MARA NYINGI HUWA IKO HIVI...
- -
Jambazi "wote laleni chini pesa ni za serikali na maisha ni ya
kwenu",wote wakalala chini HII INAITWA DHANA YA
USHAWISHI-kubad -ilisha njia ya kawaida ya kufikiria
- -
Kuna dada kwa woga akawa amelala chini kimitego,
Jambazi "dada embu kuwa na adabu chukua kanga jifunike hili ni
tukio la ujambazi na sio la ubakaji. HUU UNAITWA WELEDI-zingatia ulichofundishwa - kufanya
- -
Walipotoka kwenye wizi jambazi mdogo ambaye ana shahada ya
uzamili ya biashara akamwambia mwenzake,"tuzih -esabu hizi
fedha,yule mkubwa akamcheka kwa dharau na kumjibu,"wewe
mjinga sana hizo hazina haja ya kuhesabu saa mbili watatutangazia
kwenye taarifa ya habari tumeiba kiasi gani. HUU INAITWA UJUZI-Sikuhizi ujuzi ndio bora kuliko vyeti
- -
Baada ya majambazi kuondoka meneja akamwambia mhasibu wa
bank, " ujumlishie na zile milioni 80 tulizo iba sisi". HUKU KUNAITWA KUOGELEA NA MKONDO WA MAJI- kushabiihana na mazingira magumu kwa faida binafsi.
- -
Mhasibu akafurahi na kusema,"dah wizi ukitokea kila mwezi itakuwa burudani sana.
HUKU KUNAITWA KUWA NA MAWAZO CHANYA-Furaha ndio kitu cha muhimu zaidi
- -
Meneja kafurahi sana kwakuwa sasa matatizo yake yametatuliwa na wizi uliojitokeza.
HUKU KUNAITWA KUTHUBUTU-shikilia nafasi pale inapojitokeza hata kama ni hatari kiasi gani
- -
Haya usiku wake taarifa ya habari ikatangaza kuwa wizi mkubwa sana
wa millioni 100 umetokea leo benki kuu, Majambazi kuskia hivyo wakaanza kuhesabu zila pesa lakini
wakajikuta na milioni 20 tu. Yule jambazi mkubwa akashtuka na kusema, "dah! yani meneja kaiba mara nne zaidi yetu bila kuchezesha msuli bora umeneja kuliko ujambazi". HII INAITWA ELIMU- ishike sana elimu inanguvu kuliko dhahabu