JF Freestyle battle special thread

Comments by my man Zion got me loughing,
they aim at those faking,
my weed in the getto got me coughing,
my enemies in the streets got me punching,
my b**** got me screaming,
I got my niggas in the back,
dont be mistaken am smart,
got seven souls like a cat!
 
Mistari imesimama, nami sintolala
Majukumu kutuandama, kama msala
Nguli umerindima, kama mnyapala
Wengine kulalama pasipo mshahala
Mistari imesimama nami sintolala

Kimyakimya kama Jaymo, msituni ninatoka
Pasipo msimamo, kwenye mashindano nitatoka
2010 mwaka wa kikomo, mliong’amua mmeng’atuka
Natamani kwanza kilimo, mifuko imetoboka
Wanoko mmekula omo, watanashati mnawika

Mzima bado naishi, Jamvini nimepamisi
Wote nimewamisi naye Sishi, siku yoyote kurudi hata Alhamisi
Xpin, Nguli, Fidel, ZD, Kaizer, Geoff, bht kwa amani muishi, wengine nimewamisi
Nimebanwa na kazi ili niishi, hakika sintoweza kuwadisi
Kijijini ndiko ninakoishi, siku ikiwadia upepo wa bahari nitauhisi
 
sipo unatisha nimekumiss ile mbaya
tutakamatana siku moja ukiwa dar
tupopamoja mpwa tutaonana inshallah
unafanya nini kijijini na hukuaga?
au kimya kimya umeamua kwenda kuoa?
nakupongeza tena sana kwa kuvuka huu mwaka
maisha yanasonga siku moja tutafika
mwisho kazi njema mwombe mungu tasaidia
 

Sipo nimekumis ile mbaya mwanangu
nimepm watu kukulizia wakadia unaishi kibangu
Kibangu? sidhani kwani wewe unakula machangu,
nashukuru kunijuza u'mbana na ya dunia machungu,
chanagamoto zako nimezimis hakika ww ni jungu,
waswahili wanasema halikosi ukoko hata yawepo mawingu.
 
washkaji zangu naomba tuwekane wazi
hapa tulikuwa tunaflow kwa maana ya kubrainstorm akili zetu
i know kuna maeneo mengi ambayo ''tumepishana'' ki-mitizamo...!ukiangalia hizo verse utagundua kitu fulani.lakini naomba nitoe msimamo wangu kwamba I WAS JUST TYPING,sitegemei bifu (nimegundua kuna kila dalili za bifu).

PEACE AND LOVE PEOPLE!
LOVE YOU ALL
 

Unataka battle bila bifu, taji bila uchifu?
Kujitamba double difu kwa mistari hafifu?
Unatutia kifu kwa uhalifu ulokosa ubunifu
Kaa chonjo usifu, ushakosa uaminifu
 
Hapa bado sana vijana.

Jina lako kiranga labda ni tafsiri mbadalaya ya kifaranga,
fikra zako unazitoa kafara kama mchangani kumwaga karanga,
Sawa tunakiri hapa bado sana wewe toa lako kali
Kulalama ni yetu kawaida na ni wagumu wakutofikili
 

Jibu liko hapa

 
Whooo a.... chacha, zigzig da, who aah.
ayori yori
 
hakika Jf ina marijali

JF imejaaliwa marijali hadi mabikira
Wanaojali wasiojali hadi wenye papara
Kila siku wanajisajili kuanzia Rukwa hadi Mara
Wenye macho wamejistili hadi wamejizingira

JF ni mswano ila akili kumkichwa
Waweza kula vinono ila vichungu kama mchwa
 
Jina lako kiranga labda ni tafsiri mbadalaya ya kifaranga,
fikra zako unazitoa kafara kama mchangani kumwaga karanga,
Sawa tunakiri hapa bado sana wewe toa lako kali
Kulalama ni yetu kawaida na ni wagumu wakutofikili

Kiranga ndio nani, labda unambie kifaranga
hana tena thamani, kama faranga ya ufaransa,
faragha ndio yamlinda la sivyo angedhalilishwa
sasa kazama machimboni mafichoni kusaka kamusi
hana lolote kaishiwa kasepa kumkwepa freestyle king
omega psi phi i'm the king of freestyling
 
kurudi nitarudi wallahi tena sintokufa
majukumu kuzidi ndio kuukimbia ulofa
nakutakia heri zaidi ufanye shughuli ilo na sifa
 
Jina lako kiranga labda ni tafsiri mbadalaya ya kifaranga,
fikra zako unazitoa kafara kama mchangani kumwaga karanga,
Sawa tunakiri hapa bado sana wewe toa lako kali
Kulalama ni yetu kawaida na ni wagumu wakutofikili

Kwanza 'takufanza kipigo ka danadana
Mpaka ujibanze uniite "bwana bwana"
Nanza stanza mpaka Mwanza, we bado "Mama na Mwana"
Si saizi yako hii namba pana
Mashairi dhahiri ya kukufunza staili stahili
Yamwagika bila bahili kutoka langu faili saili
Tiririka kama Naili, kukupa lile na hili
Kuzungusha ka- tairi, kabla sijapo ghairi
Kaa chini, na sikiza utabiri tahriri
Lugha inayo tahiri na taahira ku-tahdhiri
Kama imam takdiri, kama vingine injili
Au hata vipingili vya Sangoma Ikwiriri
Nimevuka mito na kudinya wingu
Njoo anga zangu ntakupiga pingu
Na kulipua fataki, taka hutaki
Halafu ndugu zako waokote mabaki
Nitapokurarua kama vijana wa Iraki
Vita nimepita ka Cheetah nikakita
Sintosita kukucharaza ka gita
Kukuponda ka siafu, nikuombee kwa misahafu
Talmud,Torah Bhagavad-Gita
Niku.... aaaahhh

Bado unataka tu?
 
kurudi nitarudi wallahi tena sintokufa
majukumu kuzidi ndio kuukimbia ulofa
nakutakia heri zaidi ufanye shughuli ilo na sifa
hakika nimekukubali watisha kama gharika
kuishi ni majaaliwa hakuna anaependa kufa
jitume katika kazi utapata maisha bora
upatapo japo kidogo wakumbuke baba na mama
hao ni watu muhimu wastahili bakshishi yako kupata
wapwao tunakumisi kila la kheri twakutakia
 

Kiyana bado sana
Look i'm a chrystal nigga and you a red winer
You just an opening act and i'm the headliner
so homeboy step your game up or get lost
 
Nguli hamasa umenitia jamvini nikajisimika
Yako mashairi ujasiri yamejitia na kusitirika
Manani kipaji amekutia nawe umekubalika
 
Nguli hamasa umenitia jamvini nikajisimika
Yako mashairi ujasiri yamejitia na kusitirika
Manani kipaji amekutia nawe umekubalika

Thanks man wherever ur usinisahau mimi,
yeyote utakayekutana naye usisahau upo ukimwi,
Soma sana mwana usijali ugumu wa skim,
If am not reachabo napatikana www. yetu jamii,
Sala zidisha na tuombeane mazuri kwa imani.
In God willing tuonane kesho morning
 
Kiyana bado sana
Look i'm a chrystal nigga and you a red winer
You just an opening act and i'm the headliner
so homeboy step your game up or get lost

Vua gamba,
Ni kwamba unatamba? Kwa mashairi ya za viatu kamba?
Yasiyofika liyamba yasowekeka sambamba
Ni ubahili au huna staili?
Au huwezi kwenda na vibweka vyangu vilivyojaa kwa paili za maili?
Ustake nlete gharika, utaghafirika
Nakupa kipigo fika katika lugha ya mwafrika
We nenda kaibie, wakakusaidie
Kipigo pale pale mpaka wende ujifie
Jaribu kuleta vina vyenye usawia na uzito
Si mizani hafifu ya medani za kibitoz
Ntakukoa vikonzi, kwa vina vingi kama dozi za ponzi
Mpaka ulielie kama JD na machozi
Hatutaki gozigozi, nenda karudi kozi
Ustake kututisha kwa yako feki mapozi
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…