Jeshi la polisi, shame on you!!

Jeshi la polisi, shame on you!!

Hii siyo sawa kabisa.

Inaenda kukaribia miezi sita sasa tokea Tundu Lissu anusurike katika shambulizi la kutaka kumuua.

Tukio lilitokea mchana kweupe, tena kwenye makazi ya viongozi waandamizi wa bunge na serikali.

Cha ajabu kabisa [at least kwangu mimi], hakuna hata updates kutoka kwa jeshi la polisi kuhusu huo uchunguzi umefikia wapi.

Hata kutaja person of interest hakuna! Kutaka suspect hakuna!

Sasa watu tuwafikirieje hao polisi?

Au ni mimi tu ambaye sijui kuwa wanatoa updates?

Huu ukimya wa polisi unatoa uhalali kwa tuhuma za uhusikaji wa serikali katika zoezi zima.

Ajabu kabisa!!!
Wewe utakuwa unamjua mhusika, utaisaidia polisi.


Hahahaaa NN bwana!
 
Hayo mashambulio na mauaji mbona ni vitu dogo na vya kawaida tu!!
Hata Ulaya na America mambo haya yanatokea sana. So tusiyakuze kiviile...

Anyway, sijui kama ni kuyakuza au kukosa ufahamu na maarifa wa kuyashughulikia.

Nakubaliana nawe kuwa mauaji si mambo mageni duniani, kila siku yanatokea, sehemu nyingi duniani yanafanyika, ndio maana hats sinema nyingi pendwa na maarufu duniani ni za mauaji na ma star maarufu duniani wengi wao ni wanaofanya mauaji.

Mauaji yana sababu nyingi. Mfano katika sinema tuziangaliazo na kuzipenda sana sababu zinaweza kuwa ukombozi, usaliti, kudhulumiana, wizi, kuzuia siri isitoke, kuzuia haki isitendeke, mapenzi na adhalika na kadhalika.

Mauaji yapo, yamekuwepo na yataendelea kuwepo kwani mauaji ni sehemu ya dunia, sehemu ya maisha ya binadamu ndio maana viwanda vikubwa kuliko vyote duniani ni vya kutengeneza silaha za kumuulia binadamu.

Ajabu kubwa ni pale binadamu wanapolalamika eti silaha zilizotenenezwa kumdhuru na kumuua binadamu zimetumika kufanya hivyo.

Mauaji yasichuliwe kama kitu kigeni na cha ajabu, mauaji yapo, yanajulikana. Kitu cha muhimu kinachopaswa kifahamike ni sababu ya mauaji.

Kumuua muasi ni kumuua adui, na muasi kumuua mwanajeshi wa serikali ni kumuua mpiganaji wa wagandamizaji.

Jeshi kumuua informer hata kama ni ndugu yenu ni kumuua msaliti.

Ukimuua nduguyo kwa bahati mbaya katika mapigano huo ni moto wa kirafiki (Friendly fire)

Wapo wanaoua kwa kutimizwa matakwa yao binafsi, hao ni wauaji. Kila mmoja wetu anatakiwa alifahamu hilo, achukue tahadhari, ajilinde na ndio maana tunaishi mbali na wanyama wakali, tunajenga nyumba na kuweka ulinzi kujilinda. Jamii nzima inapaswa kujilinda na watu hawa na pindi wanapotambulika adhabu kali huchukuliwa dhidi yao.

La muhimu ni kufahamu unasaini kwa kitu gani. Ukisaini kuwa mwanajeshi, ukisaini kuwa mpiganaji umesaini na kukubali kufa endapo adui atakuzidi nguvu na maarifa.

Ukipita chaka la chui tambua chui wakikuzidi nguvu nini kitatokea.

Ukihifadhi milioni 900 ndani halafu ukamwambia mkeo autangazie umma jiandae kwa lolote.

Kama mitume na wasomi wazuri kama Galileo Galilei waliadhibiwa na kuuliwa kwa kusema ukweli na kuleta maarifa mapya basi wanaoamini katika kweli na kusema ukweli nao wafahamu fika wanasaini kwa kitu gani.

Mauaji sio mapya hayakuanza leo, yameanza toka kwa watoto wa Adam na Hawa, Cain na Abel.

Kweli tutaangamia kama tutakosa maarifa.
 
Hii siyo sawa kabisa.

Inaenda kukaribia miezi sita sasa tokea Tundu Lissu anusurike katika shambulizi la kutaka kumuua.

Tukio lilitokea mchana kweupe, tena kwenye makazi ya viongozi waandamizi wa bunge na serikali.

Cha ajabu kabisa [at least kwangu mimi], hakuna hata updates kutoka kwa jeshi la polisi kuhusu huo uchunguzi umefikia wapi.

Hata kutaja person of interest hakuna! Kutaka suspect hakuna!

Sasa watu tuwafikirieje hao polisi?

Au ni mimi tu ambaye sijui kuwa wanatoa updates?

Huu ukimya wa polisi unatoa uhalali kwa tuhuma za uhusikaji wa serikali katika zoezi zima.

Ajabu kabisa!!!

Kaka kuna kitu unapashwa kuelewa, Polisi wa Tanzania ni jeshi linalofata maelekezo nini cha kufanya, Polisi wa Tanzania wote wanasoma Vyuo hivyo hivyo CCP na Kurasini, lakini unaweza kuona tofauti kubwa ya Polisi wa Enzi za Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete na hawa wa Sasa Wa JPM,
 
Sasa ni zamu yenu watangnyika kuuwana kudadeki, wazanzibar washauliwa sanaaa na hili lichama sasa limewageukia nyinyi wenyewe.
 
Mkuu ndio maana wakati wabunge wa Chadema wanamshangilia Kikwete wengine tulishangaa mno!!! Unajua upinzani haujielewi na mbaya zaidi watu kama nyie ambao ni great thinker mmeamua kuwaunga mkono tuuuu hata pale wanapohitaji kukosolewa! Ndio maana sasa tunakula fimbo bila huruma na hatuwezi hata kuvuta nguvu ya umma against it ....very very bitter truth ambayo hamtaki tuseme ....tuna kazi ya kujipanga upya ...

..ni kweli cdm walikosea mahesabu na kumsimamisha Lowassa kama mgombea wao.

..yuko aliyewaaminisha kwamba hawezi kushinda ikiwa kampeni na mgombea wao watajikita kwenye hoja ya ufisadi.

..sasa hayo yameshapita hatuwezi kulilia maziwa yaliyokwisha mwagika.

..chama inabidi kijipange upya. Kinatakiwa kiibue hoja mpya ambazo wataweza kuzisimamia mpaka wakati wa uchaguzi na ikiwezekana beyond that.

..Hata ccm wana survive kwa mambo mengi, lakini moja wapo ni uwezo wao wa kubadilika kulingana na mazingira.

..Wakati wa Mwalimu Nyerere ccm walikuwa wakihubiri "ujamaa na kujitegemea." Sasa hivi wanahubiri " hapa kazi tu. " kwa hiyo utaona wanabadilika kila baada ya kipindi fulani.

..sasa cdm nao inabidi wabadilike kulingana na mazingira na matarajio ya waTz wa sasa hivi.

NB.

..Kuhusu matukio ya kikatili dhidi ya wanachama wao ni kweli cdm wana wajibu wa kupaza sauti kubwa zaidi.

..wapo wanachama wengi wameumizwa na sasa imehamia kwa viongozi wa chadema.

..chama kinapaswa kuwasemee na wale ambao wameumizwa lakini kwasababu majina yao siyo makubwa taarifa zao hazijulikani.
 
..ni kweli cdm walikosea mahesabu na kumsimamisha Lowassa kama mgombea wao.

..yuko aliyewaaminisha kwamba hawezi kushinda ikiwa kampeni na mgombea wao watajikita kwenye hoja ya ufisadi.

..sasa hayo yameshapita hatuwezi kulilia maziwa yaliyokwisha mwagika.

..chama inabidi kijipange upya. Kinatakiwa kiibue hoja mpya ambazo wataweza kuzisimamia mpaka wakati wa uchaguzi na ikiwezekana beyond that.

..Hata ccm wana survive kwa mambo mengi, lakini moja wapo ni uwezo wao wa kubadilika kulingana na mazingira.

..Wakati wa Mwalimu Nyerere ccm walikuwa wakihubiri "ujamaa na kujitegemea." Sasa hivi wanahubiri " hapa kazi tu. " kwa hiyo utaona wanabadilika kila baada ya kipindi fulani.

..sasa cdm nao inabidi wabadilike kulingana na mazingira na matarajio ya waTz wa sasa hivi.

NB.

..Kuhusu matukio ya kikatili dhidi ya wanachama wao ni kweli cdm wana wajibu wa kupaza sauti kubwa zaidi.

..wapo wanachama wengi wameumizwa na sasa imehamia kwa viongozi wa chadema.

..chama kinapaswa kuwasemee na wale ambao wameumizwa lakini kwasababu majina yao siyo makubwa taarifa zao hazijulikani.
Tatizo liko hapo ...hii kutaka mambo yapite kirahisi ndio pia yanayowafanya mumshangilie JK kirahisi na kusahau mapito yote ...mmefanya JPM anahisi mtamkumbuka tu maana mlijiapiza uadui kwa JK pia .....mnashangilia michango ya kina Bashe bungeni huku mnasahau kuwa ukija uchaguzi CCM wanaongea lugha moja ....mkianza kuwajibishana ndani kwa makosa ya kipuuzi kama yale ambayo mwenyekiti alijiapiza ndio mtaweza kuwa na ujasiri wa kupambana na CCM ....Leo ndani wote mnamuogopa Mbowe ....alafu mnataka ujasiri kwa JPM!!! ....Tuache kudanganyana ...tuanze kuambizana ukweli ili kila anayeamua kusimama na mageuzi awe amejikana kwelikweli ....
 
naona umeamua kua kama kigwangala.unajamba nakuwahi kuwasha feni chap
waziri Kigwangala akijamba ofisini mgeni akaingia ghafla anawasha feni na kusimama akijifanya anapanga panga mafaili au anamfata mgeni mlangoni mange kimambi sio wa mchezo
 
Wewe unayejiita Msimamo ni kwa nini unadhani kuwa jambo la serikali kutojali mauaji ya watu ni jukumu la upinzani. Wewe una akili sawa kweli ama unadhani hii hali ya sasa ya siasa ni nzuri kwa maendeleo ya taifa?
Ushabiki mwingine unatia hasira sana. Wewe umeona picha ya jinsi alivyokatwakatwa yule diwani wa Morogoro.
Kila siku mnaongelea uzalendo. Ni mwananchi yupi atakayekuwa na uzalendo kama anashindwa kuona serikali isivyodhamini watu wake!
Wake up and grow up usahau kupalilia tumbo kwanza.
RIP WOTE MLIOUAWA NA MAJASUSI YA NCHI HII!
 
Kuna wananchi wengine pia nchini nao wapo boti moja na Lissu..
Nao ni wananchi wanaotaka haki itendeke.. wanasubiri muda zaidi ya ya Lissu ambae pia ni mwananchi kama wengine.

Tuache polisi wafanye kazi yao..
 
Utendaji wetu [kwenye karibu kila nyanja] ni mbovu sana.
Mimi hili nimewahi liona siku nyingi sana. Watu wengi tuliowapa dhamana ya uongozi ni vilaza kabisa. Creativity hawana. Wengi wanazidiwa na makonda, ukiweka kando tuhuma zake za ovyo ovyo
 
Back
Top Bottom