minyoo
JF-Expert Member
- May 25, 2013
- 21,640
- 20,366
zinepita saa 48 cha ajabu Polisi wanatoa vioja kuwa bado wanafanya uchaguzi, ujue polisi wengi hawana vyeti wanafanya kazi kwa kujipendekeza sio kwa mujibu wa sheria za Nchi, Lisu hana kosa yy katumia haki yake kumkosoa Mtukufu malaika wa chato ambaye amebaka Demokrasia kwa kuwabambikia kesi kuwakomoa kuwadhalilisha na kuwaonea Wapinzani, ulitaka Lisu atumie njia ipi kumwambia magufuli Ukweli? njia zote wametumia lakini magufuli Mtukufu hataki kuacha Udikteta lazima lisu apaze sauti ulimwengu ujue Mtukufu ni Dikteta, wanasheria wanajua sasa Tanzania hakuna haki na hao ndiyo walimshauri ajitoe mhanga amchane Live Mtukufu malaika toka chato ingawa walijua atatumia polisi kumbambikia kesi kibao ikiwemo mbinu ya Bashite na le mutuz kuandaa maji na chakula chenye dawa za kulevya kupeleka rumande alishwe Lisu kisha akapimwe mkojo wapate kumbambikia kesi ya Unga, Mungu hapendi ndiyo maana siri zimevuja japo wapanga njama ni vilaza pia.Wangekuwa na busara basi wangeanza kumuonya Lissu kwamba kutumia lugha ya ukali, kashfa, dharau na kuudhi si njia sahihi katika kudai anachokiita haki. Kama ni sheria inavunjwa basi inadaiwa kwa kutumia njia sahihi za kisheria na si kama anavyofanya. Na pia Lissu kuwa Rais wa TLS hakumfanyi kuwa juu ya sheria. Akikosea anashughulikiwa kama kawaida. Lakini pamoja na yote hao wanasheria wenzake wamesahau kuwa sheria inawaruhusu polisi kumshikilia mtuhumiwa kwa zaidi ya masaa 48 ikiwa tu wataona kuna ulazima wa kufanya hivyo.