JF Hip-hop frestyle battle

JF Hip-hop frestyle battle

Ebu njo mbona hivi jaman anakuita au ubamdogo umeisha nijue mie nitafute bamdogo mwingine
Yupi tena umempata wa kuwa bamdogo wako?

Haujanijibu ujue, umemkubalia?
 
Sijampata kwani we umeshanikataa me kuwa mwanao nijue ndio nimemkubalia
Kwani utoto kwa mzazi huwa unaisha?

Kubalianeni mahari iniletee nitoe zawadi hapa kwa mshindi
 
Daby Daby
That's my name bro/

You'll shabies
I represent 1st color in rainbow/

Mnamake noise
Wakati nyie light weight/

Mnafail kuloud voice
Mnagombania kuwa size eight/

Nawachana jukwaani
Tena nawasha fire/

Mapepo ibadani
Dude nawasha kaya/

Ona, navyoutawala uzi
Kwa battle nawapodoa/

Onja, acha kupiga miluzi
Kidume ushaachwa unakodoa/

Hali sio poa
Namechange climate mpaka weather/

Napiga hadi naboa
Uzito mzito niite myweather/
Noma noma hapo nafanya editing kidgo tu
 
Naanza na shukrani, kwa mwenyezi/
As a dropa,nadrop thanks kwa wazazi/
Niite poorbilionea,niliye na fikra bilionz/
We si poorbilli-on-Air,unaziota tu on the air/
..................
......aaaaaaaagh mtaiba mtaiba line bhana
Ooooooh warr' up ninjaa naona kijiwe kimya sana stori za shunie tu on the air na kimbumbu michano vp.........
 
Nakaba kila kona, kwa mahaba bila noma
Si haba ninapona, naranda Dar -Kigoma
Makahaba watashona, Sodoma nishagoma
Koloni la wakoma watakoma
Nanona, ka shavu la mtoto wa geti kali
Nasonya, kwa ubavu wa moto wa cheti cha serikali
Hii habari matata, kama kupigwa mbata makata
Katika harusi ya kaka jiko aliyepata
Wapinzani, nawaacha gizani kama hawana LUKU
Wakidhani nawakacha mezani kwa mtaharuku
Hivi vitu ni fani, Nyangema usiijaribu
Hii kuntu mizani, mtagema mtaharibu
Nazoa mahela kama Bahati Nasibu
Naboa kwa trailer movie lake hutanijibu

Shall I continue ?
U better continue mkuu/
Tuko vilimanjaro wengi humu vichuguu/
Hua nastand man alone kucompete na macrew/
Wakileta mistari kinda mistari ya kidada duu/
Me natema mistari ninja inayopiga konfuu/

form1


Sent from my HTC One using JamiiForums mobile app
 
U better continue mkuu/
Tuko vilimanjaro wengi humu vichuguu/
Hua nastand man alone kucompete na macrew/
Wakileta mistari kinda mistari ya kidada duu/
Me natema mistari ninja inayopiga konfuu/

form1


Sent from my HTC One using JamiiForums mobile app
Kung-fu, kung-fu, kung-fu
Aliye chini mngoje juu
Chukua ngazi we Masakuu
Usichague kazi ka sista du
Mchagua vazi hupata tu
Muagua kizazi hufata ku
Mchagua nazi hupata koroma
Kama bazazi wadata Dodoma
Kama wazazi wataka Sodoma
Bunge bange karata za kibabe
Tufunge ugangwe parata za mazabe
Bongo si Congo michongo ya uongo
Dogo madongo fyongo mbogo sifongo
Divai ya Ndugai imekinai kwa wenye tai
Uhai wa nishai wana rai sio chai
Kama vazi la kuazima kwenda kwa Mchungaji Gwajima
Ujima hima kima tendea haji kipaji lazima
Aluta continua mapambano endelea
Karuka kautimua hata kama Segerea

Sent from my Kimulimuli
 
Once in a while nakuja kuwapa hi,

Zawadi ni yangu nimeshachoka kuidai,

Pambano lina miezi kumalizika imekua utata,

Nikatoa lyrics jiwe zikacrash hawa marapa,

Mtoa zawadi akasepa marapa wakachapa lapa,

Uzi unanuka damu nimechinjia people baharini,

Hawana tena hamu humu ndani natamba mimi,

Al-Watan na mistari myembamba ka flat screen,

Sogeza pua nikuumize kameze Asprin
 
Kung-fu, kung-fu, kung-fu
Aliye chini mngoje juu
Chukua ngazi we Masakuu
Usichague kazi ka sista du
Mchagua vazi hupata tu
Muagua kizazi hufata ku
Mchagua nazi hupata koroma
Kama bazazi wadata Dodoma
Kama wazazi wataka Sodoma
Bunge bange karata za kibabe
Tufunge ugangwe parata za mazabe
Bongo si Congo michongo ya uongo
Dogo madongo fyongo mbogo sifongo
Divai ya Ndugai imekinai kwa wenye tai
Uhai wa nishai wana rai sio chai
Kama vazi la kuazima kwenda kwa Mchungaji Gwajima
Ujima hima kima tendea haji kipaji lazima
Aluta continua mapambano endelea
Karuka kautimua hata kama Segerea

Sent from my Kimulimuli
Whatsup al_watan naona unajitahidi
Ila uliona wapi kobe kumzidi duma spidi
Me ni mzee wa kimyakimya sionekani kila thread
Nawasha moto ukizingua hua sina vita baridi
 
Whatsup al_watan naona unajitahidi
Ila uliona wapi kobe kumzidi duma spidi
Me ni mzee wa kimyakimya sionekani kila thread
Nawasha moto ukizingua hua sina vita baridi

Wewe wasema najitahidi, kwa ukaidi
Mimi gaidi zaidi inavyobidi
Kimbiza kama Diddy, msela kuliko Njaidi
Kwa mistari iliyoshinda ya Fidi
Ntakuelekeza kibra nikuchinje kama ISIS
Crisis, don't you ever try this
Wewe si duma, labda umedumaa
Hapa umebuma, shukuru Ijumaa
 
Wewe wasema najitahidi, kwa ukaidi
Mimi gaidi zaidi inavyobidi
Kimbiza kama Diddy, msela kuliko Njaidi
Kwa mistari iliyoshinda ya Fidi
Ntakuelekeza kibra nikuchinje kama ISIS
Crisis, don't you ever try this
Wewe si duma, labda umedumaa
Hapa umebuma, shukuru Ijumaa
Hii ni mistari beginner ina shombo kali la rookie,

Rudi jifunze kuongea ukashindane na Cookie,

Flow zimejaa kichwani haina haja kubusti,

Nyangema usishindane nami mistari yako midugi,

Ukizidiwa muite Daby ukija peke yako umebugi,

Hakuna one two one two nakuchana tena rudi
 
Hii ni mistari beginner ina shombo kali la rookie,

Rudi jifunze kuongea ukashindane na Cookie,

Flow zimejaa kichwani haina haja kubusti,

Nyangema usishindane nami mistari yako midugi,

Ukizidiwa muite Daby ukija peke yako umebugi,

Hakuna one two one two nakuchana tena rudi

Nilichosema unarudia, nilichotema unabugia
Nilichohema unarukia, chema hujasikia
Utungo uvundo, na upiga kwa nyundo
Lundo mdundo, pa kuiga mkumbo
Unafananisha injinia na fundi wako mchundo
Utaharisha sikia kumbikumbi wa Vunjo
Nasababisha dunia kulia kwa masizi na gunia
Kama unabisha tulia mashauzi atamia
Kaa tembe, kaa pembe, Al-Watan jembe
Kataa chembe za tembe za kupata uzembe
Sikiza mawaidha, Madela Gawiza Sukuma
Mi mfalme Kaiza, msela nawiva acha shutuma
Mi Papa, we hujapata hata ukata
Ntakukata kwa makata nikutukane, Mkapa
Hapahapa kwa karata mwanawane, ubapa
Namwaga madini, pandisha majini
Homa yako nini? Ntakupatia kwinini
Adabu ajabu, ondoa ulabu
Nakuchapa kitabu, uniamkie ka babu
Akili adili, kaa nakuajiri
Nikupe siri dili ukiri mi natema hariri
Nakunya almasi kwa kasi, kaa basi la Dar
Napiga pasi ya hasi zima taa kwenye bar
Nipitishe kijiti
Watoto wanikimbia kama jangili la Kibiti
Na sasa nakusikia waomba badili biti
 
Nilichosema unarudia, nilichotema unabugia
Nilichohema unarukia, chema hujasikia
Utungo uvundo, na upiga kwa nyundo
Lundo mdundo, pa kuiga mkumbo
Unafananisha injinia na fundi wako mchundo
Utaharisha sikia kumbikumbi wa Vunjo.....
Biti isichange ibaki hapa hapa,

Humu maajabu ni mengi Al-Watan kajiita papa,

Natema madini mengi almasi zako taka taka,

Mi ndo Lucifer mshenzi we kwangu mtoto makata,

Mbele ya watu wengi nimekuja kukupakata,

Mpakato wa utata mwingi na utamu wa kuzidi kijiti,

Anauchezea Malinzi bado wewe jangili la Kibiti,

Nafreestyle siagi we unafreestyle shit
 
Nilichosema unarudia, nilichotema unabugia
Nilichohema unarukia, chema hujasikia
Utungo uvundo, na upiga kwa nyundo....
Hahahah umeingia chimbo siyo jitahidi kaza matako,

Wenzako walitoka mbio kama kuisurvive Machakos,

Mwendo wa dj cleo na night kali ya Rambo,

Unaleta komedi uchwara na ushit mbuzi wa Bambo,

Mistari inagalagaza kama imesomea Sambo,

Mistari yako muwa hii yangu ni rambo,

Jitahidi kufreestyle kiume usilete michambo
 
Back
Top Bottom