G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 12,416
- 39,521
Ni vyema jeshi la polisi likaachana sasa na propaganda zisizo na maana. Walitaka kumalizana na dereva wa Tundu Lissu wamewahiwa.
Nawasihi wautumie muda huu mfupi vizuri kuachana na ulaghai la sivyo watu wakitoka Nairobi jeshi hili tulilokosa nalo imani litaumbuka vibaya! Waache kujiumauma na watende haki. Wasiendelee kulimbikiza vinyongo ambavyo siku ikifika watu watavitapika waziwazi na hapo hakutakuwa tena na subira!
Mimi nawakumbusha tu kuwa bado muda wa kujisahihisha wanao kwa kuamua kuhusu hili sakata la Tundu Lissu!
Nawasihi wautumie muda huu mfupi vizuri kuachana na ulaghai la sivyo watu wakitoka Nairobi jeshi hili tulilokosa nalo imani litaumbuka vibaya! Waache kujiumauma na watende haki. Wasiendelee kulimbikiza vinyongo ambavyo siku ikifika watu watavitapika waziwazi na hapo hakutakuwa tena na subira!
Mimi nawakumbusha tu kuwa bado muda wa kujisahihisha wanao kwa kuamua kuhusu hili sakata la Tundu Lissu!