Waziri Jerry Silaa aigiza Wizara ya Ardhi Kitengo cha Upimaji na Ramani kupima kila kipande cha ardhi nchi nzima

ChoiceVariable

JF-Expert Member
May 23, 2017
43,076
49,774
Waziri wa Ardhi na Nyumba ameagiza Nchi nzima ipimwe.

Moja ya shida kubwa kabisa ya Tanzania ni ujenzi holela na Nchi inakuwa kama dampo Kwa kujaaa ma slums na mabanda Kila sehemu.


My Take:
Peleka Kwenye Balaza la Mawaziri pendekezo la kuunda Mamlaka au Wakala wa Mipango Miji na Matumizi Bora ya Ardhi (Urban planning & Land administration Agency).

Wakala huyo ndio atafaulu kupima Nchi nzima dizaini ya Luwasa, Tarura nk.

=========

Waziri mpya wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ambaye pia ni Mbunge wa Ukonga Jerry Silaa amemtaka Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani kuja na mpango wa kuipima Nchi nzima ya Tanzania pamoja na kuwasilisha ‘case study’ ya Nchi zilizofanikiwa kwenye eneo hilo.

Waziri Silaa ameyasema haya leo kwenye siku yake ya kwanza Wizarani hapo wakati akiweka wazi Vipaumbele vyake 12 atakavyovifanyia kazi kama Waziri mwenye dhamana (video nzima ya tukio hili ipo kwenye Youtube ya millardayo ).

“Mara ya mwisho sheria za ardhi zimefanyiwa marekebisho mwaka 2019 na leo ni 2023 hakuna jinsi kwa miaka hii minne hizi sheria zipo ‘valid’ kwa asilimia 100 lazima kuna mambo yamejitokeza hapa katikati kwahiyo sheria zote zikiwemo sheria za nyumba ambazo zinakwamisha, tukikutana tuzungumze tutengeneze mchakato wa kurekebisha sheria, Bunge lipo.

”Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani tukikutana uje na mpango wa kupima hii Nchi, hii Nchi nzima ipimwe na uje na ‘case study’ ya Nchi zilizofanikiwa, ukishapima ukawa na mfumo madhubuti wa ki-digitali tukija hapa miaka mitano baadae kuna baadhi ya idara zitafungwa na neno mgogoro litakuwa halipo tena”
Screenshot_20230905-114924.jpg
 
Waziri anatoaje maelekezo wakati hajasema pesa ya budget itatoka wapi...??
Au anadhani kutoa tamko ndio wanachi tutamuona mchapa kazi...!!
Hii wizara alie jaribu kuiweza ni Lukuvi tu, tena alianza kufanikiwa kwasababu hakukaa ofisini, alikua mfuatiliaji na hakua mtu wa kutoa maagizo.
 
Waziri anatoaje maelekezo wakati hajasema pesa ya budget itatoka wapi...??
Au anadhani kutoa tamko ndio wanachi tutamuona mchapa kazi...!!
Hii wizara alie jaribu kuiweza ni Lukuvi tu, tena alianza kufanikiwa kwasababu hakukaa ofisini, alikua mfuatiliaji na hakua mtu wa kutoa maagizo.
Nakwambia hawa viongozi wetu wqnashida sana,ni full kukurupuka,mchakato mzima unahitaji pesa,harafu anakuja na matamko utadhani kabla ya kupewa uwaziri alikuwa nchi za nje kwamba haijui hali ya nchi yetu
 
Hawa vijana huwa akili wanapelekaga wapi wakishasoma hayo madegree na kupata makaratasi?
Stupid kabisa...anamuagiza nani sasa.
No Plan, No strategy, No manpower, no budget...nothing. unatoa tamko tu.
 
Huu jamaa nimemsikiliza akiongea kwenye hiyo meeting leo, anaonekana ni smart na anaelewa kazi yake, tumpe muda kidogo, i was impressed na record yake ya ukusanyaji wa pesa alipokuwa meya wa ilala, anaonekana sio mjinga
Apunguze papara.Ni kweli Yuko smart ila apunguze papara
 
Watu wanaishi mjini , hifadhi za barabara hakuna, hakuna sehemu za kupita watoto pindi waendapo shule, hakuna sehemu za watembea Kwa miguu, ni Bora Kuwe slums halafu hifadhi za barabara ziwepo!! Sasa unakaa na kufikiria kazi ya viongozi ni nini!? Wizara ya ardhi inafanya nini!? Nini umuhimu wake!?
 
Mheshimiwa Waziri
Acha mbwembwe !
Pesa ya kupima kila kipande cha radhi iko wapi ??
Leo hii mmewaachia watu wanapima maeneo na kuwauziwa wengine kwa bei kubwa wanatengeneza pesa nyie mmelala usingizi mnono!!!! kwa mfano huko Kimbiji kuna dalali mwanamke anapima na kuwauzia wananchi!!! serikali inashindwa nininiii ???
 
Back
Top Bottom