Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,702
Sikumbuki hasa kilichotufikisha kwenye mjadala wa kujadili kuhusu mwanandoa mmoja kufariki,lakini ambacho nakijua ni kuwa kuna mgogoro mkubwa kwenye tulichokua tunakijadili.Mjadala wenyewe ni kuwa,je mume anapofariki na kuacha watoto na mjane,mali alizoacha nani anatakiwa kuzisimamia?Pia kama mjane atakuwa anahitaji kuliwazwa je akipata mtu ahame nyumbani na akakae sehemu tofauti au palepale?Vijana wote isipokuwa mimi tu walidai kuwa,mali anatakiwa asimamie ndugu wa mume na kama atahitaji mume ahame pale nyumbani,walizungumza mengi na kudai mali ni za mume na mke haruhusiwi kuzisimamia!!Nilishangaa sana!MSIMAMO WANGU ulikuwa hivi;mke ana haki sawa na mume kwenye suala la kutolea maamuzi,mume ni kiongozi mkuu,maadam hayupo mke ndie mwenye last say!Ni aibu kubwa mwanaume mzima kwenda kuleta usumbufu kwenye mali za mwanaume mwingine,atafute zake!Pia mke anaweza kutumia mali atakavyo bila kuulizwa na YOYOTE,hata akitaka kuolewa hatakiwi kuulizwa chohote ni sawa na mume angeoa na kuishi pale na mke mpya!!Je nyie wana JF mwasemaje?