Horseshoe Arch
JF-Expert Member
- Aug 10, 2009
- 13,402
- 12,787
Sijui kwanini bado Kikwete ni Mkuu wa nchi,sijui kwanini Ofisi ya waziri Mkuu ipo,Sijui kwanini serikali bado ipo madarakani,sijui kwanini kitengo cha Usalama wa Taifa Kipo,Sijui nani ameloga Watanzania na Taifa kwa ujumla! Kwa hali ya mambo ilivyo sasa nadhani ni wakati sasa wa serikali kukasimisha madaraka kisheria kisha watendaji wote wawaombe radhi wananchi,kisha waburuzwe mahakamani na baada ya kesi zao kuisha wafilisiwe mali zao kasha tukiona inafaa tuwatenge kabisa ama watafutiwe pori waishi huko.