JF Karibuni Tanzania Professionals Network

kwa nini umeamua kuitambulisha TPN huku JF badala ya kutumia vyombo vya habari
 
Naomba nimsaidie Rais Mtsimbe kujibu swali lako kwa kukujulisha kuwa JF pia ni chombo cha habari.

Asante zemarcopolo kwa kuweka wazi kwa JF pia ni chombo cha habari. Pia TPN imekuwa ikijitangaza kwa nyakati tofauti katika vyombo vya habari kila kunapokuwa na haja ya kufanya hivyo kama Magazeti, Radio, TV na Mikutano.

Napenda sasa kutamka rasmi kuwa mjadala huu umefungwa.
 
Hivi Mtsimbe Huna PR Wako? Au Ndio Prossionalism Yenyewe? Au Uongozi Haupo? Na Kama Upo Mbona Haufanyi Kazi?AU WENGINE MAFISADI? President Anakuwa Na Role Kubwa Si Hii Ya Kuja Jf...

Kama Hii Ndio Prossionalism Yenyewe, Basi Tuna Kazi Kubwa!!!!
 
TGeofrey, asante sana kwa kutuunga mkono na karibu tushirikiane wote kujiletea maendeleo yetu sote.

Ndugu yangu Chuma, nilikuwa nafikiri mjadala umekwisha na nilikwisha kuufunga. Hata hivyo ukipitia posts mbalimbali katika thread hii utagundua kuwa kuna maelezo ya kutosha sana kwa comments zako. Hata hivyo kama una mambo au maoni mazuri ya kuboresha unakaribishwa kuyatoa.

Naomba nichukue nafasi hii kwa mara nyingine kuwashukuru wote mliochangia katika mjadala huu na kwa mara nyingine tena naomba nitamke kuwa mjadala huu sasa umefungwa.
 
Sanctus Mtsimbe, tembelea hii website hapa chini:
The Federation of Small Businesses, in UK

About the FSB
The Federation of Small Businesses is the UK's largest campaigning pressure group promoting and protecting the interests of the self-employed and owners of small firms. Formed in 1974, it now has 215,000 members across 33 regions and 230 branches.​


Tanzania tuna network kama hii?
 
Huyu katoa mwalikona ni kwa nia nzuri saana,ametambua mchango wa wana JF na ndo maana akatoa mwaliko.Mwaliko kama mwaliko ni ihari yako,waweza kuwa mwana jf na ukawa mwana TNP uamuzi ni wako aua ukaamua kubaki ktk kimoja wapo kati ya hivi viwili. Matusi siyo mazuri,nia yetu ni kuelimishana na kusahihisha pale penye mapungufu.
 
Sanctus Mtsimbe, tembelea hii website hapa chini:
The Federation of Small Businesses, in UK

About the FSB
The Federation of Small Businesses is the UK's largest campaigning pressure group promoting and protecting the interests of the self-employed and owners of small firms. Formed in 1974, it now has 215,000 members across 33 regions and 230 branches.​


Tanzania tuna network kama hii?

Mzalendo LazyDog;

Asante sana kwa dokezo. Nimetembelea tovuti hiyo ina mengi mazuri ya kujifunza. Ni kutokana na hilo pia kuna issue moja nataka tuifanyie kazi pia.

Stay blessed.
 
Naitwa Sanctus Mtsimbe na naomba niungane na wana JF wengine waliojitambulisha kwa majina yao halisi na kuomba tuweze kuungana na kufanya mambo ya kimsingi katika kuleta maendeleo ya nchi yetu.

Nimekuwa msomaji mkubwa wa JF toka mwaka 2007 na leo nimeona ni vema nami nijitokeze kuandika machache. Napenda kuishukuru na kuipongeza JF na uongozi na wanachama wake kwa kazi kubwa na nzuri manayoifanya katika kuleta changamoto mbalimbali.

Napenda kutoa mualiko rasmi kwa kuwakaribisha wana JF wenye mtazamo na mwelekeo wa kupenda maendeleo ya kweli kujiunga katika Mtandao wa Wanataaluma Tanzania (Tanzania Professionals Network, TPN). TPN ni mtandao unaowaunganiasha wanataaluma wa fani mbalimbali bila kujali nafasi au vyeo vyao ikiwa na madhumuni ya kuwezeshana Wanataaluma na Wananchi kwa ujumla kiuchumi na kifedha.

Kwa kuwa michango mingi ya Wana-JF ni kwa ajili ya maendeleo na ustawi wa Watanzania na Nchi kwa ujumla (Kitu ambacho TPN pia inafanya), karibuni sana tuweze kuungana na kuonana katika mikutano ya mara kwa mara ambayo ina lengo la kuboresha maisha yetu.

Kwa taarifa zaidi, tafadhali tembelea tovuti ya www.tpn.co.tz (Bado tovuti inaboreshwa . . . ). Tunakaribisha pia maoni yenu yenye mwelekeo wa kujenga na kuimarisha TPN.

Na kama kuna ufafanuzi wowote unahitajika, tafadhali tuwasiliane kupitia barua pepe president@tpn.co.tz au +255-754-833-985.
Hili ndilo bandiko la kwanza la Santus akiwa verified.
Kwa maoni yangu, a deserving farewell kwa member wetu yoyote, aliyetangulia mbele ya haki ni kumuaga kupitia maandishi yake, threads zake ili kujikumbusha mawazo yake, maneno yake na matendo yake tukiendelea kuishi Tribute to Sanctus Mtsimbe: Sio tu ni smart kwa mavazi na muonekano, pia ni smart kwa mawazo, maneno, na matendo, na very smart upstairs!

RIP Comred Santus Mtsimbe, maandishi yako humu JF, yatakuishi milele!.

Umepigana vita vilivyo Vitakatifu,
Mwendo Umeumaliza, Imani umeilinda.

Bwana Ameleta, Bwana Ametwaa, Jina Lake Lihimidiwe!.

Paskali
 
Back
Top Bottom