanaweza? Vikokotoo vimechukua akili zao
JF hii ya sasa ya kuumiza kichwa ili mtu aandike mada. Afikirie sana, awe na simu yenye network na chaji halafu iwe na bundle.. Kisha aanze kuandika heading halafu maudhui.. Na wakati wa kuandika akosee hapa na pale .. Aandike afutd.. Andike afute.. Hii tabu yote haitakuwepo tena!

Kwa kujua ama kutojua JF ya sasa inatengeneza kitu kikubwa sana ambacho vizazi vijavyo miaka 50 mbele havitakuwa na uwezo wa kutengeneza na vitaiona JF na wanachama wake watu waliokuwa na akili kubwa za kipekee na za ziada

Haya mabadiliko yameshaanza kutokea kwenye taaluma ya sanaa ya picha.. Hakuna ubunifu wa kuchora tena kwa kutumia akili binafsi na mikono.. Unaiamrisha tu akili bandia kupitia application maalum kile utakacho nayo ndani ya sekunde chache inakuletea vilevile ulivyotaka
Nimeliona hili pia kwenye vitu vingine vidogo vidogo lakini ndio hivyo akili zetu asilia zinaliwa taratibu na kirusi kibaya cha akili bandia
Huko tuendako hakutakuwa na haja ya kutumia muda mwingi, kuwaza kuumiza kichwa na kuandika mada .. Itakuwa ni mwendo wa kuamrisha akili bandia ikuandikie nayo ndani ya dakika mada kwa idadi ya maneno utakayo utakuwa tayari.. Na hili wala haliko mbali View attachment 2914315
umeona mbali mbali sana brother, ila mimi ninaamini katika mzunguko, ipo siku duniani mwanadamu vitarudi katika asili yake ya mpaka kwenye za mawe , japo athari itakayokuwa na teknolojia itakuwa sio ndogo ila wakati fulani mwanzo utarudi.
 
Waboreshe zaidi sex dolls za AI na iwe nafuu kupatikana. Hakuna mambo ya kutuma nauli tena. Unaingia kwenye app tu unamprogramme mdoli wako alie kihindi kwa tendo husika. Raha mustarehe.
 
Waboreshe zaidi sex dolls za AI na iwe nafuu kupatikana. Hakuna mambo ya kutuma nauli tena. Unaingia kwenye app tu unamprogramme mdoli wake alie kihindi kwa tendo husika. Raha mustarehe.
Mungu wangu
 
  • Kicheko
Reactions: xox
umeona mbali mbali sana brother, ila mimi ninaamini katika mzunguko, ipo siku duniani mwanadamu vitarudi katika asili yake ya mpaka kwenye za mawe , japo athari itakayokuwa na teknolojia itakuwa sio ndogo ila wakati fulani mwanzo utarudi.
Inaweza asili itarudi ila ni baada ya anguko la ulimwengu huu kutokana na kikomo cha matumizi ama matokeo ya matendo ya binadamu
 
Sema AI inajibu maswali vizuri , nilichogundua uwepo wa AI umekuja na faida pia. Kwa sisi knowledge seekers
 
Back
Top Bottom