Duh siyo unanionea kweli?Mazee itabidi tuite watu wapige kura hii battle ya Castr na Al-watan
unanigeaje beginner sasa?Jinsi vina ninapanga,sijui utapita wapi/Wewe wasema najitahidi, kwa ukaidi
Mimi gaidi zaidi inavyobidi
Kimbiza kama Diddy, msela kuliko Njaidi
Kwa mistari iliyoshinda ya Fidi
Ntakuelekeza kibra nikuchinje kama ISIS
Crisis, don't you ever try this
Wewe si duma, labda umedumaa
Hapa umebuma, shukuru Ijumaa
Bolo young a.k.a fc libolo,Kamikaze kamakazi waziwazi
Nivikaze kamba kazi wasiwasi
Ganzi kwa vichwapanzi wa takwimu
Banzi kwa jicho pasi na unajimu
Watoto na wazazi wakose radhi kwa kazi
Mashauzi mashuzi ya mbaazi kwa baadhi
Tukwite Suzi huna vuzi mpuuzi
Vifaranga vya juzi vinaudhi kubuzibuzi
Kazini, mpini mjini sikijijini
Toa vimini, kula yamini hamsini
Ubongo wako mdogo
Udongo kwako msongo
Uongo wako kibiongo
Longolongo kama bomba la Songosongo
Nakutoa tongotongo, kidogo kidogo
Natunga sheriaka kigogo wa Kigogo
Kila mstari unachana, shari kwa vijana
Kwa sana, usiku na mchana
Nawaka, hela kwangu nasaka
Wenye njaa sera zangu nafaka
Mistari ya kibepari, hatari ka jemedari
Hii ari kali zali ka habari ya serikali
Kitambo sijatia Miguu kilingine humu.Mazee itabidi tuite watu wapige kura hii battle ya Castr na Al-watan
Ulipotea sana chlorine gas!!!The gas jina ,uwezo mkubwa ka waves za katrina
Mtonyo sina,ila flows zangu znavua bikin wakina tina
Wanao nijua wanajua am the best rapper
Kama jini anayatisha basi niite makata
Hakuna utata
Hawa kinda nawapakata
Daby usinifananishe mana sifanani nao
Mana wao wana copy swaga na viwalo vya dada zao
Habar wanayo
Wanavyo hate mi nakaza natoboa mpaka pande zao
Call me mfarisayo mwenye uchu na ushuru
Akya Mungu ningekua takukuru ningekua kigogo zaidi ya beno nduru
Ukitaka kua maarufu,basi mdis gas
Rapper mwenye kura turufu,hata nikiua sipati kesi
Post sent using JamiiForums mobile app