😂💔😂KUANGALIA MPIRA NA MWANAMKE👩 NI STRESS KUBWA 😂💔😂
👩Mke: Timu gani zinacheza?
👱🏾♂️Mume: Arsenal dhidi ya Manchester United.
👩Mke: Aaah safi! Napenda Arsenal...
👱🏾♂️Mume: Hiyo ni timu nzuri...
👩Mke: Drogba anacheza?
👱🏾♂️Mume: Hachezi kwenye hizi timu...
👩Mke: Sawa mpenzi...huyo ni Chris Brown?
👱🏾♂️Mume: [🤦🏾♂️😫] Hapana, huyo ni Chamberlain...
👩Mke: Aaah lakini wanafanana...ile kadi ya njano ni ya nini?
👱🏾♂️Mume: Ni onyo kwa mchezaji...
Baada ya dakika chache Rooney anafunga goli kwa Manchester United...
👩Mke: [anashangilia🥳🥳] Hiyo goli kafunga Chamberlain?
👱🏾♂️Mume: [🥺] Hapana, Rooney wa Manchester United...
👩Mke: [😡] Inakuwaje? Arsenal ndio walipaswa kufunga!
👱🏾♂️Mume: [🤐]
👩Mke: Na ile kadi nyekundu ni ya nini?
👱🏾♂️Mume: [🤦🏾♂️😢] Hiyo inamaanisha mchezaji anatakiwa kutoka nje ya uwanja kwa tabia mbaya.
👩Mke: Ahaaa! Sasa atakuwa kocha?
👱🏾♂️Mume: [hajisikii kujibu] Aaaaa hapana...
👩Mke: Ni kama taa za barabarani: njano = onyo; nyekundu = hatari.
👱🏾♂️Mume: Ndiyo mpenzi...
👩Mke: Na kijani inamaanisha nini?
👱🏾♂️Mume: Mmmm hakuna kitu kama hicho uwanjani...
👩Mke: Nataka Arsenal ishinde Kombe la Dunia...
👱🏾♂️Mume: [kimya kabisa]
👩Mke: Huyo jamaa aliyesimama anafanana na Mr. Bean ni nani?
👱🏾♂️Mume: [amechoka kabisa] Huyo ni kocha wa Arsenal... Arsene Wenger.
👩Mke: Basi kocha wa timu pinzani anaitwa Manchester Wenger?
👱🏾♂️Mume: [anabadilisha chaneli kuwa Zee World ili apate amani] 😂😂😂