JF imefunguliwa(?) Naipata bila VPN

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
38,817
Reaction score
90,210
Hamjambo wote!

1. Turudi kwenye majukwaa, vilinge na vijiwe vyetu.

2. Matusi tupunguze maana kuacha kabisa kuna watu najua hawataweza.

3. Uzushi, bullying, kejeli, kuvuana nguo tuache.

4. Ukosoaji uendelee sambamba na suluhu kwa Kila ukosoaji.
Haina maana kukosoa bila kutoa suluhu kwa kile unachokosoa.

5. Kupongeza kusizidi hasa kwa kile kikosi kazi cha uchawa. Kwa sababu uchawa ukizidi wengine uvumilivu huwa Mdogo hujikuta wanatukana.

6. Mada za elimu, kuonya, burudani, kupiga soga, kuchombeza, fursa, n.k. ziendelee.

7. Tuwape Uhuru vijana wetu wadogo wale wenyw umri wa kujadili ngono, uchakataji, mapenzi kufanya hivyo bila kuwa kejeli kwani huo ni umri wao.
Lakini pia wapo watu wazima wachache ambao kwao hiyo ni starehe na hobby.

8. Mabishano na uchokozi wa hapa na pale ni muhimu kuchangamsha kijiwe lakini usizidi.
Sisi wengine hatuwezi ishi sehemu tulivu bila kuona hekaheka, uchokozi,

9. Mada tata zianzishwe, zile ambazo wengine hasa watu wengi huogopa kujadili. Ndio maana ya kutumia anonymous.

10. Spana ziendelee kama kawaida bila kumuangalia mtu usoni. Dadeki!

11. Kumekucha

Kazi ianze.
 
Hiyo ni glitch tu kwenye system Hii ngoma kufunguliwa sio leo Man.
 
Baada ya kudukua ID zetu ndio mnaleta fungula mbwa

Kuna siku nilifuta data kwenye app ya jf na nikashindwa tena kurudi mpaka nimetuma browser imbayo ipo connect na ID zangu za Google.!?

Acheni ujuaji na tutatukana sana tu
 
Kama imefunguliwa basi ni muda wa kuweka nyuzi za kutafuta wake
 
Haijafunguliwa.

Saazingine huwa app inamissbihave inaachia na baadaye kujifunga tena.

Emb rudi nyuma uone kama utaweza kuingia bila Vpn mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…