Wakuu habari,
Tufuatilie live ya Jeshi la Polisi ikitoa tamko kuelekea kampeni za vyama vya siasa inayotarajiwa kuanza kesho Agosti 28, 2025
View: https://youtu.be/oMKspe2-o1Y?si=K58UWSQsgIJMBPg7
Msemaji wa Jeshi la Polisi David Misime: " Kesho Agosti 28, 2025 kama ilivyotangazwa na Tume huru ya Taifa Uchaguzi INEC Kampenin za wagombea za nafasi za Urais, Ubunge na Udiwani zinaanza rasmi. Jeshi la Polisi Tanzania lingependa kuwajulisha wananchi na wadau wote kuwa liko tayari na limejipanga vizuri ipasavyo kuhakikisha tunaendelea kuimarisha usalama wakati wote wa kampeni na baada ya kampeni
Aidha Jeshi la Polisi linatoa wito kwa wagombea na wafuasi wao na wananchi wote kwa ujumla kukumbuka kuwa jukumu la kudumisha amani, utulivu, usalama ni letu sote kama watanzania na kamwe asiwepo mmoja wetu akawa chanzo cha kukiuka sheria, kanuni na utaratibu wakati wote wa kampeni na baada ya kampeni ili kuepuka vurugu au uhalifu wa aina yoyote kutokea.
Pia tunatoa wito kila mmoja azingatie ratiba na muda wa kampeni aliyopangiwa ili kuepeuka mivutano, migongano, migogoro au uhalifu kutokea kwani hatutasita kuchukua hatua kama sheria za nchi zinavyoelekeza"
Tufuatilie live ya Jeshi la Polisi ikitoa tamko kuelekea kampeni za vyama vya siasa inayotarajiwa kuanza kesho Agosti 28, 2025
View: https://youtu.be/oMKspe2-o1Y?si=K58UWSQsgIJMBPg7
Msemaji wa Jeshi la Polisi David Misime: " Kesho Agosti 28, 2025 kama ilivyotangazwa na Tume huru ya Taifa Uchaguzi INEC Kampenin za wagombea za nafasi za Urais, Ubunge na Udiwani zinaanza rasmi. Jeshi la Polisi Tanzania lingependa kuwajulisha wananchi na wadau wote kuwa liko tayari na limejipanga vizuri ipasavyo kuhakikisha tunaendelea kuimarisha usalama wakati wote wa kampeni na baada ya kampeni
Aidha Jeshi la Polisi linatoa wito kwa wagombea na wafuasi wao na wananchi wote kwa ujumla kukumbuka kuwa jukumu la kudumisha amani, utulivu, usalama ni letu sote kama watanzania na kamwe asiwepo mmoja wetu akawa chanzo cha kukiuka sheria, kanuni na utaratibu wakati wote wa kampeni na baada ya kampeni ili kuepuka vurugu au uhalifu wa aina yoyote kutokea.
Pia tunatoa wito kila mmoja azingatie ratiba na muda wa kampeni aliyopangiwa ili kuepeuka mivutano, migongano, migogoro au uhalifu kutokea kwani hatutasita kuchukua hatua kama sheria za nchi zinavyoelekeza"