Waziri wa madini
JF-Expert Member
- Jun 12, 2019
- 379
- 465
Mbunge wa Jimbo la ukonga Jerry silaa kumbuka ahadi zako ulizozitoa wakati wa kampeni,kumbuka jinsi ulivyopigana na kupiganiwa ili kupata ubunge wa ukonga. Kumbuka wananchi wa ukonga wanakutazama na wanasubiria utekelezaji wa ahadi zako.
Tangia uapishwe kuwa mbunge hujawahi kuitisha mkutano wowote katika Jimbo lako kujadili changamoto zinazowakabili na jinsi ya kuzitatua,hujawahi kuonekana hata siku moja bungeni ukichangia hoja zinazo husiana na kero pamoja na changamoto za wakazi wa Jimbo lako la ukonga.
Ushauri wangu kwako bado mapema sana ila tunakukumbusha kuwa Jimbo unaloliongoza ndio linaongoza kwa changamoto ya miundombinu kuliko sehemu yoyote ya mkoa wa Dar Es Salam,Jimbo unaloliongoza ndio linaongoza kwa shida ya maji japokuwa mradi wa maji umezinduliwa lakini kunaurasimu mkubwa kwenye usambazaji wa maji hayo,kumbuka Kuna ahadi nyingi ulizitoa wakati wa kampeni.
Kuwakimbia wapiga kura wako mapema hivi unajiweka hatarini Sana kuja kutetea nafasi yako ya ubunge.
Mheshimiwa Silaa tumekuona unachangia hoja za kutetea ndege za Magufuli umefanya jambo zuri kumtetea mpendwa wetu na kuchambua ukweli kuhusu ATCL lakini kumbuka Kuna kazi uliyotumwa na wakazi wa ukonga mbona huifanyi kwanini huwasemei?
Nakuomba hebu siku moja jaribu upite barabara ya majohe ,viwege hadi mbondole uone maisha ya wakazi wa ukonga yalivyo hatarini barabara haipitiki kabisaa mbaya mbovuu ,mbunge upo na barabara ipo katika ilani ya uchaguzi 2020-2025 lakini mbunge umekaa kimya tu barabara inamashimo haipitiki .
Mwisho kumbuka Kura za wanaukonga ulizopewa kuwa na utu na ukumbuke ulipotoka.
Tangia uapishwe kuwa mbunge hujawahi kuitisha mkutano wowote katika Jimbo lako kujadili changamoto zinazowakabili na jinsi ya kuzitatua,hujawahi kuonekana hata siku moja bungeni ukichangia hoja zinazo husiana na kero pamoja na changamoto za wakazi wa Jimbo lako la ukonga.
Ushauri wangu kwako bado mapema sana ila tunakukumbusha kuwa Jimbo unaloliongoza ndio linaongoza kwa changamoto ya miundombinu kuliko sehemu yoyote ya mkoa wa Dar Es Salam,Jimbo unaloliongoza ndio linaongoza kwa shida ya maji japokuwa mradi wa maji umezinduliwa lakini kunaurasimu mkubwa kwenye usambazaji wa maji hayo,kumbuka Kuna ahadi nyingi ulizitoa wakati wa kampeni.
Kuwakimbia wapiga kura wako mapema hivi unajiweka hatarini Sana kuja kutetea nafasi yako ya ubunge.
Mheshimiwa Silaa tumekuona unachangia hoja za kutetea ndege za Magufuli umefanya jambo zuri kumtetea mpendwa wetu na kuchambua ukweli kuhusu ATCL lakini kumbuka Kuna kazi uliyotumwa na wakazi wa ukonga mbona huifanyi kwanini huwasemei?
Nakuomba hebu siku moja jaribu upite barabara ya majohe ,viwege hadi mbondole uone maisha ya wakazi wa ukonga yalivyo hatarini barabara haipitiki kabisaa mbaya mbovuu ,mbunge upo na barabara ipo katika ilani ya uchaguzi 2020-2025 lakini mbunge umekaa kimya tu barabara inamashimo haipitiki .
Mwisho kumbuka Kura za wanaukonga ulizopewa kuwa na utu na ukumbuke ulipotoka.