Mwenyekiti wa Bunge Jenister Mhagama, wakati wa kipindi cha matangazo mbali mbali (kutambua wageni, ratiba za vikao vya kamati n.k.) amesema ana tangazo ambalo amefikiria ameona si vibaya likitangazwa.
"Waheshimiwa Wabunge Kampuni ya AZAM inawatangazia waheshimiwa wabunge kwamba watumie bidhaa za Azam... (kicheko ukumbuni!) ...aidha, AZAM inawatangazia wabunge kwamba bidhaa za AZAM ni bora kwa afya."
Ndugu zangu, hii ni sawa? Serikali (na hususan Bunge) kazi yake moja kubwa ni kusimamia, ku monitor, mienendo ya biashara nchini. Kitendo cha Bunge kutangaza biashara za Bakhressa ni kinyume na maadili ya utawala bora, na si jambo la kufanyia utani na kuchekeshea bungeni. Utawezaje kumratibu mfanyabiashara ambae unamtangazia biashara yake wewe mwenyewe?
AZAM amelipia shilingi ngapi, na wamemlipa nani (Jenister Mhagama?) kutumia muda wa bunge na wa TBC kutangaza biashara? And why AZAM? Kamati ya maadili ya Bunge iko wapi, viongozi wa Bunge mbona mnashusha viwango vya bunge hili namna hii?