Anaandika Jerry C. Muro
[HASHTAG]#Taifa[/HASHTAG] la Tanzania limeingia katika Historia ya Dunia Kufuatia Kampuni ya _Barrick Gold_ kukubali kwa mara ya kwanza Kugawana asilimia hamsini kwa hamsini *50/50* ya Faida katika uzalishaji wa Dhahabu nje ya *Asilimia 16* ya Mrahaba na Kodi ambayo taifa itapata.
[HASHTAG]#Nimedadisi[/HASHTAG] katika nchi mbalimbali ambazo Barrick wamefanya uwekezaji kama huu na kugundua Tanzania ndio nchi *PEKEE* ambayo *IMETHUBUTU* na kufanikiwa katika hili, Hongera Tanzania Hongera Rais Mzalendo *Mhe, Dkt. John Pombe Magufuli* katika kurekebisha kwa vitendo makosa ya watangulizi wako, huu ndio Uongozi *UNAOACHA ALAMA* tukufu, naamini kwa sasa watangulizi wako wanafuraha kubwa ya kuona umesahihisha kwa vitendo pale walipokosea.
[HASHTAG]#Muafaka[/HASHTAG] Baina ya Tanzania na Barrick umewaacha "UCHI" tena nasisitiza "*UCHI WA MNYAMA* " wale wote waliokuwa wakisubiri Tanzania ipelekwe mahakama ya kimataifa kutokana na kuchukua hatua za kuzuia MAKINIKIA, kwangu nasema *SHAME ON YOU!!!* najua wamenielewa na wamesikia, Leo Tanzania imepata Shilingi Bilioni 700 kama hela tu ya kujenga *UAMINIFU*, bado nasubiria tupate kodi yetu, tupate Mrabaha wetu, kisha tugawane faida hamsini kwa hamsini.
[HASHTAG]#Nimefarijika[/HASHTAG] sana na kauli ya Mhe Rais, *Dkt. John Pombe Magufuli* ya kuwataka wawekezaji wengine *WOTE* katika Sekta ya Madini kujitafakari na kuanza kufuata uelekeo wa makubaliano kama Haya na Barrick, sasa tutaanza kuvuna neema kwenye Tanzanite, Almasi na kisha tutaingia kwenye Gesi na Mali asili zingine, Haya ni mafanikio makubwa katika kipindi cha takribani miaka miwili ya Uongozi wa Mhe Magufuli, naamini akimaliza miaka Mitano ya kwanza na ile mingine lazima Tanzania tutakuwa "*Donor country*"
[HASHTAG]#Naomba[/HASHTAG] nimalize kwa kufikisha salamu kule Nairobi, mwambieni kulikuwa na sababu ya Mungu kumuweka hai ili aje ashuhudie ukuu wa Mungu kupitia Mhe Magufuli, lile alilosema haliwezekani kwa sasa *LIMEWEZEKANA* na Hatimae Mhe Magufuli ameibuka shujaa na kinara wa kielelezo cha Rais Bora Africa anaepigania *RASILIMALI* za nchi yake, Mungu alisema Muombee sana "*ADUI* " yako aishi miaka mingi ili Ashuhudie Baraka za Mungu kwako, Hatimae maombi yetu yamejibu sasa.
Wasalamu
*Jerry C. Muro*
*Dodoma, Tanzania*
*20/10/2017*